Jumapili, 31 Desemba 2017

DIWANI WA CHADEMA MBEYA ASIFU UTENDAJI WA RAIS MAGUFULI, MHE MWANJELWA AONGOZA MAOMBI KWA AJILI YA RAIS NA SERIKALI

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Maabara ya Kutazama kiwango cha Uotaji wa Mbegu wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro alipotembelea Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), Jana 30 Disemba 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Jana 30 Disemba 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Maabara ya Kutazama kiwango cha Uotaji wa Mbegu Mkoani Morogoro wakati wa ziara yake ya kikazi alipotembelea Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), Jana 30 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na wafanyakazi wa Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) Mkoani Morogoro wakati wa ziara yake ya kikazi, Jana 30 Disemba 2017. 

Na Mathias Canal, Morogoro

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa, Jana 30 Disemba 2017 ametangaza KIAMA kwa wafanyabiashara wa mbegu  nchini wanaouza Mbegu feki zilizopigwa marufuku na serikali.

Amewataka wafanyabiashara wote wa mbegu ambao wamekuwa wakifanya biashara hiyo kwa kuwauzia wakulima mbegu feki zilizopigwa marufuku na serikali kuacha haraka iwezekanavyo kwani serikali itawachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kukiuka maagizo ya serikali.

Ametoa agizo hilo akiwa ziarani Mkoani Morogoro ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), Taasisi iliyopewa jukumu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la usajili wa wafanyabiashara wa mbegu (Seed Dealers).

"Serikali imepokea malalamiko mengi kwa wananchi kuhusu Ubovu wa mbegu jambo ambalo limepelekea kwa kiasi kikubwa kuwa na mavuno kidogo pasina kukidhi matakwa ya wakulima wetu nchini" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Naibu Waziri huyo pia ameiagiza Taasisi ya udhibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kujitathmini kwa utendaji duni kwani wameshindwa kutimiza majukumu yao kwa kuwabaini wafanyabiashara wanaokiuka maagizo ya serikali pamoja na taratibu na sheria za nchi.

Ijumaa, 29 Desemba 2017

MHE MWANJELWA ATOA SIKU MOJA KWA WAFANYABIASHARA WALIOFUNGA MAGHALA YA MBOLEA KUYAFUNGUA LA SIVYO KUNYANG'ANYWA LESENI

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Katikati) akikagua mbegu zilizohifadhiwa ghalani kabla ya kuanza kusambazwa alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Wakala wa Mbegu Dkt Sophia Kashenge Kilenge (Kulia) na Meneja uzalishaji Wakala wa Mbegu Ndg Charles Levi (Kushoto). Picha Zote Na Mathias Canal 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Mkurugenzi Wakala wa Mbegu Dkt Sophia Kashenge Kilenge alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo baada ya kukagua baadhi ya mashine za mbegu alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Leo 29 Disemba 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua namna mbegu za mazao mbalimbali zilivyohifadhiwa alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro, Mwingine ni Kaimu Mkurugenzi Wakala wa Mbegu Dkt Sophia Kashenge Kilenge (Kushoto). Leo 29 Disemba 2017. 

Na Mathias Canal, Morogoro

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa leo Disemba 29, 2017 amewaagiza wafanyabiashara wa mbolea kote nchini walioweka mgomo wa kupeleka mbolea kwa wakulima kufikia 30 Disemba 2017 wawe wamefungua maghala yao kwa ajili ya kuwauzia mbolea wakulima.

Alisema endapo wafanyabiashara hao wasipofanya hivyo serikali itawanyang'anya leseni zao haraka iwezekanavyo ili kuruhusu wafanyabiashara wenye uwezo wa kufanya jukumu hilo pasina kuwaumiza wakulima kutokana na bei ghali ya mbolea.

Mhe Mwanjelwa ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro alipotembelea Wakala wa mbegu za kilimo (Agricultural Seeds Agency-ASA) Mara Baada ya kubaini kuwa kuna wafanyabiashara ambao wameanza kufunga maghala kwa madai ya kupanda kwa mbolea katika soko la Dunia.

