Jumamosi, 31 Mei 2014

FAIDA ZA WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA VITUO VYA AFYA HIZI HAPA

IKIWA mkoa wa Mbeya una asilimia 57 ya wajawazito wanaojifungulia hospitali na vituo vya afya, wito umetolewa kwao kujitokeza kwa wingi kuhudhuria Kliniki ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mhadhiri, kaimu mkuu wa taasisi ya tiba ya St. Aggrey Jijini Mbeya, Dr. Karim Segumba.
Dr. Karim alisema kuwa faida wanazozipata wajawazito wanapohudhuria Kliniki ni pamoja na mjamzito kuchunguzwa afya yake kwa undani, ikiwemo umri wa mimba, kimo cha mimba, historia ya uzazi wa awali, uwingi wa damu, mkojo kwa protini na kutoa wasiwasi wa kifafa cha mimba.

‘’Mwanamke anachunguzwa shinikizo la damu, mlalo wa mtoto, mapigo ya moyo ya mtoto, ikibidi ultrasound kuangalia kama mtoto yupo hai, au ni mlemavu, ukubwa wa mtoto, kondo la nyuma la mama, kukomaa kwa mtoto, nyonga za mama kama zinaruhusu kujifungua kwa njia ya kawaida au upasuaji na anaelezwa tarehe ya makisio ya kujifungua’’ alisema Dr. Karim.

Mbali na uchunguzi huo, alisema kuwa mjamzito anayehudhuria kliniki anapimwa pia VVU na anapoonekana kuwa ana maambukizi anapewa mbinu za kumkinga mtoto aliye tumboni.

Alipoulizwa madhara yanayoweza kuwapata wajawazito ambao hawaendi kliniki na hawajifungulii hospitali na vituo vya afya, alisema ni pamoja na mjamzito kutoelewa maendeleo ya mimba yake na hatari ambazo zingeweza kugundulika na kutatuliwa na wataalam ili kuzuia kifo chake na mtoto.

‘’Hivyo ili kupunguza vifo vya mama na mtoto ni muhimu wajawazito wakahudhuria kliniki na kujifungulia katika vituo vya tiba na kizuri zaidi huduma zote hizo kwa mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano hutolewa bure kote nchini’’ alisema mhadhili huyo.

Mratibu wa huduma ya mama na mtoto katika hospitali ya mkoa wa Mbeya Prisca Butuyuyu, alisema kwa sasa mkoa wa Mbeya, wajawazito wengi wanahudhuria kliniki lakini wengi wao wanajifunguli nyumbani.

Aliitaja wilaya ya Ileje kuwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa wajawazito kujifungulia nyumbani, ambapo Jiji la Mbeya linaongoza kwa wajawazito wengi kujifungulia katika vituo vya tiba.

‘’Zaidi ya asilimia 40 wajawazito wanajifungulia nyumbani lakini baadhi wanajifungulia kwa wakunga wa jadi na njiani ingawa hatuna takwimu sahihi zaidi’’ alisema Butuyuyu.

Alisema Jiji la Mbeya wajawazito wanajifungulia hospitali hasa hospitali ya wazazi Meta kwa asilimia 109, Kyela 67, Chunya 58, Rungwe 55, Mbozi 45, Mbeya Vijijini asilimia 38 na wilaya ya Ileje asilimia 33.

FAIDA ZA WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA VITUO VYA AFYA HIZI HAPA

IKIWA mkoa wa Mbeya una asilimia 57 ya wajawazito wanaojifungulia hospitali na vituo vya afya, wito umetolewa kwao kujitokeza kwa wingi kuhudhuria Kliniki ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mhadhiri, kaimu mkuu wa taasisi ya tiba ya St. Aggrey Jijini Mbeya, Dr. Karim Segumba.
Dr. Karim alisema kuwa faida wanazozipata wajawazito wanapohudhuria Kliniki ni pamoja na mjamzito kuchunguzwa afya yake kwa undani, ikiwemo umri wa mimba, kimo cha mimba, historia ya uzazi wa awali, uwingi wa damu, mkojo kwa protini na kutoa wasiwasi wa kifafa cha mimba.

