Jumapili, 29 Desemba 2013

VYOO VYENYE USIRI VIJIJINI NI TAABU KWELIKWELI



ELIMU ya matumizi sahihi ya vyoo, mashimo ya taka na vichanja, inahitajika zaidi Vijijini ili kupunguza magonjwa ya milipuko.
 
 
Hayo yamebainika katika warsha ya wadau wa mpango wa usafi wa Mazingira(WASH), kutoka wilaya za Mbeya na Mbarali, iliyofanyika eneo la Mbalizi ukumbi wa Tughimbe, uliopo wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani hapa.
 
 
Wadau hao walitembelea katika kata za Ihahi iliyopo wilaya ya Mbarali na kata ya Mshewe iliyopo wilaya ya Mbarali, na kujionea vyoo vya baadhi ya wananchi ambapo walikuta baadhi ya kaya hazina vyoo.
 
 
Katibu tawala msaidizi-Maji, ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhandisi, Fredius Magige, alisema maafisa afya kwa kushirikiana na watendaji wa vijiji na kata, wanatakiwa kupeleka kikamilifu elimu hiyo kwa wananchi mara kwa mara ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji.
 
 
‘’Kwa kuwa imebainika kuwa wahudumu wa afya ya msingi ya jamii(WAV) ni watu muhimu, ni vema wakatumika vizuri lakini kama wanajitolea bila kulipwa hawataweza kufanya kazi zao vizuri’’ alisema Mhandisi, Magige.
 
 
Akiwasilisha taarifa ya utafiti wa kundi la kwanza uliofanyika katika kijiji cha Mjele kata ya Mshewe, Afisa Afya wilaya ya Mbarali, Emedan Mgode, alisema;‘’Kijiji kina kaya 418, katika vyoo, maji na sabuni ya kunawia hakuna na kaya 117 zina matarajio ya kuwa na vyoo bora na kaya 38 hazina vyoo kabisa’’ alisema Mgode.
 
 
Alisema walitembelea pia shule ya Msingi Itega yenye wanafunzi 334, na  hali halisi ya miundombinu ya shule hiyo siyo mizuri na uwiano wa matundu ya vyoo kwa wasichana ni 1 ya 60 na wavulana ni 1 ya 153.
 
 
‘’Vyoo hivyo havina sakafu inayosafishika wala havina falagha, pia vina harufu na havina maji ya kunawa kutokana na tatizo la maji katika eneo hilo na vyoo vya walimu pia havina falagha wala maji ya kunawa mikono’’ alisema.
 
 
Alibainisha changamoto inayokikumba kijiji hicho kuwa ni tatizo la maji ambayo yanapatikana katika mto songwe umbali wa kilometa 10 kutoka kijijini hapo, hivyo suala la kutumia maji katika hatua nne muhimu za kunawa mikono ambazo ni wakati wa kutoka chooni, kabla na baada ya kula na baada ya kumuhudumia mgonjwa na wakakati wa kumuhudumia mtoto inakuwa vigumu.
 
 
Alitoa ushauri kuwa watu au jamii ihamasishwe juu ya uvunaji wa maji ya mvua katika kaya na taasisi na jamii iendelee kuhamasishwa kujenga vyoo vyenye faragha au usiri vilivyoezekwa na kuwekewa milango.
 
 
Naye Afisa elimu ufundi wilaya ya Mbeya, Florence Mbwele, aliwasilisha taarifa ya ziara ya kata ya Ihahi, akisema kuwa katika ziara yao walijionea hali mbaya ya vyoo hasa kwa jamii za wafugaji.
 
 
‘’Changamoto zilizochangia uchelewaji wa utekelezaji wa mpango wa WASH, ni pamoja na uhaba wa maji, vyoo havina viwango, jamii ya wafugaji haijawafikiwa na elimu ya matumizi ya vyoo na watendaji wana uhaba wa vitendea kazi’’ alisema Florence.
 
 
Alisema hali halisi ni kwamba kuna mwitikio wa wastani kuhusu masuala ya afya na usafi wa mazingira ikiwemo maofisini tofauti na hali mbaya iliyopo kwa jamii za wafugaji.
 
 
‘’Kuhusu elimu ya matumizi ya kibuyu chilizi(maji ya kunawa yanayotiririka) jamii imeipokea lakini imeeleweka tofauti, ambapo wanatoboa garoni kwa chini hivyo wakiweka maji yote yanaisha kabla ya kutumia’’ alisema mwasilishaji huyo.
 
