Jumatano, 29 Januari 2014

DR.MARY MANJELWA ATEMBELEA KAMBI LA VIJANA WA HALAIKI CHIMALA MBEYA NA KUWAPONGEZA

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(kushoto), akiwa na katibu wa Jumuiya ya wazazi katika shule ya sekondari Chimala, ambapo limewekwa kambi la vijana wa Halaiki kwa ajili ya maazimisho ya miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), yatakayofanyika Februari 2, mwak huu mkoani Mbeya.
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akizungumza na viongozi wa umoja wa vijana (UVCCM) Mkoani Mbeya.

 Vijana wa halaiki, wakifanya mazoezi yao katika uwanja wa shule ya sekondari Chimala, wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
 Vijana wa halaiki, wakichora maumbo mbalimbali kwa kutumia miili yao.....ubunifu....
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(kushoto), akizungumza na mwalimu wa halaiki hiyo uwanjani hapo, katikati ni katibu wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, Mr. Yassin.
 Sarakasi....


 CCM HOYEEEE.....Akapusipusi, akanyaunyau....
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akizungumza na vijana wa halaiki uwanja wa Chima;la Sekondari.
 Vijana wa halaiki wakiwa wamembeba juu Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Mbeya, Amani Kajuna.
 Wakimbeba mmoja wa matron wao....




MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, amewatembelea vijana walioko kambini katika shule ya Sekondari ya Chimala wilayani Mbarali mkoani Mbeya na kuwapa moyo na kuwachangia Mchele nusu gunia, viazi viroba viwili na mahitaji muhimu kwa kutoa Tsh. 200,000.

Dr. Mwanjelwa amewaambia vijana hao kuwa mbalina halaiki hiyo, wao ni chachu kubwa kwa chama na chama kitawathamini kwa kuzingatia msemo wa mchumia juani, kivulini.

Sherehe za miaka hiyo 37 za Chama Cha Mapinduzi(CCM), zinatarajia kufanyika Jijini Mbeya na mgeni rasmi atakuwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Jumatatu, 27 Januari 2014

MAONI YA MWANAHABARI RASHID MKWINDA


Dr. Mary Mwanjelwa siku ya ubatizo wa Mtoto Shasa Joseph Mbilinyi (Sugu) Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema) katikati, mtoto akiwa amebebwa na mama yake Mbeya Mjini.
 
Rashid Mkwinda ameacha maoni mapya kuhusu chapisho lakoSIASA SIYO UGOMVI, AMANI YA JAMII YETU KWANZA:

Nimeipenda sana hii siasa sio ugomvi, nawatakia kila la kheri katika majukumu yenu ya kila siku msitumie majukwaa au vyombo vya habari kuchafuana nanyi hampaswi kubagua wanahabari katika harakati zenu.


(Tunakushukuru sana Rashid Mkwinda, maoni yako ni ya kujenga)

 TAARIFA YENYEWE ILIKUWA HIVI;

SIASA SIYO UGOMVI, AMANI YA JAMII YETU KWANZA

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(CCM), akimpatia zawadi mke wa Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi(Chadema).
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa na Mbunge wa Jmbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi(SUGU).
Dr. Mary Mwanjelwa siku ya ubatizo wa Mtoto Shasa Joseph Mbilinyi (Sugu) Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema) katikati, mtoto akiwa amebebwa na mama yake Mbeya Mjini.

 Tufurahi pamoja...

 Sote ni ndugu....

SUGU AWATUHUMU MAAFISA USALAMA KUTOA SIRI ZA SERIKALI


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa (N i kama anamuonya kitu) Mbunge wa Jmbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi(SUGU).

..........................................................................................................

MBUNGE wa Jimbo la Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi(sugu), amesema kuwa chama chake cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), kinapata taarifa za serikali kutoka kwa baadhi ya maafisa usalama wa taifa.

Hayo aliyasema Januari 25, mwaka huu, katika mkutano wa hadhara wa chama hicho, uliofanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya.

