Alhamisi, 30 Novemba 2017

MHE MWANJELWA AMUAGIZA MKURUGENZI KUMSIMAMISHA KAZI MSIMAMIZI WA ZAO LA PARETO KUPISHA UCHUNGUZI

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017. 
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mhe Oran Njeza akizungumza katika mkutano huo kufikisha kilio cha wananchi mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwwa kuhusu zao la Pareto na matatizo la wafanyabiashara kujaza Lumbesa kwenye uuzaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la viazi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Jojo Kata ya Santilya, Jana Novemba 29, 2017.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana Novemba 29, 2017 amemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kumsimamisha kazi Afisa Kilimo Wilaya ya Mbeya anayesimamia zao la Pareto Ndg Emmanuel Halinga ili kupisha uchunguzi.

Mhe Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania mara baada ya Mhe Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Oran Njeza na Wananchi wote waliokuwepo kwenye mkutano huo wa hadhara kumrushia shutuma nzito na kumkataa mtaalamu huyo wa kilimo mbele ya Naibu Waziri.

Alisema kuwa pamoja na zao hilo la Pareto kuwa la kwanza kwa uzalishaji katika nchi za Afrika huku likiwa zao la pili kwa uzalishaji Duniani lakini bado halijamkomboa Mkulima nchini jambo ambalo linaonyesha namna ambavyo baadhi ya wataalamu Wa Kilimo wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema kuwa wataalamu wa kilimo walipaswa kusimamia kwa kiasi kikubwa zao hilo kwani Pato lake ni wastani wa tani 2000 kwa mwaka sawa na Bilioni 12 mpaka 14 ambapo katika kipindi hili bei ya kuanzia Mkulima analipwa shilingi 2300 kwa kilo lakini inapanda mpaka shilingi 3300 kulingana na ubora wa zao hilo ambalo mkulima amelima.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli inaamini katika kazi ambazo matokeo yake yanapaswa kuonekana hivyo Mkulima kushindwa kunufaika na mazao ya Kilimo ni uzembe wa baadhi ya wataalamu Wa Kilimo unaosababishwa na kufanya kazi kwa mazoea.

Aidha, Mhe Mwanjelwa ametoa siku saba kwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto nchini Ndg Lucas Ayo kutoa sababu za kwanini mnunuzi ni mmoja wa zao hilo jambo ambalo linaonyesha kuwa na harufu ya rushwa au kupelekea kudumaza solo la zao hilo kwa kuwa na mnunuzi mmoja asiyekuwa na ushindani.

Ili kuongeza ufanisi wa zao hilo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameelekeza wakulima Kuanzisha vikundi vya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitakuwa na usajili serikalini kwani vitasaidia kuwa na mjadala wa jinsi ya kuwa na ubora wa zao la pareto jambo litakalopekea kuanzisha viwanda vidogo ambavyo ni ishara ya kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuwa na Tanzania ya Viwanda.

"Mkishaanzisha tu vikundi vya vyama vya ushirika mtoe taarifa mapema iwezekanavyo na serikali kupitia mrajisi itatoa Elimu ya ushirika" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Ameagiza zao la Pareto kuwa huru ili mkulima awe huru kuuza kwa mnunuzi anayemtaka kwani kwa sasa kuna mnunuzi mmoja tu ambaye anajipangia mwenyewe namna ya kununua zao hilo kwa gharama atakazo pasina kupingwa.

Pia alielekeza wakulima Kuingia kwenye Kilimo cha mkataba kati yao na Chama cha msingi (AMCOS) jambo litakalorahisisha kupata mikopo ya Kilimo kupitia Benki ya Kilimo nchini (TADB).

Kuhusu Lumbesa, aliwataka wafanyabiashara wa wanaojaza Lumbesa badala ya kujazwa kilo 100 kwa gunia lakini linajazwa mpaka kilo 120 kuacha haraka tabia hiyo kwani wanakwenda kinyume na sheria hivyo kwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua Kali za kisheria.