 
Alisema kunahitajika nguvu ya ziada katika jamii za wafugaji kwasababu katika ziara hiyo walikosa hata mtu wa kutoa ushirikiano kupata taarifa na walipofika kwenye nyumba moja, mwenyeji alipoona gari aliingia ndani na kujifungia.
 
 
Wakichangia katika warsha hiyo, Afisa afya msaidizi wa kata ya Ihahi, Khatibu Kilumbu, alisema kuwa katika kata yake wamejiwekea mikakati ya kuendelea kutoa elimu kwa wananchi, kufanya mashindano ya usafi na kwamba ni wakati muhafaka kwa viongozi wote kuwa na mipango na tathimini shirikishi kuhusu suala la usafi wa mazingira.
 
 
Afisa afya mkoa wa Mbeya, Salehe Mwango, alisema kuwa katika kijiji cha Mjele kuna udhaifu wa mashimo ya takataka, ambapo mashimo yapo lakini hayatumiki hivyo aliwataka viongozi wa eneo hilo kufanyia kazi jambo hilo.
 
 
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mjele, Evarist, alisema jamii ina elimu ya masuaa ya usafi lakini haitaki kuitikia na katika suala la ujenzi wa vyoo vyenye kuta za nyasi katika eneo lake alisema ni kutokana na kijiji hicho kutokuwa na maji hivyo wanashindwa kufyatua tofali.
 
 
Kuhusu tatizo la upatikanaji wa takwimu sahihi kutoka kwenye kata na vijiji, Afisa Afya wilaya ya Mbeya, Emmanuel Mwaigugu, alisema kuwa ni kutokana na uhaba wa watumishi wa sekta ya afya akitolea mfano katika wilaya yake kuwa katika kata za Ilungu, Ilembo na Iwiji hakuna watendaji wa idara yake.

Ijumaa, 27 Desemba 2013

VIJANA WAZALENDO MBALIZI, WAENDELEA KUJITOLEA KUFANYA USAFI KATIKA MJI WA MBALIZI MBEYA

 Vijana wazalendo Mbalizi chini ya umoja wao wa (UVIWAMBA), wakiwa wanafanya kazi za usafi katika mji wa Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya. Vijana hao wanajitolea kufanya kazi za usafi ili kuondoa dhana ya vijana kutaka kulipwa kwa kila jambo au kufanyiwa na serikali.
 Hapa ni Ghuba la eneo la Mashine ya Bariki, lililopo katika barabara ya vumbi kutoka kituo cha polisi Mbalizi kwenda Tarafani kwenye stendi ya wilaya ya Mbeya. Vijana hao waliamua kutoa takataka zilizokuwa zimelizidi dampo hilo na kuziba nusu barabara, hivyo waliingiza ndani ya ghuba takataka hizo baada ya magari ya Halmashauri hiyo kuonekana kuwa hayakuwa mazima nyakati hizi za sikikuu ya X-mass 2013.
 Vijana wakiwajibika na kutimiza wajibu wao kwa taifa, kila aliyeguswa na uzalendo huo alihusika katika kufanya kazi hiyo ya usafi ambapo kila siku ya Jumamosi ya kila Juma, vijana hao wanafanya kazi hiyo ya usafi katika eneo hilo la Mbalizi na wilayani humo.
 Vijana wa kike na kiume, wote wanawajibika, wakiwemo watu wazima...
Ghuba hilo baada ya kusafishwa hivi ndivyo linavyoonekana ingawa kuna baadhi ya wananchi siyo wastaarabu, wanaendelea kutupa taka nje ya ghuba.
 
Chanzo; kalulunga media blog

Alhamisi, 26 Desemba 2013

SIASA SIYO UGOMVI, AMANI YA JAMII YETU KWANZA

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(CCM), akimpatia zawadi mke wa Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi(Chadema).
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa na Mbunge wa Jmbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi(SUGU).
Dr. Mary Mwanjelwa siku ya ubatizo wa Mtoto Shasa Joseph Mbilinyi (Sugu) Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema) katikati, mtoto akiwa amebebwa na mama yake Mbeya Mjini.

 Tufurahi pamoja...

 Sote ni ndugu....

Jumatatu, 23 Desemba 2013

HAPPY & MERRY CHRISTMAS

Happy & Merry Christmas
Happy & Merry Christmas

ANZISHENI VIKUNDI

Dk.Mary mwanjelwa akizungumza na akina Mama wauza ndizi wa kijiji cha Iponjola kata ya Rufingo wilaya ya Rungwe na kuwataka waanzishe vikundi kwani benki ya wanawake ipo karibuni kufunguliwa katika mkoa wa Mbeya hivyo itawasaidia kupata mikopo kwa riba nafuu.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alisimama kuwasalimu wakina mama hao kisha kuutambulisha uongozi wote aliokuwa nao kwenye msafara.