Alilazimika kutoa siri hiyo alipokuwa akizungumza kuwa amepata taarifa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), kupeleka vijana 300 kambini katika shule ya sekondari Chimala wilayani Mbarali mkoani hapa, kwa ajili ya mafunzo ya kuvuruga mikutano ya Chadema.

‘’Chama cha magamba kimepasuka na ndiyo maana tunapata siri zote, na popote palipo na maafisa usalama zaidi ya watatu mmoja wao ni wa Chadema na walipo maafisa watatu au wanne wa Polisi, wawili ni wetu’’ alisema Mbilinyi huku akishangiliwa na wafuasi wake.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dr,Wilbroad Slaa, alisema kutokana na taarifa hiyo anaagiza kukutana na vijana wake wa kikosi cha Red Briged kwa ajili ya kukabiliana na vijana hao wa CCM.

Mbali na hilo, alisema wamepata taarifa kuwa serikali inataka kutumia jopo la waganga wa kienyeji kuwashughulikia wapinzani lakini yeye hawatamuweza kwasababu yeye pia ni Mganga wa jadi na kwao Karatu wanamfahamu alipokuwa Fratee katika kanisa Katoliki.

Aidha, aliweka wazi kuwa pamoja na mambo mengine, hakupendezwa na suala la kuona jeneza ambalo lilitengenezwa na chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini na kuandika buriani Zitto Kabwe, kwasababu ishara hiyo siyo nzuri kwa mtu aliye hai.

Kutokana na tamko la viongozi hao, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), Mkoa wa Mbeya, ulilazimika kuitisha waandishi wa habari na kukanusha jambo hilo.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, Aman Kajuna, alisema kuwa chama hicho kimepeleka vijana wasiozidi 280 katika kambi lenye lengo la mafunzo ya haraiki kwa ajili ya sherehe za miaka 37 ya CCM zitakazofanyika Jijini Mbeya kitaifa.

Hata hivyo, baadhi ya waandishi wa habari mkoani Mbeya, walitembelea kambi hilo baada ya mkutano wa Chadema uliofanyika karibu na shule ya Chimala kuisha na kukuta vijana hao wakifanya mazoezi ya kuumba maumbo yanayoashiria sherehe hizo sambamba na kuimba nyimbo za chama chao.

Alhamisi, 23 Januari 2014

Mbunge wa viti maalum mkoani Mbeya Dr. Mary Mwanjelwa akiwa anafunga goli kuashiria ufunguzi wa mechi ya kirafiki ya mpira wa pete kati ya timu kutoka wilayani Mbozi na Mbeya mjini.

TUJIKUMBUSHE; MWIGULU NCHEMBA ALIPOISIMANGA CHADEMA MBEYA. ALISEMA ANAMCHUKIA SHETANI NA CHADEMA.



 AKIPOKELEWA MBEYANA VIONGOZI WA CCM MKOA
 KUTOKA KULIA NI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MBEYA GODFREY ZAMBI, MWIGULU NCHEMBA NA MBUNGE DR. MARY MWANJELWA.
 DR. MARY MWANJELWA NA MWIGULU NCHEMBA
 MWIGULU NCHEMBA AKISALIMIANA NA MNEC WA WILAYA YA MBEYA CAPT. SAMBWEE SHITAMBALA. KULIA KWA SHITAMBALA NI MJUMBE WA MKUTNO MKUU WA TAIFA CHARLES MWAKIPESILE.

Jumanne, 21 Januari 2014

BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA, PETER KALAGHE, AWAKARIBISHA WABUNGE WANAWAKE WA TANZANIA

Balois wa Tanzania nchini Uingereza Amb. Peter Kalaghe katikati mwenye suti akiwa na Wabunge Wanawake waliokwenda kutembelea ofisini kwake Jana. Wabunge hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa TWPG mhe. Mama Anna Abdallah -kushoto na Naibu Katibu Mkuu wa TWPG Dk. Mary MWANJELWA kulia mwenye koti la chuichui-wapo nchini Uingereza kwa mwaliko wa Bunge la Uingereza-CPA kwa mafunzo.

