Alhamisi, 4 Juni 2015

LUTENGANO MWALWIBA (kulia), AKIWA NA MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA MBEYA, DKT. MARY MWANJELWA


MAKUSANYO YA KAHAWA MKOANI YASHUKA






MAKUSANYO ya zao la kahawa mkoani Mbeya yameshuka kutoka tani 340 mwaka juzi hadi kufikia tani 120 mwaka jana kutokana na mgogoro wa kimaslahi ulioibuka kati ya Shirikisho la Vikundi vya Wakulima wa Kahawa Tanzania, SHIVIWAKA na baadhi ya wadau wa zao hilo.

Mwenyekiti wa SHIVIWAKA, Edward Masawe, alisema hali hiyo ilitokana na kampuni moja ya ununuzi wa kahawa mkoani hapa kuwarubuni baadhi ya wakulima waliokuwa wanachama wao na kusababisha kutouza kahawa yao kwa shirikisho hilo.

Masawe, alitoa taarifa hiyo wakati wa mkutano Mkutano wa mwaka wa shirikisho hilo ulioambatana na uchaguzi mkuu wa viongozi wake.

Alisema mgogoro huo wa kimaslahi ulitokana na msimamo wa SHIVIWAKA wa kuwahamasisha wakulima kutokubnali kuuza kahawa yao kwa bei nafuu kwa wanunuzi wanaotaka kuwanyionya wakulima hivyo kusababisha baadhi ya wanunuzi hao kulichukia shirikisho hilo.

“Kimsingi changamoto hii imetuathiri kwa kiasi kikubwa katika ununuzi wa kahawa kutoka kwa wakulima kwani baadhi yao walikataa kuuza kahawa yao kwa SHIVIWAKA na kuwauzia wengine na kusababisha makusanyo yetu kushuka ktoka tani 340 hadi 120.” Alisema Masawe.

Baadhi ya wakulima wa kahawa walisema wakulima wengi bado hawana ufahamu mzuri wa kubaini ujanja unaofanywa na wanunuzi katika kuwanyonya haki zao hivyo wamewashauri kuwa makini katika uuzaji wa kahawa yao.

Neema Mwaogoma, mkulima kutoka Mbozi alisema wakulima wengi wana haraka ya kuuza kahawa yao ili kujipatia pesa za haraka lakini hawachunguzi kwa makini bei zinazotolewa na wanunuzi hao.

Akitoa mfano, Neema, alisema katika msimu uliopita baadhi ya wakulima waliouza kahawa yao kwa wanunuzi binafsi waliuza kwa bei ya kati ya shilingi 3,000 hadi 3,500 kwa kilo moja wakati SHIVIWAKA ilinunua kahawa hiyo kwa bei ya shilingi 5,000.

Kutokana na hali hiyo, Masawe, alisema SHIVIWAKA imeweka mikakati ya kuwashawishi wakulima wa kahawa kuliamini shirikisho hilo na kuendelea kuliuzia zao hilo badala ya wanunuzi binafsi.

Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja kufungua vituo vipya vua ununuzi wa kahawa katika maeneo ya wakuima, kuongeza bei ya zao hilo na kuimarisha mfumo wa uongozi wa shirikisho hilo.

Jumanne, 2 Juni 2015

HOTUBA YA PROF. MARK MWANDOSYA AKITANGAZA NIA MBEYA JANA TAREHE 1.6.2015, KATIKA VIWANJA VYA MKAPA HALL, HII HAPA.


PROFESA M. J. MWANDOSYA 

Nianze kuwa kumshukuru Mwenyezi Mungu,muweza wa yote kwa rehema nyingi alizotushushia kutuwezesha kuifikia siku hii ya leo.
 

Kwani hatukustahili zaidi ya wengi waliotutangulia mbele za haki. Nawashukuru ninyi nyote mliofika kuungana nami katika siku hii muhimu katika kukuza,kuimarisha na kuendeleza demokrasia ndani ya Chama chetu,Chama Cha Mapinduzi. 
 