 Mbunge wa Viti Maalum Wananwake mkoa wa Mbeya Dk.maru Mwanjelwa akicheza ngoma  kabala ya kuanza kwa mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Ikuti ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi wa kitaifa aliofutana nao Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro na Katiibu wa NEC Itikadi na Uenezi walihutubia.

Jumanne, 10 Desemba 2013

FURSA ZA UTALII MKOANI MBEYA, KARIBU KWETU


Mlima Loleza uliojitokeza karibu na Mbeya Peak, ndio huonekana
kutokea Mbali pale unapoingia Mbeya Mjini.
 
MKOA wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini inayozalisha mazao ya chakula kwa wingi nchini.

Mbeya ambayo kwa sasa kiutawala ipo chini ya Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro, ina wilaya tisa na majimbo ya uchaguzi 12.

Wilaya hizo ni Mbeya, Chunya, Mbeya Vijijini, Mbarali, Momba, Mbozi, Ileje, Rungwe na Kyela.

Majimbo ya uchaguzi ni Rupa, Songwe, Momba, Mbozi Magharibi, Mbozi Mashariki, Ileje, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbarali, Rungwe Magharibi, Rungwe Mashariki na Jimbo la Kyela.


Picha ya Ziwa Nyasa ambapo ndipo inapopatikana Beach Mno 
iitwayo Matema Beach kama ionekanavyo pichani.
 
Mbali na uzalishaji wa mazao ya chakula, mkoa una kivutio cha utalii kinachojulikana kuwa labda pekee ndicho kilichopo mkoani hapa ambacho ni Kimondo kilichopo Wilaya ya Mbozi.

Mbali na kivutio hicho ambacho walau kimetangazwa na serikali kwa asilimia fulani, vivutio vingine vilivyojaribu kutangazwa ni Mbuga ya wanyama Lukwati iliyopo wilayani Chunya na Hifadhi ya Taifa ya Kitulo huku vivutio lukuki vya utalii wa ndani vikiwa vimeachwa kama vile havina umuhimu.

Kati ya vivutio vya ndani vilivyopo Mbeya ambavyo havijatangazwa ni alama ya unyayo wa mguu wa mtu wa kale iliyopo Nkangamo wilayani Momba, michoro ya kale iliyopo eneo hilohilo inayosadikika kuchorwa miaka 3,000 iliyopita.

Pia kuna makundi makubwa ya mamba yaliyopo katika Ziwa Rukwa upande wa Mbeya wilayani Mbozi na maji ya moto yaliyopo katika chemichemi ya Songwe, maporomoko ya maji ya Nsala na Mfuto wilayani Mbozi.

 Kimondo kilichoangukia Mbozi miaka mingi iliyopita.

Si hivyo tu, bali kuna vivutio vingine vya utalii wa ndani ambavyo havijatangazwa kama mashamba makubwa ya kahawa yaliyopo Mbeya ambapo inasadikika kuwa ni sehemu ya kwanza katika uwekezaji uliofanywa na Wazungu hapa nchini kufungua mashamba hayo yaliyopo wilayani Mbozi.

Hivyo ni vivutio muhimu katika kizazi hiki ambacho kinahitaji kipate historia yake maana utamaduni na mambo kama haya ya historia ndiyo urithi na kielelezo cha nchi yoyote duniani.

Urithi mwingine wa historia hapa nchini ambao ni kivutio tosha ni daraja linalojulikana kwa jina la Daraja la Mungu lililopo Kiwira wilayani Rungwe ambapo wenyeji wa eneo hilo wanasema kuwa daraja hilo halijawahi kutengenezwa na mtu yeyote bali vizazi na vizazi vililikuta daraja hilo na ndiyo kisa cha kuliita daraja la Mungu.

Picha 2 tofauti zikilionyesha Daraja la Mungu, ambalo
halijatengenezwa na binadamu liliumbwa hivyo vivyo.
 
Kuna Ziwa Ngozi lililopo Namba One ambalo liko urefu wa mita 150 kutoka kilele cha milima inayozunguka ziwa, ambapo kina cha maji lina urefu wa mita 73 na ukubwa wa kilometa za mraba ni 3.75.

Ziwa hilo limezungukwa na misitu mizuri ya asili ya kitropiki hali nzuri ya hewa na tulivu.

Ili kulifikia ziwa hilo ni lazima kutembea kwa mwendo wa kati ya dakika 45 na saa moja kutoka Kijiji cha Mbeya One ambacho kipo barabara kuu ya Mbeya-Kyela.