Jumapili, 26 Novemba 2017

ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA-MARY MWANJELWA


Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Machuche Mwanjelwa leo Octoba 26, 2017 amewaagiza watumishi kutofanya kazi kwa mazoea badala yake kuongeza ufanisi katika kazi kwa kuwa wabunifu, na waadilifu.
Mhe Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa kikao cha kazi alipokuwa akizungumza na Wakuu wa Idara na Vitengo wa wizara hiyo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa wizara ya Kilimo (Kilimo IV), kwa lengo la kufahamiana na kujua majukumu ya kila idara na vitengo.
Alisema kuwa ili kutimiza adhma ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dokta John Pombe Magufuli katika kuboresha huduma za wananchi ni lazima watumishi kubadili taswira ya kufanya kazi kwa mazoea na kuhamia kwenye kasi ya viwango yakinifu na weledi.
Mhe Mwanjelwa alisema kuwa Wakuu hao wa Idara na Vitengo wanajukumu kubwa la uwakilishi wa watumishi wenzao 1828 wanaohudumu katika Wizara ya kilimo kote nchini hivyo ili kuwafanya wananchi kubadili mbinu za kilimo kutoka kilimo kwa ajili ya chakula pekee hadi kufikia kilimo kwa ajili ya chakula na biashara ni lazima watumishi wote kuwa wabunifu na kutumia taaluma zao kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Katika kikao hicho kilichoongozwa na Naibu Waziri Mhe Dkt Mary Machuche Mwanjelwa Kilihudhuriwa na Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu, Sera na Mipango, Mafunzo, Zana za kilimo, Utafiti na Maendeleo, Usalama wa Chakula, Maendeleo ya mazao na Matumizi bora ya Ardhi.
Wengine ni Wakuu wa Vitengo; Kitengo cha Fedha na Uhasibu, Kitengo cha Ukaguzi wa ndani, Kitengo cha Habari na Mawasiliano serikalini, Kitengo cha sheria, Kitengo cha Ugunduzi na Ugavi na Kitengo cha TEHAMA.
“Kubwa na la msingi ambalo ningependa kuwaasa na ninyi kukumbuka kuwa hii ni awamu ya tano  ya kazi na mchakamchaka, hivyo badilisheni Mindset ili tufanye kazi kwa kumsaidia Rais kwa weledi, ubunifu, Maarifa, Juhudi na uzalendo, bado kuna watu wanatembea badala ya kukimbia’’
“Ni lazima tukimbie lakini uwe mchakamchaka with Quality kwani watu wanaamini katika matokeo chanya, kwahiyo kuanzia sasa ni lazima tukimbizane na kasi ya awamu ya tano kwa kuongeza ufanisi kwenye wizara ya kilimo na business As Usual ni Marufuku” Alikaririwa Mhe Mwanjelwa
Mhe Naibu Waziri Dkt Mwanjelwa alisema kuwa wataalamu wanapaswa kutumia utaalamu wao na kuonyesha matokeo chanya kwani kufanya hivyo kutaongeza imani kubwa kwa serikali inayotekeleza ilani ya ushindi ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi CCM.
Aliongeza kuwa Kilimo ni uti wa mgongo kwani zaidi ya asilimia 75 ya wananchi ni wakulima ambapo mtaji wake ni nguvu na ardhi hivyo wasiposaidiwa kuboresha kilimo chao na kuongeza uzalishaji ni wazi kuwa Taifa litaendelea kusalia nyuma kimaendeleo.