Jumapili, 19 Januari 2014

UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

______________________________ ________________


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-



  1. OFISI YA RAIS


Hakuna mabadiliko.


  1. OFISI YA MAKAMU WA RAIS


2.1 Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko


  1. Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)

Waziri wa Nchi (Mazingira).


  1. Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)

Naibu Waziri



  1. OFISI YA WAZIRI MKUU


Hakuna mabadiliko

4.0 WIZARA

4.1 WIZARA YA FEDHA

  1. Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)

Waziri wa Fedha
Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha

  1. Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)

Naibu Waziri wa Fedha



  1. WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


Hakuna mabadiliko


4.3 WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

4.3.1 Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
Waziri wa Katiba na Sheria



  1. Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko




  1. WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI


Hakuna mabadiliko


4.5 WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA

4.5.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

4.5.2 Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara


4.6 WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA

Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa



  1. WIZARA YA UJENZI


Hakuna mabadiliko

4.8 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

4.8.1 Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
Waziri wa Mambo ya Ndani


  1. Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko



4.9 WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII


  1. Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii


  1. Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii


4.10 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

4.10.1 Waziri: Hakuna mabadiliko

4.10.2 Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi


14.11 WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

14.11.1 Waziri: Hakuna mabadiliko

14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto


14.12 WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi


  1. Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi



  1. WIZARA YA KAZI NA AJIRA


Hakuna mabadiliko


  1. WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA


Hakuna mabadiliko
14.15 WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

14.15.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.15.2 Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi


14.16 WIZARA YA MAJI

14.16.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.16.2 Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji


14.17 WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA

14.17.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

14.17.2 Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika


4.18 WIZARA YA UCHUKUZI

Hakuna mabadiliko


4.19 WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

4.19.1 Waziri - Hakuna mabadiliko

4.19.2 Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo


4.20 WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii

4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

4.21 WIZARA YA NISHATI NA MADINI


  1. Waziri - Hakuna mabadiliko



  1. Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko


4.21.3 Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)

Naibu Waziri (Nishati)





Balozi Ombeni Y. Sefue
KATIBU MKUU KIONGOZI



Ikulu
DAR ES SALAAM

19 Januari, 2014

DR. MWANJELWA SIKU ALIPOWAPONGEZA NA KUTOA MSAADA KWA WAISLAM MBEYA

 Dr. Mary Mwanjelwa, akimkabidhi Imamu Mkuu wa msikiti huo, Iliyasa Mchalikwao, mifuko 60 yenye saruji ndani ya gari.
 Sasa kumekucha......sasa kumekucha...
*****************************************************************************************************8


WAISLAM wa msikiti wa Almasjid Tawfiq,  Soweto Jijini Mbeya, wamepongezwa kwa ubunifu wa maendeleo na kuwa na nia ya dhati ya kuleta amani na mshikamano nchini.


Pogezi hizo zimetolewa Juzi na Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(CCM), alipokuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchagia ujenzi wa msikiti wa kisasa unaotarajiwa kujengwa eneo hilo la Soweto. 
 
Dr. Mwanjelwa alisema, Misikiti na makanisa ni maeneo ya kiimani pia ni maeneo ya kutengeneza maadili na kuiweka jamii kuwa salama.

‘’Kiongozi mzuri ni yule mwenye maadili, asiyejali itikadi za kiimani, bali kuhudumia jamii, mimi ni kiongozi wa wote sibagui kabila, dini wala tabaka lolote, moyo wangu ni wa kusaidia jamii’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Alisema kuna baadhi ya wananchi na makundi yenye nia nzuri ya kimaendeleo, wanawachukia baadhi ya viongozi hata bila kuwashirikisha, jambo ambalo alisema jamii inapaswa kuondokana nalo na aliomba yeye ashirikishwe kwa kila jambo la kimaendeleo kwasababu yeye ni mwanamaendeleo na si ‘’longolongo’’.