Wazee wangu,  Waheshimiwa Maaskofu, Viongozi wa Dini na madhehebu mbalimbali,Waheshimiwa viongozi wa kimila,Waheshimiwa Machifu,Mama yangu Helena Mwaipasi, Mzee wangu Chifu Mwakibwili,akina mama,vijana,WanaCCM wenzangu,Viongozi wa vyama vya siasa,Wananchi,Wana Mbeya, Wajumbe wa NEC ya CCM Taifa,Wahashimiwa Wabunge wenzangu, Marafiki zetu kutoka Zanzibar,Watanzania wenzangu.
 

Asanteni sana kwa uwepo wenu, na pale popote mnapotusikiliza na kutuona.Nawashukuru. Nimehemewa.



Ndugu zangu, Kwa muda mrefu na kwa njia mbalimbali za mawasiliano mmekuwa mkinidadisi Mbona kimya kuhusu mwaka 2015? Pamoja na kwamba mliutaja mwaka tu, lakini niliwaelewa.
 

Wengi mliushangaa ukimya wangu.Pamoja na kwamba ukimya ni sehemu ya haiba yangu na daima nimeupokea kama ni karama aliyonitunuku Mwenyezi Mungu,Muweza wa yote,baadhi yenu niliwajibu " Ukimya una Kishindo"! 
 
 

Kuhusu Sultan Qabus wa Oman,mwandishi mmoja maarufu aitwae Robert Kaplan amemwelezea ifuatavyo: Ni mtu mkimya, mpole, hapendi kuzungumza na waandishi wa habari mara kwa mara, hapendi habari zake ziandikwe kwenye magazeti mara kwa mara,lakini ameibadilisha nchi ya Oman kutoka makundi hasimu ya makabila na kuwa taifa linaloheshimika na linaloendelea kwa kasi sana na kuwa mfano wa kuigwa...." Sijifananishi na Sultan Qabus, la hasha.
 
 

Isipokuwa najaribu kusisitiza kwamba mara nyingi ni bora katika maisha kuwa mjenga hoja na mtendaji makini kuliko kuwa  mpayukaji na mwenye maamuzi ya papo kwa papo yenye matokeo hasi na yenye hasara kwa taifa. 
 
 

Nimeenda nje kidogo ya mada yangu!


Kwa staili ya siku hizi wagombea watarajiwa huwa tunajitokeza na kusema : tutatangaza nia siku hii au ile! Nadhani tunawashangaza na mtuwie radhi. 


Kwani kwa kusema hivyo tunakua  tayari tumetangaza nia!Basi nami kwa staili hiyo hiyo naomba kutangaza rasmi mbele ya kadamnasi hii kama mashahidi,kwamba  kwa unyenyekevu mkubwa, nitaomba ridhaa ya kuchaguliwa kuwa mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
 

Natarajia kuendeleza rasmi safari niliyoianza leo kwa kuchukua fomu za maombi hayo pale Dodoma,Makao Makuu ya CCM, jumatano, tarehe 3 Juni,2015, saa 4 barabara.



Kipindi cha mpito kutoka awamu moja ya uongozi kwenda awamu nyingine kingekuwa kigumu sana kwa nchi nyingi hasa nchi zetu za kiafrika. Mifano iko wazi.Majirani zetu wamepata shida.Lakini waasisi wetu Hayati Mwalimu Nyerere na Hayati Abeid Amani Karume wametujengea misingi imara. 
 

Tuna kila sababu ya kuwashukuru na tuna kila sababu ya kujivunia misingi hiyo.

 
CCM haijayumba na CCM haitayumba. Baadhi ya wanachama inawezekana wameyumba. Hebu tuzirudie Ahadi za mwana CCM: binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja; nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote; nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma;rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa; cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu binafsi; nitajielimisha kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote; nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu; nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika nzima; nitasema kweli daima fitna kwangu ni mwiko. Hii ndiyo CCM tunayoijua na atoaye ahadi mbele ya Mwenyezi Mungu ndiye Mwana CCM,na si vinginevyo.
 