Jumatano, 22 Novemba 2017

Wafanyabiashara Acheni Kuwalangua Wakulima-Mh Mwanjelwa
















Mary Mwanjelwa wakati akihutubia kwenye ufunguzi wa mkutano wa kwanza kati ya mikutano saba (7) katika Kanda saba (7) za kilimo nchini inayotegemewa kufanyika ambao ni muhimu kwa makatibu tawala na washauri wa kilimo wa mikoa ya nyanda za juu kusini wa kuelimishana kuhusu ubora wa mbolea na mfumo wa bei elekezi ambao umefunguliwa rasmi.
Mhe Naibu Waziri wa Kilimo aliwasihi Makatibu Tawala hao wa Mikoa na wataalamu wa kilimo kuhakikisha kwamba wanasimamia bei elekezi ya mbolea, Wanatoa Elimu kwa Wakulima ili wanunue mbolea bora na pia kuimarisha vikundi vya wakulima ili waweze kutumia nguvu ya umoja katika kuboresha kilimo kwa ajili ya utoshelevu wa mahitaji ya kaya zao na kuuza ziada hapa nchini na nchi za nje.

Alisema kuwa wafanyabiashara licha ya kufahamu kuwa wanatakiwa kugawana faida na wauzaji wa rejareja lakini bado wanakiuka taratibu za kisheria hivyo aliwaagiza kuacha tabia hiyo ili mawakala wauze kwa rejareja na kwa bei elekezi bila kuathiri biashara zao.

Alisema Katika Sekta ya Kilimo mbolea ni moja ya pembejeo zinazohitaji ushirikiano mkubwa kutokana na ukweli kwamba inahitajika kwa wingi na ina gharama kubwa, inahitaji utaalamu katika matumizi yake na kwamba ni bidhaa inayoharibika kwa haraka endapo viwango vya utunzaji wake havizingatiwi.

Mhe Mwanjelwa aliwaagiza wakaguzi wote wa mbolea nchini kufuatilia na kuhakikisha kwamba kila mfanyabiashara wa mbolea ana leseni ya kufanya biashara ya mbolea ambayo itatolewa bure na TFRA na pia wahakikishe kwamba wote wamepata mafunzo haraka iwezekanavyo.

“Mbolea ni moja ya vichocheo vikubwa sana katika suala hili na hivyo, mwisho wa mkutano huu tunategemea kupata taarifa ya mikakati ya namna Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa zitakavyosimamia ubora na bei elekezi ya mbolea ili Mkulima aweze kuipata na kuitumia kwa lengo linalokusudiwa” Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Naibu Waziri huyo alisema kuwa Wizara ya kilimo ilitunga Kanuni ya Ununuzi wa Mbolea kwa Pamoja (Fertilizer Bulk Procurement Regulations) na kuzitangaza kwenye Gazeti la Serikali kupitia tangazo G.N. 49/2017. Pamoja na kuunda kanuni hizo, Wizara ya kilimo  ilirekebisha Kanuni ya Mbolea ya mwaka 2011 kwa Kanuni zilizotangazwa katika Gazeti la Serikali kwa tangazo G.N. Na. 50/2017 ili kuipa nguvu TFRA kukokotoa, kutangaza na kusimamia bei elekezi ya mbolea.

Aliwaagiza pia wafanyabiashara wanaotunza mbolea bila kuzingatia viwango vilivyowekwa na TFRA kuacha haraka tabia hiyo kwani kwani wanasababisha mbolea kumfikia mkulima ikiwa imepungua ubora au kuharibika kabisa na hivyo kumfanya mkulima asipate tija inayotokana na matumizi ya mbolea.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa amewataka wataalamu hao Kutenda haki katika uwajibikaji wao, Kufanya kazi kwa weledi, uaminifu, uwajibikaji uliotukuka, na nidhamu ya hali ya juu.

Aliongeza kuwa kwa yeyote atakaye kwenda kinyume na matakwa ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli itamchukulia hatua kali kwa mujibu wa sheria.

Jumatatu, 20 Novemba 2017

MHE MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21



Na Mwandishi wetu

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo amewasihi wananchi kwa kauli moja kuchagua kiongozi makini anayetokana na CCM.

Mhe Mwanjelwa alisema kuwa kumchagua diwani wa CCM ni dalili nzuri ya kumpongeza na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anazozifanya kwa muktadha wa kuwaletea maendeleo watanzania wote.