Kutoka katika kilele cha milima inayozunguka ziwa hilo unalazimika kushuka kwa zaidi ya dakika 45 kwa kutumia mizizi migumu ya miti ya asili iliyopo katika msitu mnene kwa sababu ya mteremko mkali kuelekea katika ziwa hilo.

Ziwa hilo linasadikika kugunduliwa mwaka 1925 likitokea kijiji cha Mwakaleli wilayani Kyela baada ya kudaiwa kuchomwa na jiwe la moto na wakazi wa kijiji hicho ambao ni kabila la Wanyakyusa.

Pia linasadikika kuwa na maajabu ikiwa ni pamoja na kusikia sauti za vikohozi vya watu wasioonekana pamoja na miujiza ya watu wanaotwanga mahindi lakini hawaonekani.

Hata hivyo kwa sasa unapofika eneo hilo misitu inayozunguka ziwa hilo ina hali nzuri pamoja na baadhi ya wanyama wakiwemo nyani huku maji ya ziwa hilo yakiwa yanatumiwa kama mradi wa vijana ambao wamekuwa wakiuza kati ya sh 300 na 500 kwa lita.

Wakazi wa kijiji hicho, wanaamini kuwa maji ya ziwa hilo ni dawa kwa ajili ya kutibu watoto ambao wamekuwa wakishtuka nyakati za usiku na kwamba pindi wanaponywesha maji hayo hali hiyo hukoma mara moja.

Ziwa Ngozi ni moja ya maziwa 10 yaliyopo wilayani Rungwe ambapo maziwa mengine yanayofaa kwa utalii wa ndani ni Ndwati, Kisiba, Chungululu, Ikapu, Itamba, Asoko, Ilamba, Kingili, Katubwi na Itende.

Ziwa Kisiba lililopo eneo la Masoko ambalo hakuna mto unaoingia humo lakini maji yake hayapungui kwa msimu wa kila mwaka linasadikika kuwa kuna masanduku ya fedha chini yake lakini hakuna anayefanikiwa kuyachukua kutokana na mazindiko ya kiasili.

Pia kuna kivutio kingine kijulikanacho kwa jina la Kijungu kinachosemekana kiliua watu zamani hasa kabila la Kindali linalosadikiwa ni la watu wabishi.

Hivyo watu wa kabila hilo walikuwa wakiruka na kupotelea ndani ya kijungu hicho ambapo wenzao walikuwa wakiwadhihaki na kusema (utanyelite bhukomu) maana yake haujui kuruka vema ndiyo maana walikuwa wakitumbukia na kupotea.

Kijungu hicho kinasadikika kuwa mahala kilipo kulikuwa ni sehemu ya matambiko ya kimila hivyo ukipita eneo hilo na kuruka kilikuwa kinatanuka kisha mrukaji kutumbukia na kupotea.

Kijungu hicho kipo chini ya mto wa Kiwira karibu na Daraja la Mungu na maporomoko ya maji wilayani Rungwe.

Kwa upande wa Ziwa Nyasa lenye samaki zaidi ya aina 1000 wakiwamo samaki wa mapambo ambao ni sehemu nzuri ya utalii wa ndani na uchumi wa taifa letu kwa ujumla ukiwemo ufukwe wa Matema Beach.

Mbali na vivutio nilivyoviainisha hapo juu, pia kuna kivutio cha utalii wa ndani ambacho ni mbunga ya kutengenezwa (kufugwa) na makumbusho yaliyopo eneo la Ifisi-Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe.

Nikirudi kuhusu Kimondo ambacho ni kama jiwe gumu, kinaelezwa kuwa kilidondoka kutoka mawinguni hadi ardhini.

Kimondo hicho kipo eneo la Kijiji cha Ndolezi wilayani Mbozi, mkoani Mbeya na ni kimondo chenya utofauti mkubwa na vimondo vilivyowahi kuanguka duniani.

Eneo hilo ambalo kimondo hicho kinapatikana takribani kilomita 70 kutoka jijini Mbeya na ili kukifikia unapita barabara ya lami ambayo ni barabara kuu ya Tanzania-Zambia, ambapo ukifika eneo la Mahenje kuelekea njia ya Masangula na Masoko unaelekea Kijiji cha Ndolezi mahala ambapo kipo kimondo hicho.

Kupitia makala hii natoa wito kwa wanaharakati, waandishi wa habari na serikali kwa ujumla kujitokeza kuhamasisha utalii wa ndani na kuvitangaza vivutio kama hivi ninavyoamini vipo kila kona ya nchi yetu na huo ndio urithi wa vizazi vyetu.