 


Ahadi ya mwanaCCM ya kuondoa umaskini inanipa nafasi ya kuelezea na kusisitiza kipaumbele muhimu sana cha serikali iliyodhamiria kuwaondoa wananchi wake kutoka lindi la umasikini ni kukuza uchumi,uchumi wa kisasa,uliojikita katika misingi ya sayansi na teknolojia na kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano kama kichocheo cha maendeleo hayo.
 
 

Kama sayansi na teknolojia  ndio msingi wa uchumi wa kisasa basi naweza kusema,tena kwa unyenyekevu mkubwa kwamba aliye mbele yenu ndiye pekee mwenye ujuzi,uelewa,na uzoefu wa masuala haya. 
 

Ninalotaka kusisitiza hapa ni kwamba kukuza na kusimamia uchumi ndio utakuwa kipaumbele namba moja. Jenga kwanza uchumi imara na mengine yatafuata.


Uchumi imara unajengwa hasa pale panapokuwa na lengo la kitaifa.Lengo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ni Tanzania kufikia nchi yenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025. 
 

Lengo hilo liliwekwa mwaka 2000. Tudhamiria sasa kwamba ifikapo mwaka 2030 Tanzania iwe nchi  za juu zenye kipato cha kati (High Middle Income),na kwamba ifikapo 2050 Tanzania iwe nchi iliyoendelea.
 


Tunawezaje kuyafikia malengo hayo? Tunawezaje kukuza uchumi na ukuaji huo uwe endelevu?Hili ndilo swali.
 

1.Kilimo cha kisasa na cha kisayansi kupitia matumizi zaidi na bora ya mbolea; kuendeleza utafiti kwa kuboresha miundombinu,vifaa, na kuendekeza rasilimali watu;kuboresha mifumo na aina ya mikopo kwa wakulima wadogo; kuboresha barabara za vijijini; kuendeleza ujenzi wa maghala kwa ajili ya kutunza nafaka;kuwa na migumo ya uhakika ya masoko ya mazao;na kuhakikisha kiwanda cha kimkakati cha mbolea itokanayo na gesi asilia kinajengwa haraka iwezekanavyo.
 

2.Kuanzisha na kuendeleza viwanda,kwa kuanzia viwanda vinavyoongeza thamani ya mazao na rasilimali asili
 

3.Kuendeleza kilimo cha umwagiliaji ili kuwa na uhakika wa upatikanaji wa chakula.
 

4.Kuendelea kusimamia kutengemaa kwa uchumi mpana
 

5.Kuondoa vikwazo vinavyozuia uwekezaji wa ndani na kutoka nje
 

6.Kuhakikisha sekta ya utalii inakuwa ipasavyo kwa kufungua fursa nyingi za utalii wa ndani na utalii katika sekta ya kusini.
 

7.Kuongeza tija katika utendaji wa kazi kwa kuthamini kazi (kufanya kazi kwa bidii,kwa uadilifu,na kwa kujituma), kusimamia kanuni,maadili na miiko ya utumishi wa umma na kuufanya utumishi wa umma usiwe wa mazoea tu bali wa ushindani unaopimika katika kutoa huduma kwa wananchi. Hii itakwenda sambamba na kulinda haki na kuboresha msilahi ya wafanyakazi.

 
8.Kuchukia,kuzuia na kupambana na ufisadi na rushwa. Kuondoa vikwazo vinavyoonekana kuwepo  kwa matabaka mawili ya wananchi; wale wanaoshughulikiwa na takukuru moja kwa moja,na wale ambao kibali kinahitajika kuwashtaki,kwa kuipa Takukuru uwezo wa kisheria kufanya kazi bila kuingiliwa na chombo chochote,wakati huohuo kuhakikisha haki za wananchi wema zinalindwa kupitia chombo cha kusimamia malalamiko (ombudsman).
 

9.Kuendeleza na ikibidi kuimarisha uhuru wa Benki Kuu  na uhuru wa vyombo vya udhibiti wa huduma za kiuchumi,mifuko ya jamii, bima.
 

10.Serikali kuwa injini ya ukuaji wa uchumi lakini kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi,mtu mmoja,vikundi vya wajasiriamali,saccos,na kampuni binafsi kuchochea ukuaji wa uchumi.