Mjumbe huyo wa NEC, aliyasema hayo Leo Novemba 20, 2017 katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Bujinga A na B kilichopo Kata ya Ibigi, Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya ambapo alimnadi mgombea Udiwani wa Kata hiyo Bi Suma Ikenda Fyandomo.

(Mnec), Mhe Mwanjelwa aliwakumbusha wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kuwa Hawachagui ilani mpya Bali wanachagua Diwani kwa ajili ya kutekeleza ilani ya Ushindi ya CCM ya Mwaka 2015-2020 ambayo wananchi waliiamini na kuichagua Octoba 25, 2015.


Alisema kuwa nchini Tanzania hakuna chama chenye uwezo wa kuwaletea maendeleo wananchi Bali Chama Cha Mapinduzi pekee ndicho chenye uwezo na jukumu la kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.


Katika Mkutano huo wanachama 21 walivutiwa na hotuba ya Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM wakati akimnadi mgombea hivyo kufanya maamuzi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na CCM ambapo wameahidi kushirikiana na mgombea udiwani wa CCM ili kuhakikisha anashinda kwa kishindo.


Ushiriki wa kampeni hizo katika Kata ya Ibigi unajili wakati ambapo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo pamoja na mambo mengine Kesho Disemba 21, 2017 atashiriki ufunguzi wa Mkutano wa Makatibu Tawala na washauri wa kilimo wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini juu ya mfumo wa ununuzi wa mbolea (BPS).


Mkutano huo utafanyika katika Ukumbi wa Benjamini Mkapa Jijini Mbeya.

Jumatano, 8 Novemba 2017

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MARY MWANJELWA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA MAZAO YA CHAKULA WAKATI NA BAADA YA KUVUNA


Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisiitiza jambo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna wakimlaki Mgeni Rasmi-Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa mara baada ya kuwasili kufungua Kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna wakifatilia Kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Mgeni Rasmi-Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Washiriki wa Kongamano la wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna wakifatilia  Kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Washiriki wa Kongamano la wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna wakifatilia  Kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Mgeni Rasmi-Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna lililofanyika katika Ukumbi wa Nkuruma, Chuo Kikuu cha Dar es salaam Leo Novemba 8, 2017.
Na Mwandishi Wetu Dar es salaam
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa leo Novemba 8, 2017 amefungua Kongamano la Wadau wa Mazao ya Chakula wakati na baada ya kuvuna lenye dhima ya kujadili masuala muhimu yanayohusiana na PHM na mchango wake katika uhakika wa chakula na kuchochea uanzishwaji wa viwanda nchini Tanzania kwa ajili ya kupunguza upotevu, kuimarisha usalama wa chakula na kuchochea uanzishwaji wa viwanda.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo linalofanyika Katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Naibu Waziri Mhe Mwanjelwa alisema kuwa anataraji kongamano hilo litakuwa na mjadala muhimu kujadili  masuala muhimu yanayohusiana na Kuzuia Upotevu wa Mazao kabla na baada ya kuvunwa (PHM).
Alisema Serikali imeweka msisitizo wa kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi na kwa Wabia wa Maendeleo kuwekeza katika eneo hilo la PHM.
“Serikali kwa kuzingatia umuhimu wa sekta binafsi itahakikisha mchakato wa kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kupunguza upotevu unakuwa shirikishi na unatekelezwa na wadau kwa ufanisi”
“Nadhani mtakubaliana na mimi kuwa hili ni tukio kubwa sana kwa Wadau wa Mpango wa kupunguza Upotevu wa Mazao baada ya Kuvunwa (PHM) nchini tangu jitihada za kushughulikia suala hili zianze na kwa sasa suala hili linaanza kueleweka kwa wadau wengi tofauti na uko nyuma ambako msisitizo ulikuwa juu ya uzalishaji na tija” Alikaririwa Mhe Mwanjelwa
Alisema, Kulingana na takwimu zilizopo bado kuna upotevu mkubwa wa mazao ya chakula ambao unafikia wastani wa asilimia 30 mpaka 40  kwa mazao ya nafaka na mikunde na kwa wastani wa asilimia 50 kwa mazao ya mboga na matunda.
Alisema ili kupunguza upotevu wa mazao ni muhimu sana na ni mkakati mzuri wa kuihakikishia nchi usalama wa chakula na lishe.Kuwepo kwa chakula cha kutosha katika Taifa na katika ngazi ya kaya ni msingi wa Taifa lenye uchumi imara, watu wenye afya nzuri na amani.
Alisema kuwa jitihada za kushughulikia UPOTEVU WA MAZAO BAADA YA KUVUNWA zilianza miaka ya 1980 baada ya kujitokeza kwa wadudu waharibifu wa mazao wajulikanao kamaDumuzi ambao walisababisha upotevu mkubwa wa mazao na kuhatarisha uhakika wa chakula nchini Tanzania.
Aliongeza kuwa Kuanzia wakati huo mabadiliko ya kisera katika sekta ya kilimo yalianza kujitokeza kupitia Serikali ya Tanzania hasa madiliko yanayolenga kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvunwa.
Sambamba na hayo pia alisema kuwa jitihada nyingi nchini Tanzania za kupunguza upotevu wa mazao zimefanyika zikiwemoKujenga maghala kupitia Miradi mbalimbali, Kuanzishwa Kitengo cha Hifadhi na Usindikaji wa Mazao, chini ya Idara ya Usalama wa Chakula na jukwaa la wadau (TPMP), Kuanzishwa kwa mashirika ya kubuni teknolojia mbali mbali zinazohusiana na PHM kama vile SIDO, CAMARTEC, Kuigizwa kwa masuala ya PHM kwenye Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP), na Kuanzishwa kwa miradi na juhudi mbalimbali zinazohusu PHM kama vile MIVARF, GPLP, COWABAMA.
Mhe Mwanjelwa alibainisha kuwa jitihada zote hizo hazikufanikiwa vizuri kwa sababu ya kukosa mfumo mzuri wa kuratibu kazi zote PHM zilizotekelezwa na wadau mbalimbali matokeo yake kukajitokeza wadau kutekeleza kazi zinazofanana bila kujuana na maeneo mengine hayakushughulikiwa kikamilifu. Hali hii ili sababisha matumizi mabaya ya rasilima na kushindwa kuwa na mipango madhubuti ya kutekeleza shughuli za maendeleo. 
Aidha, aliwataarifa kuwa maandalizi ya Mkakati wa Kuzuia Upotevu wa Taifa yako hatua za mwisho ambapo Mkakati huo utaunganisha wadau wote wanaojishughulisha na kazi za kupunguza au kuzuia upotevu wa mazao ya chakula.
“Ni Imani yangu kama mkakati huo utatekelezwa kikamilifu upotevu wa mazao utapungua kufikia wastani wa asilimia 5 nchini Tanzania” Alisisitiza Naibu Waziri Mhe Mwanjelwa.
Ksatika hatua nyingine Mhe Mwanjelwa alilipongeza jukwaa la wadau (TPMP) kwa kushirikiana vizuri na Wizara ya Kilimo, HELVETAS, Swiss Inter-cooperation-Tanzania, ANSAF na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa maandalizi ya kongamano hilo. 

Alhamisi, 2 Novemba 2017

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MARY MWANJELWA ATEMBELEA KIWANDA CHA MBOLEA MINJINGU-MANYARA

Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky) mara baada ya kuzuru katika kiwanda hicho kilichopo katika eneo na Kata ya Minjingu Mkoani Manyara.
Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Katikati) akisikiliza kwa makini taarifa kuhusu utekelezwaji wa maagizo ya waziri Mkuu mara baada ya kutembeleaa kiwanda cha Mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
 Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisikiliza kwa makini taarifa kuhusu utekelezwaji wa maagizo ya waziri Mkuu mara baada ya kutembeleaa kiwanda cha Mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
 Muonekano wa vitendea kazi vya kiwanda cha Mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd).
 Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua kiwanda cha Mbolea Minjingu akiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
  Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua kiwanda cha Mbolea Minjingu akiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
  Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua kiwanda cha Mbolea Minjingu akiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
  Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua kiwanda cha Mbolea Minjingu akiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky).
Muonekano wa baadhi ya vitendea kazi vya Kiwanda cha mbolea cha Minjingu kilichopo eneo na Kata ya Minjingu Mkoani Manyara.