Kama tutafanya hivyo kwa pamoja, kuvitangaza na kuvielezea vivutio vyetu ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha wananchi wanaoishi karibu na vivutio hivi kuvitunza hakuna ambaye atapinga kuhifadhi na kuvitunza vivutio hivi.

Naishauri serikali kuchukua hatua za makusudi kutangaza vivutio vilivyopo Mbeya na mikoa mingine badala ya kuishia kuangalia zaidi vivutio vilivyopo mikoa michache hapa nchini, hasa mikoa ya Kanda ya Kaskazini.
 Zawadi kwa mgeni; Kushoto ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akimpatia zawadi ya mkeka, Nape Nnauye alipokuwa mkoani Mbeya.
Usafiri wa Boda boda...

Alhamisi, 5 Desemba 2013

KUIMARISHA CHAMA CHA MAPINDUZI(CCM) WILAYA YA MBEYA MJINI.

 Kushoto ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa akiwa katika jukwaa viwanja vya Ruanda Nzovwe(CCM ILOMBA MBEYA), pembeni yake ni MNEC wa wilaya ya Mbeya, Capt. Sambwee Shitambala.
 Kushoto ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, Nape Nnauye na Capt. Sambwee Shitambala.
 Matembezi ya hisani kuelekea viwanja vya CCM ILOMBA MBEYA, wakati wa ziara ya katibu mkuu wa CCM Taifa, ndugu Kinana.

NELSON MANDELA DIES 95

Former South African President Nelson Mandela (left) died peacefully at his Johannesburg home on Thursday after a prolonged lung infection. He was 95.

Mandela, the country's first black president and anti-apartheid icon, emerged from 27 years in apartheid prisons to help guide South Africa out of bloodshed and turmoil to democracy. 

"Fellow South Africans, our beloved Nelson Rohlihlahla Mandela, the founding president of our democratic nation, has departed," President Jacob Zuma said in a nationally televised address.

"Our people have lost a father. Although we knew this day was going to come, nothing can diminish our sense of a profound and enduring loss. His tireless struggle for freedom earned him the respect of the world. His humility, passion and humanity, earned him their love," he added. 

Mandela would receive a full state funeral, 

Zuma said, ordering flags to be flown at half mast.

Al Jazeera's Tania Page, reporting from outside Mandela's home in Johannesburg, said that there was a real sense of celebration in tribute to Mandela there, while world leaders were also delivering their tributes.

People are "singing songs decicated to Mandela", said our correspondent.

Mandela rose from rural obscurity to challenge the might of white minority apartheid government - a struggle that gave the 20th century one of its most respected and loved figures.

He was among the first to advocate armed resistance to apartheid in 1960, but was quick to preach reconciliation and forgiveness when the country's white minority began easing its grip on power 30 years later.



Mandela was elected president in landmark all-race elections in 1994 and retired in 1999.


He was awarded the Nobel Peace Prize in 1993, an honour he shared with FW de Klerk, the white Afrikaner leader who released from jail arguably the world's most famous political prisoner.

As president, Mandela faced the monumental task of forging a new nation from the deep racial injustices left over from the apartheid era, making reconciliation the theme of his time in office.

The hallmark of Mandela's mission was the Truth and Reconciliation Commission which probed apartheid crimes on both sides of the struggle and tried to heal the country's wounds. It also provided a model for other countries torn by civil strife.

In 1999, Mandela handed over power to younger leaders better equipped to manage a modern economy - a rare voluntary departure from power cited as an example to African leaders.

In retirement, he shifted his energies to battling South Africa's AIDS crisis and the struggle became personal when he lost his only surviving son to the disease in 2005.

Mandela's last major appearance on the global stage came in 2010 when he attended the championship match of the soccer World Cup, where he received a thunderous ovation from the 90,000 at the stadium in Soweto, the neighbourhood in which he cut his teeth as a resistance leader.

Charged with capital offences in the infamous 1963 Rivonia Trial, his statement from the dock was his political testimony.

"During my lifetime I have dedicated myself to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination."

ZIARA YA KINANA, NAPE NA DR. ROSE MIGIRO JIJINI MBEYA

Kutoka kushoto ni Mbunge wa kuteuliwa Dr, Asha Rose Migiro, Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa na Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, wakiwa kwa mjumbe shina la namba 117, eneo la Iyunga Jijini Mbeya jana, Desemba 4,2013.

Jumatano, 4 Desemba 2013

KUTAWAZWA KUWA CHIFU

Dr. Mary Mwanjelwa akiwa anashukuru kwa machifu wa mkoa wa Mbeya baada ya kutawazwa kuwa mmoja wa Machifu wa mkoa huo.