Uchumi unapokua,basi serikali itakuwa katika nafasi nzuri ya kutekeleza vipaumbele katika maendeleo ya jamii: Elimu, maji safi na salama,afya, na miundombinu. Kuhusu elimu,lengo litakuwa ni kuboresha mitaala ili iendane na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ngazi zote;kuhakikisha kila mtanzania ana nafasi sawa ya kujiendeleza kielimu kuanzia ngazi ya awali mpaka elimu ya juu; kuendeleza elimu ya ufundi na kilimo; kuandaa na kutekeleza mipango kwa hatua kuifanya elimu ya msingi ifikie kidato cha pili, cha nne na hatimaye kidato cha sita;kuongeza wingi wa udahili  wa wasichana katika katika ngazi ya elimu ya juu;kuboresha hali na ari ya utendaji wa  kazi kwa walimu,ikiwa ni pamoja na ujenzi nyumba za kuishi na kuongeza ujira.



Katika maeneo mengine ya huduma za kijamii,lengo la serikali litakuwa ni kutekeleza sera zilizopo na kuhakikisha malengo yanatekelezwa na yanapimika.Katika kuleta afya bora kwa wananchi lengo litakuwa ni kuweka mizania katika kuzuia na kupambana na magonjwa.



Uchumi hauwezi kukua pasipokuwa na amani na utulivu. Amani usalama na utulivu ni tunu.Waasisi wetu wametujengea msingi wa tunu hii. Viashiria vya kupotea kwa amani vinaanza kuonekana kutoka ndani na nje.


Hali inahitaji kuimarisha vyombo vyetu vya usalama katika maeneo yote hususan mafunzo,vitendea kazi,vifaa, miundombinu na silaha za kisasa.
 

Hatimaye ulinzi wa nchi unaanzia mwananchi mwenyewe.


Nafasi ya Zanzibar katika ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni kubwa. Hii inatokana na asili na haiba ya nchi zenye visiwa, Zanzibar ikiwa mojawapo. Historia ya Zanzibar inatukumbusha hili.Kwani katika karne ya kumi na tisa Zanzibar iliongoza eneo lote la Afrika ya Mashariki kiuchumi na maendeleo,ukuondoa biashara ya utumwa.
 

Ilisemekana Ikipigwa zumari Zanzibar wanacheza ngoma maziwa makuu. Kila linalowezekana litafanywa kuondoa kabisa hali inayoweza kuikwaza Zanzibar kufikia uwezo wake mkubwa kiuchumi.Muungano utaimarika na uchumi wa Tanzania utakuwa kwa kasi zaidi.



Nahitimisha na suala muhimu la uzalendo.Kwa tafsiri isiyo rasmi,Uzalendo  ni upendo kwa nchi. Tumeanza kushuhudia kupungua kwa uzalendo. Upungufu huo unajionesha katika kuenzi tamaduni za nje,kubeza juhudi za maendeleo yaliyopatikana, viongozi kutoa matamshi yanayo kebehi nchi wakiwa nje ya nchi,kutojivunia historia yetu iliyojikita katika michango ya mashujaa wetu. Hawa ni pamoja na  wale waliopambana na wakoloni,akina Kinjeketile,  Mkwawa ,Mirambo, Chaburuma na wengineo ambao walitoa uhai wao kulinda na kutetea heshima ya mwafrika dhidi ya ukoloni.Aidha waasisi wa TANU,Hayati Mwalimu Nyerere,Sykes,Mzee Kawawa, na wenzao;
 

Waasisi wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume na wenzake akina Mzee Thabit Kombo,Kanali Seif Bakari,Hamis Darwesh,Edington Kisasi,Yusuf Himpid,Said Washoto na wengineo;ambao walionesha upendo na uzalendo wa hali ya juu.Vilevile tuna mashujaa wa ukombozi wa Kusini mwa Afrika akina  Sebastian Chale,George Magombe na Hashim Mbita na wanajeshi wetu waliopoteza maisha yao katika mapambano ya ukombozi wa Afrika. 
 