Katika harambee hiyo, Mbunge huyo alitoa mifuko 60 ya saruji yenye thamani ya Shilingi Milioni moja na Laki Nne, ambayo aliikabidhi papo hapo ikiwa kwenye gari aina ya Canter  T 441 BRL, na kuahidi kuwatafutia viongozi wengine wa kuchangia ujenzi wa msikiti huo wa kisasa.

Imamu mkuu wa msikiti huo, Ilyasa Mchalikwao, alimshukuru Mbunge huyo kwa ajili ya moyo wake wa kukubali kuchangia msikiti huo bila kujali itikadi ya kidini na kwamba huo ndiyo uongozi.

Awali akisoma risala ya Msikiti,  Katibu wa Maendeleo ya Msikiti huo wa Almasjid Tawfiq, Juma Ramadhani, alisema wanatarajia kujenga msikiti wa kisasa wenye ghorofa tatu ambao utajengwa kwa awamu nne na kugharimu zaidi ya Shilingi Milioni 700.

Alisema lengo la ujenzi wa msikiti huo wa kisasa ni maendeleo na kwamba msikiti huo ukikamilika, utakuwa ni wa mfano katika mkoa wa Mbeya na Dr. Mwanjelwa tayari ameingizwa kwenye historia ya msikiti huo kwa kuwa ni kiongozi wa kwanza kuchangia.

‘’Tayari tumekusanya Shilingi Milioni 34, na tumeshauriwa kuacha kusambaza majengo ardhini, tuna imani nawe kwasababu unaweza na ni makini sana tena sana na tunakutegemea kututafutia wafadhili kwasababu unao marafiki ndani na nje ya nchi’’ alisema Juma Ramadhani.

Alisema historia na maisha ya Mwanadamu vinaenda sawa, hivyo wanamtakia kheri katika kazi zake za kisiasa na kutumikia wananchi na kwamba mbali na yeye pia Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Aesh Hilary(CCM), alituma Sh. 1.5 Milioni kwa ajili ya kumwongezea nguvu ya harambee Dr, Mwanjelwa.

ZIARA YA MBUNGE DR.MARY MWANJELWA, ZINZAVYOIBUA UJASILIAMALI MBEYA


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya Dr. Mary Mwanjelwa akiwa na baadhi ya wananchi wa Majengo Jijini Mbeya katika ziara zake.

 Akimkabidhi Tsh. 200,000 kiongozi wa kikundi cha kukuza vipaji vya vijana Jijini Mbeya.
 Dr. Mary Mwanjelwa, akimkabidhi Shaban Robert mashine ya kufyatulia tofali za kisasa kwa ajili ya timu ya Veteran ya Jiji la Mbeya. Mashine hiyo inagharama ya Tsh.540,000 na ameahidi kuwatafutia mtaalam wa mafunzo na kuwatafutia soko la tofali hizo.

DR. MARY MWANJELWA; MWANAMKE SHUPAVU WA SIASA ZA VITENDO

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya Dr Mary Mwanjelwa(CCM) akiwa na baadhi ya walemavu Jijini Mbeya baada ya kutoa msaada wa baiskeli 10 za walemavu wa miguu zenye dhamani ya Tsh. Milioni 2.5

Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa -MB, akitoa mada juu ya kumwezesha mwanamke na uongozi katika maamuzi kwenye Bunge la ACP-EU Women Forum Brussels-Belgium Jumamosi tarehe 15/6/2013

****************************************************************************

UNAPOPATA kujua historia za wanasiasa wanawake nchini Tanzania wanaofanya vizuri katika majimbo ama mikoa yao, ni dhahili huwezi kukosa jina la Dr. Mary Mwanjelwa.

Mwanamke huyo ni Mbunge wa Viti maalum kutokea mkoani Mbeya kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

Sifa yake ya kwanza ni ucheshi ambao yeye anasema kuwa ucheshi wake unatokana na wokovu alionao(kumcha Mungu).

