Jumatatu, 2 Desemba 2013

DR. MARY MWANJELWA AWATAKA WAJASILIAMALI KUUNDA VIKUNDI. AAHIDI KUWAWEZESHA


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akiwa amepanda pikipipiki.
VIJANA wajasiliamali mkoani Mbeya, wametakiwa kuunda vikundi vinavyoanzia watu watano kisha kupelekwa taarifa ofisi ya Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya Dr, Mary Mwanjelwa ambaye atawapatia fedha za kusajili vikundi hivyo.

Ahadi hiyo imetangazwa na Mbunge huyo alipokuwa akiwahutubia vijana wa Boda boda njia panda Itende kata ya Kalobe na vijana wa eneo la Sido Jijini Mbeya.

Dr. Mwanjelwa, alisema kuwa atagharamia fedha za usajili kwa vikundi vyote vya ujasiliamali hasa kwa vijana na wanawake ambao wataunda vikundi hivyo.

‘’ Kwa sasa benki ya wanawake inakuja Mbeya na tayari kibali kutoka benki kuu kimepatikana, watakaounda vikundi ndiyo watakaoanza kupata mikopo ya riba nafuu’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Alisema kuwa licha ya kuitwa benki ya wanawake, lakini itatoa mikopo kwa watu wote bila kujali jinsi ya mtu.

Akisoma risala ya vijana waendesha bodaboda wa Njia panda Itende, Mwenyekiti wa vijana hao, Lwitiko Kibona, alisema kuwa vijana wa shina hilo wapo 33 na tayari wana kiasi cha Shilingi 99,000/=.

‘’Tunachangishana 1,000/= kwa kila mmoja kila mwezi na lengo likiwa kila mmoja awe anamiliki pikipiki yak wake tofauti na sasa ambapo wanaendesha pikipiki za matajiri na kupeleka malengo’’ alisema Kibona.

Naye Docas Nzunda na Tito Ndunguru, kutoka katika kikundi cha vijana kata ya Kalobe, walisema kuwa wameanzisha kikundi kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Dr. Mwanjelwa, aliviwezesha kiasi cha Shilingi 40,000/= kila kikundi kwa ajili ya usajili na kuahidi kuwapatia vijana wa Bodaboda pikipiki moja kama mtaji wa kitega uchumi chao.

Wakati huo huo, aliweka jiwe la msingi katika kiwanda cha kukoboa Mpunga cha kikundi cha Mbeya Aman Group cha Sido Mwanjelwa Jijini hapa na kuwachangia kiasi cha Shilingi 500,000/= kwa ajili ya kuongezea katika ununuzi wa mitambo ya kiwanda hicho kidogo.

Pia Mbunge huyo, alitoa kiasi cha Shilingi 100,000 kwa Muungano wa jamii Tanzania(MUJATA) baada ya kualikwa na kupewa Baraka na machifu wa mkoa wa Mbeya.

Mkuu wa mila wa kanda ya Nyanda za juu kusini, Rocket Mwashinga, alisema kuwa, wanasiasa wanaoanzisha vurugu watafanya kazi mchana lakini usiku watalala ndipo wao kama wazee watafanya kazi zao.

Katibu wa wajasiliamali wa kikundi cha Aman Group, Mustapha Ntupwa, alisema mbali na kikundi hicho kuwa ni cha uchumi, pia lengo lake ni kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya na kutunza mazingira.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...