Tutaendelea kuenzi, kuthamini,na kuiendeleza  mchango mikubwa wa Marais wetu wastaafu,Mzee Aboud Jumbe, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Hayati Idris Abdulwakil,Dr Salmin Amour,Dr Amani Abeid Karume,na Mzee Benjamin William Mkapa.



Kipekee napenda kuwashukuru Marais wetu wa sasa; Mheshimiwa Dr Jakaya Mrisho Kikwete,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,na Mheshimiwa Dr Ali Mohamed Shein ambao wamefanya kazi kubwa ya kuimarisha uchumi na umoja wa nchi yetu. Daima nitaenzi mchango wao.

 
Naishukuru familia yangu,Mke wangu Lucy,Watoto wetu Max, Sekela, na Emmanuel.Nawashukuru wazazi wangu ambao wametutangulia mbele za haki.
 

Wazee wa Mbeya na Lufilyo walionilea, Nawashukuru kwa michango yenu, ni baraka zitakazonifikisha Magogoni.


Tujivunie Nchi Yetu; na Kwa Pamoja Tutaijenga  Tanzania tunayoitaka.
 

Jumatatu, 1 Juni 2015

MWANAMKE MWENYE HEKIMA NI NGUZO YA FAMILIA NA TAIFA LENYE MAADILI MEMA.

MCHUJO WA SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 WAANZA LEO JIJINI DAR

 Eluka Kibona, Meneja Utetezi na Ushawishi wa Oxfam akielezea juu ya shindano la Mama shujaa wa Chakula na kumkaribisha Mgeni Rasmi kufungua rasmi hafla ya Maamuzi ya fomu za shindano la Mama shujaa wa Chakula 2015 leo.
 Muwakilishi wa Mgeni Rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa TBS Joseph Masikitiko  katika Hafla ya maamuzi ya fomu za shindano la mamashujaa wa Chakula Bi. Stella E. Mrosso ambaye ni Mkuu wa mahabara ya Chakula TBS akifungua rasmi hafla hiyo ya kuanza kuzihakiki fomu hizo .
 Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akiwashukuru TBS , Majaji pamoja na washiriki ambao ndio watazipitia fomu hizo kabla hazijafika kwa majaji.
 Mratibu wa Programu kutoka Care International in Tanzania Maureen Kwilasa akisisitiza jambo wakati wa Hafla hiyo
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster, Mkuu wa maabara chakula TBS Stella E. Mrosso, Tusfaye Legesse Obole President's Delivery Bureau, Manager Agriculture Productivity na  Mratibu wa Programu kutoka Care International in Tanzania Maureen Kwilasa wakiwa katika hafla hiyo.
 Mkuu wa maabara chakula TBS Stella E. Mrosso aliye Mwakilisha Mgeni rasmi katika hafla hiyo akimkabidhi rasmi fomu za shindano la mama shujaa wa chakula  Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster kwa ajili ya kuanza kufanya maamuzi.
Vijana wenye fani mbalimbali  kutoka vyuo vikuu na taasisi mbalimbali  wakiwa katika mchakato kwa kuzipitia Fomu zote za maombi ya kushiriki shindano la mama shujaa wa Chakula 2015
 ******
 Shindano la mama shujaa wa chakula limeingia katika hatua mpya baada ya zoezi la kukusanya fomu za washiriki kutoka mikoa mbalimbali nchini kupitiwa na majaji kwa ajili ya mchujo ambapo washiriki 18 watapatikana kisha baadaye 15 bora ambao wataingia kijijini kwa ajili ya mchakato wa kugombea nafasi ya mama shujaa wa chakula mwaka 2015.

zoezi la kusahihishwa fomu  limezinduliwa mapema leo hii na mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TBS, Joseph Masikitiko ambaye ni Mkuu wa Maabara na Chakula TBS, Bi. Stella Mrosso akiwa sambamba na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Oxfam Tanzania, Jenny Foster na majaji watakaopitia zoezi zima la mchujo wa fomu hizo.

 akizungumza na wageni waandishi wa habari katika uzinduzi huo Mkuu wa Maabara na Chakula, Bi. Stella Mrosso alilisifu shirika la Oxfam kuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za wanawake, umiliki wa ardhi na kuhamasisha uzalishaji wa chakula kwa wazalishaji wadogo wadogo.

