Alhamisi, 27 Agosti 2015

DKT. MAGUFULI; UKINUNUA MADARAKA IPO SIKU UTAWAUZA ULIOWANUNUA

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Mbalizi na kuendelea kusisitiza elimu itakuwa bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne,kuongeza maslahi ya walimu pamoja na jeshi la polisi.
 
Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dr. John Pombe Magufuli amewaomba wananchi wa Mbalizi Jimbo la Mbeya Vijijini mkoani Mbeya, kummpa kura za ndiyo ili aweze kuongoza watanzania na kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii ya watanzania wa hali ya chini.


Aliyasema hayo jana katika viwanja vya stendi Tarafani mjin hapo, na kwamba ametumikia nchi hii kwa miaka 20 serikalini akiwa Waziri na amekuwa mkweli na muwazi ndiyo maana ameweza kuisimamia vizuri kila wizara au jukumu alilopewa na wakubwa wake akiwatumikia Watanzania na sasa anaomba nafasi ya urais ili aweze kutekeleza vyema jukumu lake la kuwatumikia Watanzania .

Aliongeza kuwa ndiyo maana katika mchakato mzima wa kugombea urais ndani ya Chama cha Mapinduzi  alifanya kimya kimya na hakutumia fedha yoyote hivyo hakuna mtanzania yeyote anayemdai fedha ila anadaiwa utumishi uliotukuka wenye uaminifu, kujituma na kutetea maslahi ya watanzania na taifa kwa ujumla katika  taifa la Tanzania, Ameongeza kwamba ukitumia fedha kuingia madarakani na kununua madaraka ipo siku utawauza uliowanunua.
 
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Mbalizi na kuendelea kusisitiza elimu itakuwa bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne,kuongeza maslahi ya walimu pamoja na jeshi la polisi.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Mbalizi na kuendelea kusisitiza elimu itakuwa bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne,kuongeza maslahi ya walimu pamoja na jeshi la polisi.


Wananchi waliokusanyika kumsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika stendi ya mabasi mjini Mbalizi wakishangilia huku wakipiga makelele kwamba anatosha na anafaa kuwa Rais na wameahidi kumpigia kura ya ndiyo.

Alhamisi, 20 Agosti 2015

JUMA KASEJA ASAJILIWA NA KLABU YA MBEYA CITY

IMG-20150819-WA0008 (1)
Mkataba wa Juma Kaseja wa kujiunga na klabu ya Mbeya City umesainiwa August 19 mbele ya meneja wake mpya Athumani Tippo
kaseja atua mbeya city 4
Kabla ya kusaini mkataba na Mbeya City Juma Kaseja alikuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha zaidi ya miezi nane baada ya kuingia katika mgogoro wa kimkataba na iliyokuwa klabu yake ya zamani ya Yanga nakufanya kesi hiyo kutinga mahakamani.

MKUTANO WA MAJADILIANO KATI YA SERIKALI YA TANZANIA NA YA JAPAN JUU YA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA 2015/16



Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, pamoja na majukumu mengine, inajukumu pia la kuratibu miradi ya maendeleo kwa ajili ya ufadhili wa serikali ya Japan kila mwaka.  Maandalizi ya mwaka huu yameshakamilika na mkutano wa majadiliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muuungano ya Tanzania na Serikali ya Japan ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Hotel ya Hyatt Regeny, The Kilimanjaro, Dar es Salaam.

 Majadiliano hayo kwa upande wa Serikali ya Japan yaliongozwa na Bw. Masaharu Yoshinda, Balozi wa Japan nchini Tanzania, kwa upande wa Tanzania yaliongozwa na Mhandisi Happiness Mgalulla, Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.


Malengo ya mkutano huo ni kujua hatua iliyofikiwa katika maombi ya ufadhili wa miradi ya maendeleo kutoka Serikali ya Japan kwa mwaka 2014/15, kuwasilisha miradi ya maendeleo kwa ajili ya ufadhili kwa mwaka 2015/16, kujadiliana changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi na kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuboresha ushirikiano baina ya Serikali hizi mbili. Pia Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, iliwasilisha mawazo ya awali ya Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP II).


Wizara zilizoshiriki katika Mkutano huo ni pamoja na Ofisi Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, na Wizara ya Fedha.

Wizara zingine ni pamoja na Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Chakula na Ushirika, Wizara ya Mifugo na Mendeleo ya Uvuvi, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Maji na Umwagiliaji, na Tume ya Mipango – Zanzibar.


Kwa upande wa Serikali ya Japani taasisi zilizohudhuria ni pamoja na Ubalozi wa Japan nchini Tanzania, JICA – Tanzania, Makao Makuu ya JICA- Japan na Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan.

Ijumaa, 7 Agosti 2015

CBE MBEYA KUJENGA CHUO IGANZO.