Alisema kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria na kuijaribu serikali kwani malalamiko yao ya kupanda kwa bei katika soko la Dunia hayana tija kwani mbolea zote zilipo nchini tayari wakishanunua kipindi soko likiwa kwenye unafuu mkubwa.

Alisema kuwa serikali ilitoa bei elekezi katika mbolea ya kukuzia na kupandia ikifahamu fikra kuwa kupitia gharama hiyo wakulima watanufaika lakini pia wafanyabiashara watanufaika kutokana na faida wanayoipata lakini wameamua kubadili utaratibu wa kutaka kupata faida kubwa zaidi pasina kujali wakulima wataumizwa na bei hiyo kwa kiasi gani.

Mhe Mwanjelwa ameitaka kampuni ya Premium ambayo ni moja ya kampuni zilizogoma kufungua maghala na kupeleka mbolea kwa wakulima kwa bei elekezi iliyotolewa na serikali.

Alisema kuwa wafanyabiashara hao kwa makusudi wameamua kufifisha juhudi za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli ya kuwakomboa wakulima kupitia gharama nafuu ya mbolea hivyo kufikia kesho wasipofungua maghala hayo watanyang'anywa leseni zao ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa sheria.

Jumapili, 24 Desemba 2017

MHE MWANJELWA AWATAKA WAKUFUNZI WA VYUO VYA KILIMO NCHINI KUTOFANYA KAZI KWA MAZOEA

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Kitalu Nyumba (Green House) katika ziara yake ya kikazi alipotembelea Chuo cha Kilimo Mtwara Kilichopo katika kijiji ch a Naliendele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini, Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Kilimo Mtwara Ndg Elias L. Maijo, Juzi 22 Disemba 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua mashamba mbalimbali ya uzalishaji wa mazao ya kilimo katika ziara yake ya kikazi alipotembelea Chuo cha Kilimo Mtwara Kilichopo katika kijiji cha Naliendele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini, Juzi 22 Disemba 2017.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na Wakuu wa Idara na Wafanyakazi wa Chuo cha Kilimo (MATI) Mtwara Kilichopo katika kijiji cha Naliendele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini, Juzi 22 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo mara baada ya kukagua mashamba mbalimbali ya uzalishaji wa mazao ya kilimo katika ziara yake ya kikazi alipotembelea Chuo cha Kilimo Mtwara Kilichopo katika kijiji cha Naliendele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini, Juzi 22 Disemba 2017.

Na Mathias Canal, Mtwara

Wakufunzi wa Vyuo vya Kilimo kote nchini wametakiwa kutofanya kazi kwa mazoea badala yake kufanya kazi kwa Weledi, Ubunifu na Maarifa ili kuongeza tija katika majukumu yao ya kufundisha wanafunzi ambapo baadae wanazalisha wataalamu mbalimbali katika sekta ya Kilimo.

Kauli hiyo imetolewa juzi 22 Disemba 2017 na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa wakati akizungumza na Wakuu wa Idara na Wafanyakazi wa Chuo cha Kilimo (MATI) Kilichopo katika kijiji cha Naliendele katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Mjini.

Alisema kuwa watendaji hao wanapaswa kuwa wabunifu katika nyanja mbalimbali zitakazowawezesha kuwa na kipato cha ziada kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni.

Alisema kuwa kufanya hivyo kutawanufaisha kuwa na kipato kitakachowawezesha kuendesha chuo pasina kutegemea serikali kwa kina jambo ambalo litapunguza malalamiko dhidi ya serikali kufanya kila kitu.

Aidha, alisisitiza viongozi wa vyuo vyote vya Kilimo nchini kutumia vyombo mbalimbali vya Habari sambamba na mitandao ya kijamii ili kutangaza maudhui ya vyuo na kozi zinazofundishwa ili kurahisisha wanafunzi kupata wepesi katika uchaguzi wa vyuo vya kusoma.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alitembelea na kujionea miundombinu ya Taasisi na kazi za mafunzo ikiwa ni pamoja na kuangalia shughuli za uzalishaji wa mazao mbalimbali.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Kilimo Mtwara Ndg Elias L. Maijo alimpongeza Naibu Waziri huyo wa Wizara ya Kilimo kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli na hatimaye kuteuliwa kumsaidia katika majukumu yake ambapo pia ameahidi kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa.