Kabla ya kujikita katika masuala ya siasa alikuwa Mkurugenzi wa shirika la PSI Tanzania ambako historia haimuhukumu hata baada ya kutoka huko kwa kile kinachojieleza kuwa alitoka na utumishi uliotukuka.

Katika mahojiano na Mwandishi wa makala haya, Dr. Mary Mwanjelwa anasema kuwa alipata ubunge kupitia viti maalum mwaka 2010.

Anasema kwa sasa katika mkoa wa Mbeya, kuna wabunge wa viti maalum wawili ambao ni yeye na Hilda Ngoye.

‘’Najivunia nafasi niliyonayo maana imenipa na nafsi ya kuwa Mbunge wa Bunge la Ulaya nikiwakilisha Tanzania’’ anasema Dr. Mwanjelwa.

Alipoulizwa kuwa tangu achaguliwe kuwa Mbunge wa mkoa huo amefanya nini cha kujivunia mpaka sasa, alisema ameweza kuwainua makundi mbalimbali hasa wanawake wa wilaya zote za mkoa wa Mbeya.

Anasema anapenda sana kushiriki katika shughuli za kimaendeleo za jumuiya na hata familia moja moja.

‘’Kuanzia mwaka 2010, kwa kukumbuka baadhi ya niliyoyafanya ni pamoja na kujumuika na kuwasaidia yatima,  kusaidia vikundi vya akina mama na kufadhili semina za madiwani wa vyama vyote juu ya utendaji bora’’ anasema Dr. Mwanjelwa.

Elimu.
Anataja maeneo ambayo amewahi kujumuika na jamii kuhusu elimu kuwa ni  kushona sare za shule nguo na viatu kwa watoto yatima 100 kata za Kambasegele na Kiwira wilayani Rungwe.


Anasomesha watoto yatima 2 wa kike kila wilaya za mkoa wa Mbeya ambazo ni Mbeya mjini, Kyela, Rungwe, Mbeya Vijijini, Mbarali, Chunya, Ileje na Mbozi.

Si hayo tu bali nimesaidia ujenzi wa sekondari kata ya Itagano-Jiji la Mbeya, mifuko ya saruji tani Moja, ujenzi wa sekondari ya kata ya Ruanda saruji tani Moja na niligawa vitabu katika sekondari 9 zote za mkoa wa Mbeya, kila wilaya shule Moja na Kugawa vitanda 19 katika hosteli ya wasichana Sekondari ya Isansa ’’ anasema Mbunge huyo.

Ujasiliamali

Anasema amefanikiwa kuanzisha vikundi vya ujasiriamali kwa kina mama kila wilaya -zote za mkoa wa Mbeya na  kufadhili Mashine za kutotolea vifaranga na kutoa pesa za mitaji wilaya zote za mkoa wa Mbeya.

‘’Nilitoa mafunzo ya ujasiriamali kwa kina mama juu ya incubators hizo nilizowafadhili ili waweze kuendelea kujitegemea katika kukuza uchumi wao badala ya kuwa wategemezi kila wakati na niliendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wana Mbeya kwa kuzingatia jinsia’’ anasema Mbunge huyo.

Aliwezesha kaya 300 mbuzi wawili wawili  kaya -kata ya Kambasegela na Kiwira wilayani Rungwe.

Afya
Anaeleza kuwa ni mambo mengi ya jamii aliyoshiriki na mengine ameyasahau lakini anakumbuka pia aligawa magodoro 250 katika hospital za serikali katika wadi za wazazi wilaya ya Ileje, Mbozi, Chimala(Mbarali), Ruanda na hospitali ya Rufaa ya Mbeya kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya.

Aidha anasema amegawa vitanda 19 katika hosteli ya wasichana Sekondari ya Isansa iliyopo wilayani Mbozi, kutoa gari ya sinema katika Jiji la Mbeya juu ya uelimishaji Umma katika Tiba kwa Kadi kupitia mfuko wa Bima ya afya ya Taifa(NHIF).

Kushiriki kampeni ya kufanya usafi katika Jiji la Mbeya.

