Alhamisi, 28 Januari 2016

Mhe. Dr Mary Mwanjelwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii

Wabunge wa Bunge la Kumi na Moja wamewachagua Wenyeviti wa tatu wa Bunge ambao watasaidiana na Spika wa Bunge na Naibu Spika katika kuliongoza Bunge la Kumi na Moja katika kipindi cha Nusu ya Uhai wake.

Waliochaguliwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo Mhe. Andrew Chenge (MB), Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dr Mary Mwanjelwa (MB) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Katiba Mhe.Najma Giga (MB).


Akizungumza kabla ya uchaguzi wa Wenyeviti hao Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah alisema Kamati ya Uongozi iliwapitisha Wabunge watatu kugombea nafasi hizo tatu za Uenyekiti wa Bunge.
Dkt Kashililah alisema kwa kuwa Wagombea waliopitishwa ni watatu na kwa kuwa nafasi zilikuwa tatu hivo Bunge lilikuwa na kazi ya kuwadhibitisha.

Hivyo Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai aliwaita Wagombea wote watatu kujinadi mbele ya Bunge kabla ya kupigiwa kura ya pamoja ya Ndio au Hapana.

Ambapo Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo Mhe. Andrew Chenge (MB), Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dr Mary Mwanjelwa (MB) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Katiba Mhe.Najma Giga (MB) walichaguliwa kwa kura nyingi za Ndio kuwa Wenyeviti wa Bunge.

Alhamisi, 14 Januari 2016

Rais Dkt. Magufuli aongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam jana Januari 14, 2016. Kulia kwake ni Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na kushoto kwake ni Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa. Picha na IKULU.

Ijumaa, 8 Januari 2016

Serikali Yatoa Picha Rasmi ya Rais wa Awamu ya Tano, Dkt John Pombe Magufuli


Picha Rasmi ya Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli itaanza kuuzwa Januari 08, 2015, katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) Mtaa wa Samora.
Kila nakala ya picha hiyo itauzwa shilingi Elfu Kumi na Tano tu bila fremu.  Picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere itauzwa shilingi Elfu Tano tu.  Aidha, Picha hizo zitauzwa katika Ofisi za Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA).
 

Picha hizo zinatakiwa kutundikwa katika ofisi zote za Serikali, Taasisi za Umma, Mashirika na Ofisi binafsi.  Kila ofisi inatakiwa iwe na picha ya Mhe. Rais pamoja na Baba wa Taifa.
Serikali inatoa onyo kwa wale wote wanaosambaza  picha isiyo rasmi pamoja na Serikali kutoa taarifa kusitisha matumizi ya picha hiyo na wanaotengeneza picha ukubwa ambao siyo rasmi.

Hatua za kisheria  zitachukuliwa dhidi yao.  Idara ya Habari(MAELEZO) ndio yenye Haki miliki ya picha hiyo

Ijumaa, 1 Januari 2016

Waziri Mkuu Awapongeza Makatibu Wakuu Na Naibu Katibu Wakuu ......Awataka Wakuu wa Mikoa,Wilaya na Wakurugenzi Wajiandae Kula Kiapo


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewapongeza Makatibu Wakuu na Naibu Katibu Wakuu, mara baada ya kuapishwa Ikulu leo jijini Dar es Salaam. 

Ametoa pongezi hizo wakati Makatibu Wakuu na Naibu Katibu Wakuu wakiwa wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma mbele ya waandishi wa habari.

Waziri Mkuu Majaliwa pia amewataka viongozi hao, kuwa waaminifu, kuwajibika na  kutoa taarifa ya utendaji kwa wananchi. 

Aidha, alisema kuwa, viongozi wengine watakao apa mbele ya Kamishna wa Tume ya Maadili ni pamoja na  Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri, ikiwa ni hatua ya Serikali kudhibiti na kufuatilia matumizi ya rasilimali fedha.

“Wakuu wa Wilaya watahakikisha fedha zilizoenda katika Halmashauri zao lazima zitumike katika shughuli zilizokusudiwa” alisema Waziri Mkuu.
 
Waziri Mkuu alitoa wito kwa watanzania kuendelea kuwa na imani na Serikali ya Awamu ya Tano, kwakuwa itatimiza ahadi zote ambazo Mheshimiwa Rais na Makamu wa Rais walizitoa wakati wa Kampeni.

Makatibu Wakuu na Naibu Katibu Wakuu hao, wameapishwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli, ambapo shughuli hiyo ilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Mke wa Mheshimiwa Rais mama Janeth Magufuli pamoja na viongozi mbalimbali.

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI
S.L.P 3021
1141O DAR ES SALAAM
IJUMAA, JANUARI 1, 2016.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...