Ijumaa, 22 Desemba 2017

DKT MWANJELWA AIAMURU TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO NALIENDELE MTWARA KUWAONGEZA MALIPO WAFANYAKAZI WAKE

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua miche ya Korosho wakati alipotembelea Kitalu Nyumba (Green House) katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara Mwingine ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Dkt Omari Mponda, leo 22 Disemba 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Tanki linalohifadhi maji kwa ajili ya Skimu ya umwagiliaji wakati alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwaraleo 22 Disemba 2017.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akishiriki kazi ya kubangua korosho wakati alipotembelea Kiwanda cha Korosho na Juice katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwaraleo 22 Disemba 2017.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua shamba lenye mfumo wa kisasa wa umwagiliaji kwa Skimu ya umwagiliaji wakati alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwaraleo 22 Disemba 2017.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua miche ya Korosho wakati alipotembelea Kitalu Nyumba (Green House) katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara Mwingine ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Dkt Omari Mponda, leo 22 Disemba 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akishiriki kazi ya kubangua korosho wakati alipotembelea Kiwanda cha Korosho na Juice katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwaraleo 22 Disemba 2017.

Na Mathias Canal, Mtwara

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) ambayo Kitaifa inaratibu Utafiti wa zao la Korosho, Mbegu za mafuta na mazao jamii ya mizizi (Muhogo na viazi vitamu) Dkt Omari Mponda ameagizwa kuwaongeza malipo ya kazi wafanyakazi wa kituo hicho katika mradi wa kubangua Korosho.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa leo 22 Disemba 2017 wakati akizungumza na wafanyakazi wa kituo hicho cha Utafiti Mara baada ya kutembelea kiwanda kidogo cha kubangua Korosho na kubaini kuwa wafanyakazi hao wanalipwa shilingi 600 kwa kila kilo moja ya korosho wanayobangua kiasi ambacho hakiakisi ufanisi wa kazi kubwa wanayoifanya.

Katika maelekezo yake Naibu Waziri huyo amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa kituo hicho kuongeza kiasi cha malipo walau kufikia shilingi 1000 kwa kila kilo moja wanayobangua ili wafanyakazi hao waweze kupata malipo ambayo yatamudu gharama za maisha.

Sambamba na hayo pia ameupongeza Uongozi wa kiwanda hicho kwa kubuni ajira hizo mpya za mradi huo wa korosho zinazowanufaisha wananchi wa Mtwara sambamba na pongezi za kuajiri wafanyakazi wengi ambao asilimia kubwa ni wanawake.

Aidha, amesisitiza kuongeza bidii ya utoaji Elimu kwa wananchi kufahamu umuhimu wa mazao ya muhogo, Njugu na Mbaazi ili yaweze kutumika zaidi kwani ni fahari kwa wakulima na wananchi kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Mhe Mwanjelwa ameipongeza Taasisi hiyo kwa kufanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza Afrika kutoa/kugundua na kusajili mbegu bora 54 za korosho kwa ajili ya matumizi kwa wakulima mwaka 2006 (Aina 16), Mwaka 2015 (Aina 22 mbegu chotara), na Mwaka 2016 (Aina 16 mbegu fupi).

Alisema Aina hizo za mbegu hizo zina uwezo wa kuzaa korosho nyingi na bora, Zina uwezo wa kuvumilia magonjwa na wadudu waharibifu na kufanya Utafiti kupendekeza zaidi ya Aina 30 za viuatilifu vya kudhibiti visumbufu vya Korosho.

Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele (NARI) imepewa jukumu la kufanya Utafiti ili kuongeza tija katika Kilimo katika kanda ya kusini mikoa ya Lindi, Mtwara na Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.