Jumatatu, 2 Desemba 2013

MAKAMBA AZUNGUMZIA SUALA LA KUGOMBEA URAIS 2015

blog post image
 
*Asema anakerwa na matumizi ya fedha kutafuta uongozi
*************************************************************************
NAIBU waziri wa Wizara ya Mawasiliano sayansi na teknolojia, January Makamba,  ambaye pia ni Munge wa Jimbo la Bumbuli, ametumia dakika 17 kueleza kwanini anaweza kuwania nafasi ya Urais mwaka 2015 kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Alitumia muda huo baada ya mmoja wa waadhiri wa vyuo na vyuo vikuu mkoani Mbeya kutaka kujua uhalisia wa uvumi kuwa yeye ni miongozi mwa vijana wa CCM ambao wanatajwa kuwa watawania nafasi hiyo.

Makamba alisema kuwa, makundi ya watu wa rika mbalimbali wameendelea kumshawishi kuwania nafasi hiyo mwaka 2015 na kumtaka atafakari na kuchukua hatua.

Alisema kuwania nafasi hiyo ni jambo kubwa sana hasa wakati huu ambao yeye anakerwa na matumizi ya fedha yenye lengo la kupata uongozi.

‘’Nakerwa sana na matumizi ya fedha kutafuta uongozi jambo ambalo linawanyima fursa watu wenye vipawa vya uongozi kutuongoza, mimi sina hela, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda watu wanazidi kunifuata’’alisema Makamba.

Alisema kabla hajachukua hatua ya kutamka kuwa atagombea, anaendelea kutafakari kama kazi yenyewe ataiweza au la kwasababu kazi ya kuwa Rais si kazi yeye na familia yake bali ni ya kuwatumikia watanzania.

‘’Natafakari kuwa je! Ninaweza kuungwa mkono na watu wote Tanzania? Isije ikawa ni kikundi cha ndugu au marafiki pekee ndiyo wanakuunga mkono, Urais siyo wa Bumbuli tu’’ alisema Makamba.

Aliongeza kuwa tafakuri yake ni kwamba akijiridhisha kuwa atapata wapi fedha za kuendeshea nchi katika utawala bora, elimu na mambo mengine, atatamka rasmi kuwa anagombea nafasi hiyo kubwa na ya heshima.

‘’Ni rahisi kusema kuwa unataka kugombea, lakini ni lazima ujiulize maswali kadhaa yakiwemo kuwa je unaweza kuwaridhisha watanzania kimwili, kiakiri, kifikra na kuwa na fikra za kubadili nchi kuwa kwanini tumeshindwa mahala fulani na tunawezaje kuziba mapengo hayo. Hivyo mimi bado natafakari’’ alisema Naibu Waziri huyo.

Katika kongamano hilo lililolenga kuwakaribisha wanafunzi ambao ni wanaCCM wa mwaka wa kwanza katika vyuo hivyo, Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa alitoa mada ya asilimia hamsini kwa hamsini ya uogozi kwa wanawake.

Alisema ili kufikia kiwango hicho cha Hamsini kwa hamsini, ni lazima wanawake waache kuchukiana na jamii iwape nafasi wanawake katika nafasi za kiungozi.

‘’Wanawake ndiyo wapiga kura wakubwa na Tanzania takwimu zinaonesha kuwa wanawake ni asilimia 52, lakini wanawake tuna tatizo la kutoungana mkono na kuchukiana’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Dr. Norman Sigalla, alitoa mada ya ukosefu wa ajira kwa wasomi ambapo alisema kuwa wasomi wengi hawafanikiwi kwasababu wanachagua kazi za kufanya.

‘’Hakuna serikali yeyote duniani ambayo inaajiri wasomi wake wote, na ukiangalia wafanyabiashara wakubwa zaidi ya asilimia 86 hawana elimu ya kidato cha sita ama shahada’’ alisema Dr. Sigalla.

DR. MARY MWANJELWA AWATAKA WAJASILIAMALI KUUNDA VIKUNDI. AAHIDI KUWAWEZESHA


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akiwa amepanda pikipipiki.
VIJANA wajasiliamali mkoani Mbeya, wametakiwa kuunda vikundi vinavyoanzia watu watano kisha kupelekwa taarifa ofisi ya Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya Dr, Mary Mwanjelwa ambaye atawapatia fedha za kusajili vikundi hivyo.

Ahadi hiyo imetangazwa na Mbunge huyo alipokuwa akiwahutubia vijana wa Boda boda njia panda Itende kata ya Kalobe na vijana wa eneo la Sido Jijini Mbeya.