‘’Nilitoa vyakula katika vituo cha watoto yatima cha Iwambi na kugawa nguo na mablanketi katika kituo cha watoto yatima cha Uyole vyote vya Jijini Mbeya’’ anasema Dr. Mwanjelwa.

Sanjali na vitu hivyo, anasema kuwa alitoa pia viti vya walemavu wa viungo katika Jiji la Mbeya mbele ya Askofu kiongozi wa kanisa la Moravian Tanzania Alinikisa Cheyo siku alipkuwa akimshukuru Mungu kwa kumponya na mauti katika ajali mbaya aliyoipata mwaka jana 2012.

Uongozi.

Katika masuala ya uongozi, anasema aliendesha na atazidi kufanya hivyo kwa kufadhili mafunzo/semina za mara kwa mara kwa Madiwani wote wa Mkoa wa Mbeya, juu ya Uongozi na uwajibikaji.

‘’Mbali na mafunzo ya madiwani hao, nimewahi kuendesha mafunzo/semina kwa watendaji wote wa ngazi ya kata juu ya Uongozi na uwajibikaji na nitazidi kufanya hivyo’’ anasema.

Anajipambanua kuwa pia amewahi kuendesha mafunzo/semina kwa wenyeviti na makatibu wa umoja wa wanawake wa chama chake UWT katika wilaya zote za mkoa wa Mbeya jinsi ya Uongozi na Uwajibikaji.

Mbali na kazi za kijamii, anasema mara kadhaa huwa anashiriki kazi za kusaidia vikundi, waimbaji na hata makanisa ambapo hivi karibuni alitoa vyombo vya Muziki Kanisa la Ruanda Moravian kwaya Kuu Jiji la Mbeya.

Mbali na makanisa anaeleza kuwa anashiriki pia kusaidia michango mbali mbali ya kijamii kama vile-michango misikitini, makanisani, matamasha, harambee n.k

Alipoulizwa kuwa kuwa anapenda nini katika utumishi wake wa Ubunge, anasema anapendelea sana na atazidi kuhimiza/kuhamasisha uanzishwaji wa vikundi vya aina  mbali mbali vya ujasiriamali, Sanaa n.k. kwa wa kina mama, vijana na wazee.

Kuhusu ajali aliyoipata

Anasema kwa sasa alirudi nyuma kidogo katika kufanya kazi hizo za kuikomboa jamii kiuchumi kutokana na ajali mbaya aliyoipata mwaka jana 2012 katika mteremko wa mlima Iwambi eneo la Mbalizi wilaya ya Mbeya ambayo ilisababisha kifo cha msaidizi wake.

‘’Ajali mbaya niliyopata mwaka jana ilinikwamisha mambo mengi nilikuwa nimepanga kuendelea kuteketeleza Ilani ya CCM lakini namshukuru Mungu afya yangu inaimarika na nitazidi kuwatumikia ndugu zangu wa Mbeya kutoka rohoni, ndivyo nilivyo asili mwana jamii hata kabla sijawa Mbunge, Mungu anisaidie niwatumikie kwa maendeleo na tukishirikiana wote vema tutajikomboa katika mengi’’ anasema Dr. Mary Mwanjelwa.

Kuhusu kugombea tena mwaka 2015, anasema kuwa Mungu akimpa kibali na afya njema atagombea na anaamini sifa anazo za kuendelea kuwa Mbunge wa Jimbo ama viti maalum.