Jumamosi, 16 Desemba 2017

MHE MWANJELWA - WALIPENI WAKULIMA KWA WAKATI

 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikaanga kahawa mara baada ya kutembelea Kitengo cha kukaanga Kahawa katika Ofisi za Bodi ya Kahawa akiwa ziarani Mkoani kilimanjaro, Jana 16 Disemba 2017. Na Mpiga Mpicha Wetu
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua namna kahawa zinazohifadhiwa mara baada ya kutembelea Maabara ya kuandaa kahawa kwa ajili ya wanunuzi katika Ofisi za Bodi ya Kahawa akiwa ziarani Mkoani kilimanjaro, Jana 16 Disemba 2017
  Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisikiliza maelezo kuhusu uendeshaji wa mnada wa kahawa kwa mfumo wa kisasa Kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Ndg Primus Kimaryo alipotembelea Ofisi za Bodi ya Kahawa akiwa ziarani Mkoani kilimanjaro, Jana 16 Disemba 2017
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiwasili katika chuo cha mafunzo ya Kilimo Kilimajaro (KATC) wakati wa ziara ya kikazi Mkoani humo, Jana 16 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua miongoni mwa mashamba ya kufundishia kilimo cha mpunga mara baada ya kikao na watumishi wa chuo cha mafunzo ya Kilimo Kilimajaro (KATC) wakati wa ziara ya kikazi Mkoani humo, Jana 16 Disemba 2017

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya serikali iliyopewa jukumu la Kusimamia sekta ya Kahawa nchini Ndg Primus Kimaryo ameagizwa kusimamia na kuwalipa haraka wakulima malipo mara baada ya kukusanya mazao yao kwani kufanya hivyo kutawezesha mazingira mazuri ya biashara na kuwanufaisha wakulima kutokana na kilimo hicho.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ametoa agizo hilo jana Disemba 16, 2017 alipotembelea Ofisi za Bodi ya Kahawa akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Kilimanjaro.

Mhe Mwanjelwa alisema kuwa pamoja na wakulima kuuza kahawa kwa bei ya shilingi 5000 kwa kilo katika msimu wa mwaka 2016/2017 lakini bado changamoto ni kubwa ya ucheleweshaji wa malipo kwa wananchi jambo ambalo linarudisha nyuma ufanisi wa zao.

Alisema miongoni mwa kazi kubwa ya Bodi ya Kahawa nchini ni pamoja na kulinda maslahi ya wakulima dhidi ya makundi mbalimbali yanayofanya biashara ya zao la kahawa hivyo kucheleweshwa kulipwa malipo yao ni ishara ya Bodi hiyo kutotekeleza majukumu yake ipasavyo.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi huyo wa Bodi ya Kahawa ametakiwa kuwa na mikakati imara na yenye tija itakayolifanya zao la kahawa kuwa na ubora zaidi Duniani kwa kwa kuliongezea thamani.

Katika ziara hiyo pia Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alitembelea chuo cha mafunzo ya Kilimo Cha Kilimajanro (KATC-Kilimanjaro Agricultural Training College) ambapo ameupongeza uongozi wa Chuo hicho kwa kuwawezesha zaidi ya wakulima 7000 katika skimu zaidi ya 100 kuboresha kilimo cha mpunga na mazao mengine hivyo kupata ongezeko kubwa la mazao.

Sambamba na pongezi hizo pia amewataka kuongeza ufanisi katika utendaji ili kuunga mkono kwa vitendo serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kufanya kazi kwa bidii, ufanisi, na ubunifu.

Aliwasisitiza wananchi hao kutofanya kazi kwa mazoea badala yake kuwa wabunifu katika kazi ikiwa ni pamoja na kuzikabili changamoto na kuzigeuza kuwa fursa.