Dr. Mwanjelwa, alisema kuwa atagharamia fedha za usajili kwa vikundi vyote vya ujasiliamali hasa kwa vijana na wanawake ambao wataunda vikundi hivyo.

‘’ Kwa sasa benki ya wanawake inakuja Mbeya na tayari kibali kutoka benki kuu kimepatikana, watakaounda vikundi ndiyo watakaoanza kupata mikopo ya riba nafuu’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Alisema kuwa licha ya kuitwa benki ya wanawake, lakini itatoa mikopo kwa watu wote bila kujali jinsi ya mtu.

Akisoma risala ya vijana waendesha bodaboda wa Njia panda Itende, Mwenyekiti wa vijana hao, Lwitiko Kibona, alisema kuwa vijana wa shina hilo wapo 33 na tayari wana kiasi cha Shilingi 99,000/=.

‘’Tunachangishana 1,000/= kwa kila mmoja kila mwezi na lengo likiwa kila mmoja awe anamiliki pikipiki yak wake tofauti na sasa ambapo wanaendesha pikipiki za matajiri na kupeleka malengo’’ alisema Kibona.

Naye Docas Nzunda na Tito Ndunguru, kutoka katika kikundi cha vijana kata ya Kalobe, walisema kuwa wameanzisha kikundi kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Dr. Mwanjelwa, aliviwezesha kiasi cha Shilingi 40,000/= kila kikundi kwa ajili ya usajili na kuahidi kuwapatia vijana wa Bodaboda pikipiki moja kama mtaji wa kitega uchumi chao.

Wakati huo huo, aliweka jiwe la msingi katika kiwanda cha kukoboa Mpunga cha kikundi cha Mbeya Aman Group cha Sido Mwanjelwa Jijini hapa na kuwachangia kiasi cha Shilingi 500,000/= kwa ajili ya kuongezea katika ununuzi wa mitambo ya kiwanda hicho kidogo.

Pia Mbunge huyo, alitoa kiasi cha Shilingi 100,000 kwa Muungano wa jamii Tanzania(MUJATA) baada ya kualikwa na kupewa Baraka na machifu wa mkoa wa Mbeya.

Mkuu wa mila wa kanda ya Nyanda za juu kusini, Rocket Mwashinga, alisema kuwa, wanasiasa wanaoanzisha vurugu watafanya kazi mchana lakini usiku watalala ndipo wao kama wazee watafanya kazi zao.

Katibu wa wajasiliamali wa kikundi cha Aman Group, Mustapha Ntupwa, alisema mbali na kikundi hicho kuwa ni cha uchumi, pia lengo lake ni kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya na kutunza mazingira.

MADA YA MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA MBEYA DR.MARY MWANJELWA KWA WASOMI WA VYUO VIKUU MBEYA LEO TEREHE 1/12/2013. UKUMBI WA MTENDA SUNSET SOWETO MBEYA.