 Viongozi wa Kata ya Iganzo pamoja na Uongozi wa Chuo cha CBE wakiwa katika meza kuu wakati wa hafla ya kukabidhiana mikataba ya kuuziana ardhi.
 Mkuu wa Chuo cha CBE, Profesa Emmanuel Mjema akiwashukuru wakazi wa Iganzo kwa kukubali kutoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa Chuo.
  Katibu wa jumuiya ya Igomanzo, Aman Mwazumbe akieleza namna walivyokubaliana na uongozi wa Chuo na kuwakabidhi ardhi.
Chief Ndele Wilson akitoa Baraka zake kwa uongozi wa Chuo cha CBE kuhusiana na kuendelea na ujenzi.
 Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Quip Mbeyela akitoa hotuba yake katika hafla ya kukabidhiana mikataba kati ya wananchi wa Iganzo na Chuo cha CBE.
 Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Quip Mbeyela akimkabidhi Mkataba Mkuu wa Chuo cha CBE, Profesa Mjema.
 Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya, Quip Mbeyela akimkabidhi mkataba Chifu Wilson kwa niaba ya wananchi wa Iganzo.
 Mkuu wa Chuo Profesa Mjema na Chifu Wilson wakipongezana baada ya kukabidhiana mikataba.
 Msema chochote(MC) ambaye pia ni mwalimu wa CBE Mbeya, Mwalimu Beni akiendelea kuendesha ratiba.
 Viongozi mbali mbali wakishuhudia sherehe za makabidhiano ya mikataba.
 Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia makabidhiano ya mikataba.
 Baadhi ya watumishi na walimu wa Chuo cha CBE wakifuatilia kwa makini matukio ya makabidhiano ya mikataba.
 Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma na Utafiti akitoa shukrani kwa wakazi wa Iganzo.
 Baadhi ya watumishi wa Chuo wakishirikiana na wacheza ngoma kutoa burudani na kuwapa zawadi.
 Kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani.
 Mwalimu Ben akipuliza kifaa kinachotumika katika ngoma za asili.
Picha ya pamoja kati ya mgeni rasmi, viongozi wa CBE na viongozi wa Kata ya Iganzo.

***** 
WANANCHI wa Kata ya Iganzo iliyopo jijini Mbeya na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Kampasi ya Mbeya wamekabidhiana ardhi tayari kwa ujenzi wa Chuo baada ya kukamilishana mikataba.
 
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya mikataba ya ardhi hiyo yenye ukubwa wa hekari 55 zenye thamani ya shilingi Milion 271, Mkuu wa Vyuo vya CBE, Profesa Emmanuel Mjema aliwapongeza wakazi wa Iganzo kwa ushirikiano walioutoa na kukubali kutoa ardhi.
 
Alisema kutokana na makabidhiano ya mikataba ya kisheria kukamilika mchakato wa ujenzi wa Chuo utaanza haraka iwezekanavyo ili wakazi wa Iganzo waliotoa ardhi waanze kupata manufaa mapema ili kuweza kuinua uchumi wao.
 
Alisema Chuo kitakapokamilika watumishi watapata huduma mbali mbali kutoka katika jamii inayokizunguka Chuo ambapo pia watoto watanufaika na elimu kwani wazazi hawatahangaika kuwapeleka mbali.
 
Kwa upande wao Chifu wa Iganzo, Ndele Wilson na Katibu wa Jumuiya ya Igomanzo, walisema hilo eneo awali walijitokeza wawekezaji ambao walitaka kulittumia kujenga Hotel lakini wakakataa kwa kuona hawatapata manufaa yoyote hivyo kukikubalia Chuo.
 
Naye mgeni rasmi katika makabidhiano hayo, Afisa tawala Wilaya ya Mbeya, Quip Mbeyela akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nyerembe Munasa, alisema mahusiano mazuri ya wananchi ndiyo yaliyopelekea wawekezaji kuwafuata na kuomba ardhi.
 
Mbeyela aliwasihi wakazi wa Iganzo kuanza kufikiria shughuli za kufanya ambazo kupitia Chuo wataweza kupata manufaa makubwa ikiwa ni pamoja na kujikita katika shughuli za uzalishaji ili Chuo kitakapokamilika waweze kuuza bidhaa zao.
 
Aidha alitoa wito kwa wananchi hao kuweka wazi makubaliano yaliyofikiwa kuwa ni mikataba ya kisheria ambayo itakuwa ya milele hivyo jambo hilo linapaswa kuelezwa hata kwa vizazi vijavyo ili kuepusha migogoro isiyokuwa na faida yoyote kwa baadaye.
 
Katibu huyo alisema pia uongozi wa CBE unapaswa kuzisaidia shule za Sekondari zitakazokuwa zinakizunguka Chuo kwa kujitolea kufundisha masomo ya sayansi jambo ambalo pia litawasaidia upatikanaji wa wanafunzi bora.
 
Akitoa shukrani kwa mgeni rasmi, Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma na Utafiti, Profesa Simon Msanjila, aliwashukuru wakazi wa Iganzo kwa kujitolea ardhi na kuongeza kuwa hivi sasa Chuo kimeanzisha masomo ya Digrii ya Ualimu hivyo wakati wa mafunzo ya vitendo watatumia shule za Sekondari zilizopo jirani na Chuo.
 
chanzo Mbeya yetu.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...