Jumatano, 6 Desemba 2017

MHE MWANJELWA AUTAKA UONGOZI WA KIWANDA CHA KUSINDIKA NA KUCHAKATA CHAI CHA ITONA KUTOA AJIRA ZA UHAKIKA SIO VIBARUA

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Jinsi uzalishaji wa Chai unavyohifadhiwa wakati alipotembelea Kiwanda cha Kusindika na Kuchaka Chai cha  Itona kilichopo Wilayani Mufindi Mkoani Iringa wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani humo, Jana Disemba 5, 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua mashamba ya Chai Kijijini Itona, Kata ya Ifwagi wakati alipotembelea Kiwanda cha Kusindika na Kuchaka Chai cha  Itona kilichopo Wilayani Mufindi Mkoani Iringa wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani humo, Jana Disemba 5, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wakulima wa zao la Chai katika Kijiji cha Itona, Kata ya Ifwagi, Wilaya ya Mufindi wakati wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Iringa . Jana Disemba 5, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Jinsi zao la Pareto linavyochakatwa kiwandani wakati alipotembelea Kiwanda cha kuchakata Pareto cha PCT cha Mjini Mafinga wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani Iringa. Jana Disemba 5, 2017.

Na Mwandishi Wetu

Wamiliki wa viwanda nchini wametakiwa kutoa ajira za uhakika/mkataba kwa wafanyakazi wao ili kuongeza ufanisi wa ajira kwani asilimia kubwa ya viwanda nchini vinaajiri wafanyakazi kama vibarua jambo ambalo linaweka mashakani ajira zao.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alipotembelea Kiwanda cha Kusindika na Kuchaka Chai cha  Itona kilichopo Wilayani Mufindi Mkoani Iringa wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani humo.

Mhe Mwanjelwa Alisema kuwa kutoa ajira zisizo na mikataba/vibarua ni sehemu ya kuwazalilisha wananchi hususani watanzania kwani wanasalia kufanya kazi kubwa huku wakiishi kwa hofu badala yake ajira hizo za mikataba zinaweza kuendelea kwa wageni na sio wazawa.

Mbele ya Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Itona, Kata ya Ifwagi Wilayani Mufindi Mhe Mwanjelwa aliwahakikishia wakulima kuboreshwa soko la zao hilo kwa kutangaza bei elekezi ya serikali hivi karibuni ili kupunguza unyonyaji unaofanywa na wamiliki wa viwanda kwa kununua malighafi hizo kwa bei ya chini ambayo kwa kiasi kikubwa haiwanufaishi wakulima.

Aliwataka wamiliki wa kiwanda cha Kusindika na Kuchaka Chai cha  Itona kuongeza nguvu katika ununuzi wa Chai kwa wakulima kwani asilimia 21 ya chai wanazonunua kwa wakulima wote wa zao hilo ni chache ukilinganisha na uzalishaji wao mkubwa.

Alisema wanapaswa kuongeza tija katika ununuzi angalau kufikia asilimia 40 ili kuwaongezea soko wakulima hao jambo litakalowanufaisha ikiwa ni pamoja na kuongeza uzalishaji ukilinganisha na uzalishaji mdogo wa sasa.

Sambamba na hayo pia aliwataka kuanzisha mashamba darasa kwa ajili ya kutoa elimu ya kilimo bora cha zao la chai kwa wakulima hao ili waweze kuwa na uzalishaji bora katika zao hilo.

Katika hatua nyingine Mhe Mwanjelwa aliwapongeza wamiliki wa kiwanda hicho cha kusindika na kuchakata chai cha Itona kwa idadi kubwa ya kuajiri wazawa ambapo zaidi ya watanzania 1500 wameajiriwa huku wageni wakiwa wanne pekee.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa amehitimisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Iringa ambapo alitembelea pia kiwanda cha kuchakata Pareto cha PCT cha Mjini Mafinga na kukagua maabara ya kupima ubora wa Pareto sambamba na kuzungumza na uongozi wa kiwanda hicho ili kuboresha na kuongeza bei ya ununuzi wa zao hilo kwa wakulima.