Bi. Stella alisisitiza kuwa kila mzalishaji anapaswa kuzalisha bidhaa bora ili kushindana na soko la ndani na la nje huku akifafanua kuwa kwa kupitia SIDO, TFDA na Wizara ya Afya, wazalishaji wadogowadogo watakuwa na uwezo wa kupata kibali kutoka TBS bure na kuongeza kuwa wakina mama nchini watumie shindano la mama shujaa wa Chakula kama chachu ya kujitokeza kwa wingi katika mashindano yanayofuata huku wengine wakijifunza uzalishaji bora kupitia mashindano hayo.

Serikali yatoa changamoto kwa watafiti wa sayansi ya afya


SERIKALI imewaomba watafiti wa masuala ya afya hapa nchini kuhakikisha kwamba wanaibua hoja mpya zitakazosaidia kuleta mabadiliko kwenye sera za kitaifa zinazohusu sekta hiyo muhimu. Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu Wizara ya Afya na ustawi wa jamii Dk. Donan Mbando mara tu baada ya kufunga mkutano mkuu watatu wa sayansi ya afya uliondaliwa na chuo kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi cha Muhimbili (MUHAS).




“Kwa sasa taifa linashuhudia ongezeko kubwa la idadi ya watu wanaosumbuliwa na magonjwa yasiyoyakuwa ya mbukiza kama vile kisukari, shinikizo la damu na kisukari. Kwa bahati mbaya sana vituo vyetu vingi vya afya havijaandaliwa vizuri kukabiliana na magonjwa haya kwasababu sera zetu wakati zinaandaliwa hazikujika zaidi kwenye magonjwa yasiyoyakuwa ya kuambukiza na ndio maana tunahitaji mabadiliko kwenye hili,’’ alisema Dr. Mbando.




Dr. Mbando alizataja sababu kubwa zinazochangia ongezeko la magonjwa hayo kuwa ni pamoja na matumizi ya pombe kupita kiasi, aina ya vyakula vinavyotumiwa na watanzania hususani wale wanaoishi maeneo ya mijini, kutokufanya mazoezi pamoja na uvutaji wa sigara. Aidha aliiongeza kuwa kwa sasa serikali ipo kwenye mpango wa kuandaa mkakati  wanne wa huduma za afya hapa nchini (health care financing strategy) utakao muwezesha kila mtanzania kuwa na bima ya afya.




“Kwa sasa ni asilimia 20 tu ya watanzania ndio wanamiliki bima za afya zinazotolewa na shirika la bima ya afya la taifa na mashirika binafsi na hivyo kufanya asilimia 80 ya watanzania kuishi bila kuwa na uhakika wa masuala ya tiba….hili tumelianza tayari,’’ alibainisha.




Kuhusu mlipuko wa ugonjwa wakipundupindu kwenye mikoa ya kagera na kigoma uliosababishwa na kuingia kwa wakimbizi kutoka Burundi, Dr. Mbando alisema kwa sasa serikali kwa kushirikiana na Wananchi, wadau wa maendeleo na asasi zisizo za kiraia wanapambana kuhakikisha tatizo hilo linakwisha.




Akizungumza kwenye mkutano huo Makamu mkuu wa MUHAS, Prof. Ephata Kaaya alisema kwa sasa taifa linahitaji zaidi tafiti za kiafya hususani kwenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza na ndio sababu mkutano huo ulijikita zaidi kujadili tatizo hilo.




“Kama wataalamu wa masuala ya afya tunaona kuna haja kubwa tukiwekeza katika tafiti zinazolenga kuibua changamoto na suluhisho kwenye magonjwa haya,’’ alisema. Mkutano huo wa siku mbili ulihudhuriwa na washiriki zaidi ya 300 wakiwemo madaktari, viongozi na wanafunzi wa udaktari kutoka MUHAS na vyuo vingine vya afya.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...