‘’Mwanamke anachunguzwa shinikizo la damu, mlalo wa mtoto, mapigo ya moyo ya mtoto, ikibidi ultrasound kuangalia kama mtoto yupo hai, au ni mlemavu, ukubwa wa mtoto, kondo la nyuma la mama, kukomaa kwa mtoto, nyonga za mama kama zinaruhusu kujifungua kwa njia ya kawaida au upasuaji na anaelezwa tarehe ya makisio ya kujifungua’’ alisema Dr. Karim.

Mbali na uchunguzi huo, alisema kuwa mjamzito anayehudhuria kliniki anapimwa pia VVU na anapoonekana kuwa ana maambukizi anapewa mbinu za kumkinga mtoto aliye tumboni.

Alipoulizwa madhara yanayoweza kuwapata wajawazito ambao hawaendi kliniki na hawajifungulii hospitali na vituo vya afya, alisema ni pamoja na mjamzito kutoelewa maendeleo ya mimba yake na hatari ambazo zingeweza kugundulika na kutatuliwa na wataalam ili kuzuia kifo chake na mtoto.

‘’Hivyo ili kupunguza vifo vya mama na mtoto ni muhimu wajawazito wakahudhuria kliniki na kujifungulia katika vituo vya tiba na kizuri zaidi huduma zote hizo kwa mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano hutolewa bure kote nchini’’ alisema mhadhili huyo.

Mratibu wa huduma ya mama na mtoto katika hospitali ya mkoa wa Mbeya Prisca Butuyuyu, alisema kwa sasa mkoa wa Mbeya, wajawazito wengi wanahudhuria kliniki lakini wengi wao wanajifunguli nyumbani.

Aliitaja wilaya ya Ileje kuwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa wajawazito kujifungulia nyumbani, ambapo Jiji la Mbeya linaongoza kwa wajawazito wengi kujifungulia katika vituo vya tiba.

‘’Zaidi ya asilimia 40 wajawazito wanajifungulia nyumbani lakini baadhi wanajifungulia kwa wakunga wa jadi na njiani ingawa hatuna takwimu sahihi zaidi’’ alisema Butuyuyu.

Alisema Jiji la Mbeya wajawazito wanajifungulia hospitali hasa hospitali ya wazazi Meta kwa asilimia 109, Kyela 67, Chunya 58, Rungwe 55, Mbozi 45, Mbeya Vijijini asilimia 38 na wilaya ya Ileje asilimia 33.

MWANAMKE MMOJA AUAWA KWA KUKATWA NA KITU CHENYE NCHA KALI SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI NA MUME WAKE.



MWANAMKE MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA CHRISTINA HAYOLA (35) MKAZI WA KIJIJI CHA LIWALANJE, ALIKUTWA AMEUAWA KWA KUKATWA KITU CHENYE NCHA KALI KICHWANI, KIFUANI NA MGUU WA KULIA  NA MUME  WAKE AITWAYE MUSSA NSAGAJE @ MWAULAMBO.

MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 06:00 ASUBUHI HUKO KATIKA KIJIJI CHA MAGAMBA, KATA YA ISANZA, TARAFA YA IGAMBA, WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA CHANZO CHA TUKIO HILO NI UGOMVI ULIOTOKANA NA WIVU WA KIMAPENZI ULIOTOKEA WAKIWA KILABUNI USIKU.

  MTUHUMIWA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO. JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAKE, VINGINEVYO AJISALIMISHE MWENYEWE.


KATIKA TUKIO LA PILI:

MTU MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA ABDI SANGA (20) MKAZI WA ISANGA ALIUAWA KWA KUPIGWA SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI WAKE  NA KUNDI LA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI WAKITUMIA SILAHA ZA JADI FIMBO, MAWE NA RUNGU.

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 31.05.2014 MAJIRA YA SAA 03:45 USIKU WA KUAMKIA LEO HUKO ENEO LA FOREST YA ZAMANI KATA YA FOREST, TARAFA YA  SISIMBA JIJI NA MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA CHANZO CHA TUKIO HILI NI TUHUMA ZA WIZI BAADA YA  MAREHEMU NA MWENZAKE MMOJA AMBAYE ALIFANIKIWA KUKIMBIA KUINGIA NYUMBANI KWA KASSIM ISSA (28)  MKAZI WA FOREST NA KUIBA VITENGE VYENYE THAMANI YA  TSHS 70,000/=,  MHANGA ALIPIGA KELELE ZA KUOMBA MSAADA, HIVYO KUNDI LA WATU WALIJITOKEZA NA KUMSHAMBULIA. 