Jumanne, 5 Desemba 2017

MHE MWANJELWA AWATOA HOFU WAKULIMA WA NYANYA MKOANI IRINGA

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa Mkoa wa Iringa mara baada ya kusomewa taarifa ya maendeleo ya sekta ya kilimo Mkoani humo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza, Jana Disemba 4, 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Meneja uzalishaji wa kiwanda cha kutengeneza Achali ya nyanya/TOMATO SOURCE cha Chai Bora Ltd/Dabaga Ndg Sanjay Rai kilichopo Kijiji cha Ikokoto Kata ya Ilula Wilayani Kilolo Mkoa wa Iringa alipotembelea kiwanda hicho sambamba na kufanya mkutano na wawakilishi wa wakulima. Mwingine ni Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe Asia Abdalah Juma, Jana Disemba 4, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Meneja uzalishaji wa kiwanda cha kutengeneza Achali ya nyanya/TOMATO SOURCE cha Chai Bora Ltd/Dabaga Ndg Sanjay Rai kilichopo Kijiji cha Ikokoto Kata ya Ilula Wilayani Kilolo Mkoa wa Iringa alipotembelea kiwanda hicho sambamba na kufanya mkutano na wawakilishi wa wakulima. Jana Disemba 4, 2017.
Mkuu Wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza akisoma taarifa ya hali ya sekta ya chakula katika mkoa huo mbele ya mgeni rasmi Naibu Waziri Wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa . Jana Disemba 4, 2017.
Picha ya pamoja Naibu Waziri wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa (Wa tatu kulia) Mkuu Wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza (Wa pili kulia) Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Bi Wamoja Ayubu, Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe David Willium Jamhuri na wataalamu wa Kilimo Mkoa wa Iringa. Jana Disemba 4, 2017.

Na Mwandishi Wetu

Wakulima wa zao la Nyanya wametakiwa kuondoa wasiwasi wa kufikiri kupunguza kasi ya kilimo kutokana na viwanda vya nyanya kununua tani chache za nyanya tofauti na uzalishaji.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikokoto kilichopo Kata ya Ilula Wilayani Kilolo Mkoa wa Iringa mara baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza Achali ya nyanya/TOMATO SOURCE cha Chai Bora Ltd/Dabaga.

Alisema kuwa kuanzishwa kwa kiwanda hicho kipya ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kuelekea Tanzania ya viwanda hivyo kitawanufaisha wakulima hao wa nyanya ambao soko lao linasuasua.

Alisema kuwa kiwanda hicho ambacho kilianza uzalishaji Octoba mwaka huu kwa kuchakata nyanya kwa Tani 16 mpaka Tani 20 kwa masaa 8 pindi kitakapokamilika na kuanza kufanya kazi kwa masaa 24 kitaongeza uzalishaji hivyo wakulima wa nyanya watapata soko la uhakika.

Mhe Mwanjelwa aliwahakikishia wakulima hao kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wakulima nchini ili waweze kunufaika na kilimo kwani inafahamika kuwa asilimia zaidi ya 75 ya watanzania wanajihusisha na kilimo.

Aliwasihi wakulima hao Kulima nyanya kwa awamu tofauti na hivi sasa ambapo wanalima kwa msimu kwani kufanya hivyo itawasaidia kupata kipato wakati wote huku viwanda vikiwasaidia kununua mazao hayo wakati wote kwani kwa sasa viwanda hivyo vinafungwa kutokana na msimu wa nyanya kumalizika.

Aidha amewasihi wamiliki wa kiwanda cha kutengeneza Achali ya nyanya/TOMATO SOURCE cha Chai Bora Ltd/Dabaga kuwa na bei rafiki kwa wakulima kwani kufanya hivyo itakuwa ni msingi wa kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.

Sambamba na hayo pia alisisitiza Uongozi wa Vijiji na Kata kusaidiana na wataalamu wa ushirika na maendeleo ya jamii kuendelea kuhamasisha wakulima kujiunga katika vikundi vya Vyama vya ushirika ili waweze kupata mikopo ya fedha, pembejeo na kupata mafunzo ya ugani na kuanzisha viwanda vidogo vya kusindika mazao wanayozalisha.

Wakati huo huo Naibu Waziri huyo wa kilimo Mhe Mary Mwanjelwa amesifu juhudi za uongozi wa Mkoa wa Iringa unaoongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe Amina Masenza kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwa ni pamoja na kuanzisha kampeni ijulikanayo kama “Mkoa Wetu, Viwanda Vyetu” yenye lengo la kuwezesha wakulima kupata masoko ya uhakika kwa mazao wanayozalisha.

Aidha, ameelekeza kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwa wafanyabiashara wote watakaobainika kukiuka bei elekezi ya mbolea katika Mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...