Jumamosi, 18 Januari 2014

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA MBEYA,DK MARRY MWANJELWA ALIPOTEMBELEA WAJAWAZITO NA KUKABIDHI MISAADA YA MAGODORO

 Dr Marry Mwanjelwa akabidhi magodoro yenye thamani za zaidi ya shilingi milioni 6, kwa Hospitali ya Rufaa Meta, Kituo cha Afya Mwanjelwa jijini Mbeya na Hospitali ya wilaya ya Ileje, Mbozi na Mbeya Vijijini.
 Akina Mama wakishangilia ujio wa Mtetezi wao Dk Marry Mwanjelwa ambaye ni Mbunge wa Viti maalum
 Dr Marry akisalimiana na mmoja wa madaktari wa Hospitali ya Rufaa Meta.
 Dr Marry akipata maelezo mafupi ya ujio wake katika Hospitali ya Meta.
 Dr Marry akisalimiana na akina Mama wajawazito katika Kituo cha Afya Mwanjelwa
  Dr Marry Mwanjelwa akipewa utaratibu na maelezo kutoka kwa Muuguzi mata baada ya kutembelea wodi la akina Mama Wajawazito.
 Dr Marry akisalimiana na kuwafariji akina Mama wajawazito
 Dr Marry akitazama Kichanga
Katika utoaji wa misaada hiyo ya Magodoro unaendelea kutolewa ambapo Hospitali ya Meta walikabidhiwa magodoro 60, Mwanjelwa walikabidhiwa magodoro 60, na Hospitali ya Ileje magodoro 60, Hospitali ya Mbozi magodoro 59 na Mbeya vijijini magodoro 60.

Ijumaa, 17 Januari 2014

WAZAZI WAPINGA KULAZIMSHWA WATOTO WAO KUJIUNGA NA ELIMU YA WATU WAZIMA



 Wananchi wakisikitika kutokana na majibu ya wakubwa....
 Baadhi ya wazazi wakiwa wanaangalia majina ya watoto wao, katika ubao wa matangazo ya shule ya sekondari Usongwe.

BAADHI ya wazazi wa kata ya Utengule Usongwe, wilaya ya Mbeya Vijijini, wametibua mpango wa kuchangishwa fedha harakaharaka, ili watoto wao waanze kidato cha kwanza kupitia elimu ya watu wazima.

Mpango huo ulikuwa ukiratibiwa na kitengo cha Elimu ya watu wazima mkoa wa Mbeya chini ya Mkufunzi mkazi wa taasisi hiyo Danstan Msamada, kupitia shule ya Sekondari Usongwe iliyopo eneo la Mbalizi.

Baada ya baadhi ya wananchi kushtukia suala hilo, walimpigia simu Diwani wa kata hiyo, Elia Mkono(Chadema), ambaye alianza kufuatili kisha kuitisha mkutano wa wazazi, walimu na Mkufunzi wa taassi hiyo.

Katika kikao hicho kilichofanyika leo katika ukumbi wa shule ya Sekondari Usongwe, wananchi waliuliza maswali 22, ambayo wakati wa kujibiwa, zilitokea zomeazomea kwa kiongozi wa taasisi hiyo na baadhi ya walimu.

Mwananchi Harun Abdalah, aliuliza kuwa iweje baadhi ya watoto wenye wastani wa alama C, wachukuliwe kwenda taasisi ambayo inaendesha elimu katika mfumo usio rasmi?

Benard Tawete, alisema kuwa huo ni mpango wa biashara (dili), kati ya Mkuu wa shule ya Usongwe na taasisi hiyo ili kujipatia fedha kutoka kwa wazazi kwasababu iweje, fomu wazazi wachukue katika shule ya Usongwe kisha wanafunzi wakasome Taasisi iliyopo mbali na shule hiyo?

Wananchi wengi waliulza maswali ambayo, yakawa mwiba kwa baadhi ya viongozi na kushindwa kuyajibu kwa ufasaha kisha kuzomewa.

Afisa Mtendaji wa kata hiyo, Godwin Kaunda, aliamua kujitoa katika zomea zomea hiyo, kwa kuweka wazi kuwa ofisi yake baada ya kulipata jambo hilo aliwakataza wahusika kubandika majina hayo kwenye ofisi yake kabla wananchi hawajaelimishwa, lakini alishangaa kuona kuambiwa majina hayo yamebandikwa siku chache shuleni na wazazi kuanza kuchukua fomu.