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA INA MADHARA MAKUBWA NA BADALA YAKE WAWAFIKISHE WATUHUMIWA WANAOWAKAMATA KWA TUHUMA MBALIMBALI KATIKA MAMLAKA HUSIKA KWA HATUA ZAIDI ZA KISHERIA.


KATIKA TUKIO LA TATU:

MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU KATIKA SHULE YA MSINGI IBUMILA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA FATINA FESTO @ MWANDOSYA (12) MKAZI WA KIJIJI CHA MAHONGOLE ALIFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA  KUDONDOKA KUTOKA  KWENYE POWER TILLER ILIYOKUWA IKIENDESHWA NA AIZACK MWASHANGWA (22) MKAZI WA MAHONGOLE.

TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 15:30 ALASIRI HUKO KATIKA KIJIJI CHA IBUMILA-MAHONGOLE, KATA YA SONGWE-IMALILO, TARAFA YA RUJEWA, WILAYA YA MBARALI, MKOA WA MBEYA. WAKATI TUKIO HILO LINATOKEA MAREHEMU NA WENZAKE WALIKUWA WANATOKA KUVUNA MPUNGA WA SHULE. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. DEREVA ALIKIMBIA NA KUACHA POWER TILLER MARA BAADA YA TUKIO.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA [DEREVA] AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAKE, VINGINEVYO AJISALIMISHE MWENYEWE.


KATIKA TUKIO LA NNE:

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI KATIKA SHULE YA SEKONDARI MAKONGOLOSI ALIYEMBALIWA KWA JINA LA ADEN PETER @NGOMBE (17) MKAZI WA MAKONGOLOSI AMEFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.117 APK/T.150 AVM AINA YA SCANIA LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA AITWAYE ALLY MOSHI (35) MKAZI WA MBARALI.

TUKIO HILO LA AJALI LIMETOKEA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 13:00 MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI NA KATA YA MAKONGOLOSI, TARAFA YA KIWANJA WILAYA YA CHUNYA MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MAKONGOLOSI/LUPA. CHANZO CHA AJALI DEREVA ALIKUWA AMELEWAPOMBE. MTUHUMIWA AMEKAMATWA NA GARI LIPO KITUO CHA POLISI – MAKONGOLOSI.

 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WATUMIAPO VYOMBO VYA MOTO HASA KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI. AIDHA ANAENDELEA KUTOA WITO KWA WATEMBEA KWA MIGUU KUFUATA NA KUZINGATIA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI IKIWA NI PAMOJA NA KUTEMBEA PEMBENI MWA BARABARA NA KUVUKA KATIKA MAENEO YENYE VIVUKO VYA KUVUKIA ILI KUEPUKA AJALI.

TAARIFA YA MISAKO:

KATIKA MSAKO WA KWANZA:

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA MWIYULEGHE MBUGHI (60) MKAZI WA KIJIJI CHA ITENTULA AKIWA ANAMILIKI BILA KIBALI SILAHA /BASTOLA MOJA AINA YA   BABY YENYE NAMBA 946663 ILIYOTENGENEZWA NCHINI UBELGIJI IKIWA NA RISASI TATU [03] KWENYE MAGAZINE.

MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 01:00 USIKU WA KUAMKIA LEO HUKO KATIKA KIJIJI CHA ITENTULA, KATA YA   BARA, TARAFA YA ITAKA, WILAYA YA MBOZI, MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA ALIKUWA AMEKUFICHA SILAHA HIYO CHUMBANI NDANI YA   NYUMBA YAKE. TARATIBU ZA KUMFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA KWA JAMII KUACHA KUJIMILIKISHA SILAHA KINYUME CHA SHERIA NA BADALA YAKE WAFUATE TARATIBU ZA UMILIKAJI WA SILAHA KIHALALI.

KATIKA MSAKO WA PILI:

JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA DEZDERIS JACKSON (30) MKAZI WA KIJIJI CHA SAZA AKIWA NA KETE 17 ZA BHANGI KWENYE KIBANDA CHA KUUZA SABUNI SAWA NA UZITO WA GRAM 85.

MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 11:00 ASUBUHI HUKO KATIKA KIJIJI CHA SAZA, KATA YA   MKWAJUNI,   TARAFA YA   KWIMBA, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA NI MTUMIAJI NA MUUZAJI WA BHANGI.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.


KATIKA MSAKO WA TATU:

MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA EVA WILSON (23) MKAZI WA KIJIJI CHA BWAWANI ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA ANAUZA  POMBE KALI ZILIZOPIGWA MARUFUKU NA SERIKALI[VIROBA] AINA YA  BOSS PAKETI 51.

MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 14:00 MCHANA HUKO KATIKA KITONGOJI NA KIJIJI CHA BWAWANI, KATA YA MAKONGOLOSI, TARAFA YA   KIWANJA, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII HASA WAFANYABIASHARA KUACHA KUJIHUSISHA NA UUZAJI WA BIDHAA ZILIZOPIGWA MARUKUFU NA SERIKALI KWANI ZINA MADHARA KIAFYA KWA WATUMIAJI.


KATIKA MSAKO WA NNE:

MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA ESTER MWALUGAJA (34) MKAZI WA KIJIJI CHA MAMBA-F ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA   POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA MBILI [02].

MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE 30.05.2014 MAJIRA YA SAA 14:00 MCHANA HUKO KATIKA KITONGOJI CHA MTANDE, KIJIJI CHA MAMBA -F, KATA YA   MAMBA, TARAFA YA   KIPEMBAWE, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA MBEYA.


TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI WATUHUMIWA ZINAENDELEA.

            KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA ANATOA WITO KWA JAMII KUENDELEA KUTOA TAARIFA ZA WATU WANAOJIHUSISHA NA MTENGENEZAJI NA UUZAJI WA POMBE HARAMU YA MOSHI.


Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Ijumaa, 30 Mei 2014

MBEYA CITY FC YATINGA ROBO FAINALI CECAFA NILE BASIN CUP


 Table standings as per Wednesday 28TH/May 2014
Group ‘A’

NAFASI ZA KAZI


Apply Before: 07 Jun 2014
Company: Terre Des Hommes
Location > Dar Es Salaam
Position Description:
Terre Des Hommes Netherlands Is Re-
Advertising The Position Of A Programme Officer
To Be Based In Dar Es Salaam, Tanzania With
Frequent Travel To The Field. Terre Des
Hommes Netherlands Supports Services For
Children In Need Through Partner Organizations.
Objective Of The Position
To Ensure That The Project Partner
Organizations Of The Assigned Part Of The
Partner And Programme Portfolio Deliver
Effective And Efficient Services To Vulnerable
Children, In Line With Tdh Netherlands (Tdh)
Strategy, Policies And Procedures.
We Are Specifically Looking For Someone With:
• Ability To Work Independently, Well Organized,
Accurate Presentation And Writing Skills (Uk
English)

Jumanne, 27 Mei 2014

GHARAMA ZA MWENGE WA UHURU NI HIZI HAPA

Screen Shot 2014-05-27 at 11.27.07 AMBunge la bajeti linaendelea Dodoma Tanzania ( 104.4 CloudsFM ) ambapo leo May 27 2014 kwenye kipindi cha maswali na majibu asubuhi, moja ya majibu yaliyotolewa ni kuhusu uwepo wa mbio za mwenge na gharama zake.

Naibu waziri wa habari vijana utamaduni na michezo Juma Nkamia amesema ‘serikali kuu hutenga kiasi cha fedha kulingana na mahitaji na gharama halisi ya wakati husika ambapo mwaka 2012 jumla ya shilingi milioni mia sita hamsini (650) zilitengwa kwa ajili ya kuadhimisha uzinduzi na kilele cha mbio za mwenge wa uhuru na kati ya hizo milioni 450 zilitumiwa na Wizara na milioni 200 zilitumiwa na mkoa uliokua mwenyeji wa sherehe za kilele’

‘Kuhusu kiasi cha fedha kinachotumiwa na wilaya, ni kwamba zinatofautiana kulingana na michango ya Wananchi katika wilaya husika kwani michango hiyo ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo ambayo huzinduliwa wakati ya mbio za mwenge, kwa ujumla mwaka 2012 Wananchi walichangia zaidi ya BILIONI 11 na milioni 500′
Screen Shot 2014-05-27 at 11.26.46 AM‘Halmashauri za wilaya na manispaa zilichangia shilingi BILIONI 45, Wahisani na watu binafsi walichangia zaidi ya shilingi milioni 52 ambapo faida zinazopatikana kutokana na Mwenge wa Uhuru nchini ni pamoja na kuendelea kutunza historia na falsafa ya ukombozi wa taifa letu, kuhamasisha Wananchi kuhusu umuhimu wa kuendelea kuenzi amani, mshikamano, upendo na zaidi kupambana na ubaguzi wa dini, rangi au ukabila’