 1.    UTANGULIZI
ASILIMIA ya Wanaume katika uongozi ni kubwa kuliko ya Wanawake. Hii ni katika Nyanja zote. Na sio kwa Tanzania tu, tatizo hili ni a kidunia.
Kutokana na data za Bunge la Kidunia, Wanawake wameendelea kuwa ni ‘’minolity’’ katika Mabunge, wakiwa ni asilimia 12.7 dunia nzima(1999). Hii ni pamoja na kwamba Wanawake ndio wapiga kura walio wengi.
Asilimia kubwa Bungeni kwenye nchi za Nordic ilikuwa asilimia 38.9, na asilimia ndogo ilikuwa 3.4 katika nchi za Uarabuni. Nchi za Nordic walifanikiw kutokana na kuwathamini wanawake kiusawa katika elimu na umuhimu wao wa kupiga kura.
   2.    WANAWAKE.
Uwezo wa kuongoza hauangalii jinsia. Mtu yeyote anaweza kuongoza. karama na uwezo wa mtu.
Tanzania Wanawake hawajashirikishwa kwa asilimia ya kutosha. Mfano; Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wamekuwa ni wanaume tangu enzi na enzi hizo, na dalili ya kubadilisha hili ni finyu.
Itabidi tuliangalie kwenye katiba mpya kama Wanawake kwa maana ya kwamba tunaendelea na mchakato wa katiba mpya.
Wanawake wanaonekana kuwa sehemu yao ni kazi za nyumbani tu, kuzaa watoto, kulea familia na wanaume, hivyo hawana sauti.
  3. MWANAMKE KATIKA MAAMUZI KIDUNIA
Kidunia, maamuzi mengi yamekuwa yakifanyika kuhakikisha wanawake wanapata haki sawa na wanaume katika maamuzi ya uongozi na utawala (Platform for Action 1995 (SADC) ambayo inataka serikali iji-commit katika suala zima la usawa wa kijinsia katika ngazi zote-sheria, uwakilishi wa wananchi, Executive, taasisi binafsi, Asasi mbalimbali n.k Viongezeke.
Tanzania, kabla ya uhuru mwaka 1961 ilikuwa inatawaliwa kichifu ingawa tulitofautiana kijamii. Machifu hawa walikuwa ni wanaume.
Tanzania Wanawake ni asilimia 52 zaidi ya wanaume. Hii ina maana kwamba mchango wao katika jamii, uchumi pia ni mkubwa kulinganisha na wanaume.
Ingawa serikali na vyama vya siasa wanazungumzia umuhimu wa kuwashirikisha wanawake katika maamuzi, bado asilimia ni ndogo; haijafanya juhudi za utekelezaji wa kutosha.
Tanzania, statistics za vyama vingi(Multi parties) ilianza mwaka 1995. Kwa sasa Tanzania Mawaziri wanawake ni 9 kati ya mawaziri wanaume 30.
Wabunge wanawake sasa ni 100 kati ya wabunge 350 na hii ni kwasababu ya viti maalum.
Katiba ibara ya 46 (1)(a)(g)-Haki za wanawake; Kuheshimiwa, kuthaminiwa, kutambuliwa.
   4.    SABABU ZINAZOSABABISHA MWANAMKE KUTOPEWA NAFASI ZA KIMAAMUZI.
·       Mila na desturi, katika nchi nyingi Wanawake wanachukuliwa kama daraja la pili.
·       Structure ya kisiasa ilivyokaa na utawala wake(tunahitaji hii tuibadilishe na iingie kwenye katiba mpya) i.e viti maalum 50/50 majimboni.
·       Wanawake kutojiamini.
·       Social Attitude i.e Wanawake kutopendana, i.e wivu roho ya kwa nini?
5. MAONI NA MWELEKEO UJAO-TUFANYEJE?
·       Wanawake LAZIMA wawe ‘empowered’ wawe ‘sensitized’ wapewe mafunzo na wawekwe vizuri katika uongozi/ujuzi ili waweze kushiriki vema kama walivyo Wanaume.
Wanawake ambao wako kwenye uongozi waungane kuwapa moyo wengine na kuwasaidia, wasiwe wabinafsi ili nao wagombee nafasi mbalimbali katika level zote na kuwa kitu kimoja na sauti moja kama Wanawake. Wasijione wao zaidi kwa vile wamepata.
·       Wanawake wanaharakati wasaidie kupinga vikali mila potofu zozote za kumdidimiza mwanamke.
·       ‘Empowerment’ ya Mwanamke ianze ndani ya famiia, watoto wa kike na wa Kiume tangia umri mdogo wanavyolelewa. Hii itasaidia maana mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
·       Serikali pia iandae program maalum ya –empower Wanawake (capacity bulding).
·   Kuwepo na tume/chombo cha kushughulikia haki na masuala ya Wanawake tu.

·       Wanawake wasibaguliwe.
                                              AHSANTENI !!!!!!
 
ZAIDI SOMA MTANDAO WA MBUNGE HUYO www.marymwanjelwa.blogspot.com

Jumapili, 1 Desemba 2013

MAKAMBA AWAPA SOMO WASOMI WA VYUO VIKUU MBEYA KUHUSU MWELEKEO WA CCM.

 Kushoto ni January Makamba akiwa na Mbunge Mary Mwanjelwa katika ukumbi wa Mtenda Sunset Soweto Mbeya, wakati wa kongamano la wanavyuo lililolenga kuwapokea(kuwakaribisha) wanaCCM wasomi wanaoanza masomo yao katika vyuo vilivyopo mkoani Mbeya.
 Kulia ni Dr. Norman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya, akiwa ndani ya ukumbi.
 January Makamba akiwa anazungumza jambo na wasomi wa vyuo mkoani Mbeya.

ENDELEA KUTEMBELEA BLOG HII YA KIJAMII




Watembeleaji wa blog hii ya www.marymwanjelwa.blogspot.com hakuna habari yeyote inayotupwa ikishawekwa katika mtandao huu.

Ukifika mwisho wa kurasa gonga(Click) neno Machapisho ya zamani na ukitaka kurudi ukurasa wa kwanza gonga au (CLICK) neno Nyumbani.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...