Ukweli huo ulimwondoa katika doa la kuwa mmoja wa washiriki wa jambo hilo ambalo wananchi walisema kuwa awali walilaghaiwa kuwa watoto wao walikuwa wamefaulu kwenda huko na kutakiwa kulipa karo ya Tsh.200,000/=, na michango mingine zikiwemo fedha za madawati Tsh.15,000/=, vitambulisho Tsh. 5,000/=, ulinzi Tsh. 5,000 na fomu Tsh.5,000/=.

Diwani wa kata hiyo, Elia Mkono ambaye pia ni mwenyekiti wa Kijiji cha Mbalizi, aliwaambia wananchi kuwa yeye hawezi kuwaambia wananchi kuwa huko wanakotakiwa wawapeleke watoto wao ni kuzuri au kubaya.

“Jaribuni kupima wenyewe, kwasababu hata mimi nimepata takwimu za wanafunzi ambao majina yao yameenda huko Taasisi baada ya kupambana na kulazimisha kupata taarifa zaidi!’’ alisema Mkono na kuanza kufafanua zaidi.

Alisema mpaka sasa, wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na shule mbili za serikali zilizopo katika kata yake katika mfumo maalum ni 601.

Lakini alisema kuwa wakati shule hizo mbili zina idadi ya wanafunzi 601, Taasisi ya elimu ya watu wazima kwa shule moja, imechagua majina ya wanafunzi 493, hali ambayo alisema wazazi wenyewe wachanganue kama wakiwapeleka watoto wao huko watapata elimu bora au la.

Akijibu maswali zaidi, Mkufunzi mkazi wa elimu ya watu wazima huku mara kadhaa akiomba radhi, alisema kuwa taasisi hiyo ni ya serikali na majina hayo ameyatoa serikalini kwa wanafunzi ambao wana wastani wa alama D.

‘’Kama mnaona mfumo huu hamna imani nao msiwalete wanafunzi lakini kwa wale walioelewa wawalete wanafunzi ambao watafundishwa na walimu kutoka hapa shule ya Sekondari Usongwe, wakitoka kufundisha wanafunzi waliopo kwenye mfumo maalum’’ alisema Msamada.

Baadhi ya walimu wa shule ya Usongwe waliozungumza na Mwandishi wa habari hizi shuleni hapo kwa makubaliano ya kutoandika majina yao, walisema wanashindwa kwenda kufundisha vema katika taasisi ya elimu ya watu wazima kutokana na kupewa ujira mdogo.

Waliutaja ujira huo wanaolipwa kwa mwezi kuwa ni Tsh.20,000/= wakati hata wasipokwenda huko hakuna sheria inayowabana kwasababu mikataba yao ya kazi haielezi kuwa watakuwa na kazi nyingine ya kufundisha au kujitolea katika taasisi hiyo.

Kwa takwimu zilizopatikana, zinaonesha kuwa, katika kata hiyo, kuna shule za msingi 13 ambazo zimetoa wanafunzi wa elimu katika mfumo rasmi kama ifatavyo na wanafunzi kwenye mabano.

Shule ya Msingi, Mlima reli(87), Jitegemee(60), Mapambano(35), Mtakuja(100), Mkombozi(117), Mbalizi Moja(96), Onicar(37), Utengule(41), Itimba(5), Idugumbi(6), Iwala(10), Igunga(6) na Iwanga(1).

Taasisi ya elimu ya watu wazima imejinyakulia Mlimareli(47), Jitegemee(124), Mapambano(35), Mtakuja(54), Mkombozi(46), Mbalizi Moja(31), Iwanga(32), Itimba(30), Igunga(28), Iwala(23), Utengule(18) na Idugumbi(25).

Mkutano huo uliisha huku baadhi ya viongozi akiwemo WEO, kuondoka na makubaliano yalikuwa hakuna ulazima wa kumlazimisha mzazi kuchukua fomu ili wanafunzi hao waende kusoma kwenye mfumo huo ambao siyo rasmi na ziachwe propaganda kuwa watoto hao wamefaulu kwenda huko.
 
Chanzo; kalulunga.com

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...