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ametembelea kiwanda cha mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) kilichopo katika eneo na Kata ya Minjingu Mkoani Manyara ambapo pamoja na mambo mengine amejionea hali ya uzalishaji wa mbolea asilia ya kupandia aina ya Minjingu.

Mhe Mwanjelwa alitembelea kiwandani hapo ambapo miongoni mwa matakwa yake ilikuwa ni pamoja na kufatilia maagizo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa aliyoyatoa mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu alitembelea eneo la machimbo ya mbolea ya Minjingu na kupokea taarifa ya uendeshaji wa Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu.

Mhe Mwanjelwa alishuhudia uzalishaji ukiwa umeongezeka kufikia Tani 150,000 kwa mwaka ambapo uongozi wa kiwanda hicho umetii agizo la Waziri Mkuu la kuwasihi kuboresha teknolojia ili kuzalisha Tani zaidi ya 150,000 ambazo zitaongeza kiwango cha upatikanaji wa mbolea hapa nchini kwwani bado upo chini kuliko mahitaji

Katika hatua nyingine Uongozi wa kiwanda hicho ulitii agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye aliwagiza kuandika barua kwa Mhe Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pomnbe Magufuli kuomba radhi kwani mifuko waliyokuwa wanatumia kuuzia Mbolea hiyo ya Minjingu ilikuwa na nembo ya nchi ya Kenya licha ya kuwa inazalishwa hapa nchini.

Hata hivyo Mhe Mwanjelwa alijionea mifuko hiyo ikiwa imebadilishwa na kuwa na muonekano wa anuani ya Tanzania kama uzalishwaji wake ulivyo.

Sambamba na hayo pia Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameutaka uongozi wa kiwanda hicho cha mbolea Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) kutoa elimu kwa umma juu ya ubora na umuhimu wa mbolea hiyo ya kupandia.

Mbolea hiyo inatokana na miamba inayochimbwa katika eneo la Minjingu Mkoani Manyara ambayo husagwa na kufungashwa kwenye kiwanda kilichojengwa katika eneo hilo. Mbolea ya Minjingu imeboreshwa kwa kuongezwa virutubisho vya Nitrogen, Salfa, Magnesi, Zinki na Boron (N, S, Mg, Zn, na B). 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Mbolea cha Minjingu (Minjingu Mines and Fertilizer Ltd) Ndg Pardeep Singh Hans (Tosky) ameiomba serikali kupitia wizara ya kilimo kuwaruhusu maafisa ugani kote nchini kupatiwa mafunzo maalumu yatakayowaimarisha ili waweze kuwa sehemu ya kuitangaza mbolea bora ya Minjingu ambayo inazalishwa nchini.

Alisema kuwa serikali inapaswa kutazama upya utozaji wa VAT kwa wazalishaji wa bidhaa mbalimbali hapa nchini kwani tozo ya VAT ya asilimia 18 wanayotozwa ni kubwa huku waagizaji wa mbolea nje ya nchi wao wanaingiza pasipo tozo kama hiyo.

Aidha, alisema kuwa tayari makala za vipindi vya Redio, Televisheni na Magazeti mbalimbali zimeanza kuandaliwa kwa ajili ya kuelimisha wakulima juu ya umuhimu wa mbolea hiyo ya Minjingu ambayo ni bora kuliko mbolea nyingine yoyote nchini na nje ya nchi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli imejidhatiti katika viwanda hivyo inathamini bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...