‘Mbio za mwenge wa uhuru hutumika kuhimiza miradi mbalimbali kwa njia ya kuweka mawe ya msingi au kuzindua miradi iliyowekewa jiwe la msingi mwaka uliopita na pia kuhamasisha moyo wa Wazalendo na kujitolea kwa vijana hasa kuonyesha umuhimu na nafasi yao katika kudumisha nchi yao, kulinda uhuru na kuleta maendeleo ya nchi yao’

Baada ya kusoma haya yaliyosemwa na Naibu waziri wa habari Juma Nkamia leo May 27 2014 bungeni, 
  
Credit; millardayo.com

Jumatatu, 26 Mei 2014

KINANA NA ZIARA YAKE JIMBO LA SINGIDA MJINI

DSC_0204
Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini, Mh. Mohammed Dewji (MO), Naibu Waziri wa Fedha ambaye pia Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Mh. Mwigulu Nchemba wakiwa kwenye boda boda, wakati wa msafara wa kuelekea kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika eneo la viwanja vya People’s Club mjini Singida.
DSC_0232
Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Abdulrahman Kinana , sambamba na Katibu wa Itikadi na  Uenezi Nape Nnauye,wakiwasili kwenye viwanja vya People’s Club kwenye mkutano wa hadhara kwa staili ya aina yake kwa kutumia usafiri wa Bajaji.
DSC_0848
Katibu mkuu wa CCM , Kinana, (kwanza kulia),akifurahia ujumbe ulioandikwa kwenye bango la wajasiriamali waliohudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Peoples klabu mjini Singida.
DSC_0855
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,(wa kwanza kushoto) akishiriki kutoa burudani kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya katibu mkuu CCM taifa,Abrahamani Kinana,kuzungumza na wakazi wa jimbo la Singida mjini.
DSC_0858
Naibu waziri wa fedha Adamu Malima,(wa kwanza kushoto) akifurahia jambo na mbunge wa jimbo la Singida mjini juzi kwenye hafla ya mbunge Dewji kukabidhi msaada mabati na mifuko yenye thamani ya  zaidi ya shilingi 125 milioni.

DEWJI (MO) AMWAGA MSAADA WA ZAIDI YA MILIONI 127 KWENYE TAASISI ZA DINI ZAIDI YA 80 JIMBONI KWAKE

DSC_0025
Mbunge wa Singida Mjini, Mh. Mohammed Dewji (MO), akizungumza na viongozi wa Mahakama ya Qadhi wakati alipotembelea Mahakama hiyo kuona namna inavyohudumia waumini wa Dini ya Kiislamu katika kutatua migogoro ya ndoa.
DSC_0029
Sheikh wa Mahakama ya Qadhi, Ramadhani Kaoja akimweleza Mheshimiwa Mbunge shughuli za Mahakama hiyo pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili, Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Singida Mjini , Hamis Nguli, wa pili kulia ni Katibu wa Mahakama ya Qadhi, Alhajj B. Mlau.
DSC_0133
Mbunge wa jimbo la Singida Mjini MO akisalimiana na waumini wa Msikiti wa Kata ya Mtipa wakati alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa Msikiti huo, ambapo mara baada ya kuona hatua zilizofikia za ujenzi huo aliahidi kutoa  Mabati 50 pamoja na mifuko 50 ya Saraji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo.
DSC_0171
MO akitoka kukagua ujenzi wa Msikiti wa kijiji cha Mangwanjuki kata ya Mtipa.

Jumapili, 25 Mei 2014

DR. MWANJELWA AMTEMBELEA HOSPITALI VICKY KAMATA

Mhe Dkt. Mary Mwanjelwa alipokwenda kumfariji Mbunge mwenzie leo Mhe Vicky Kamata ambaye amelazwa Tabata Hospital  baada ya kuugua ghafla

MWENGE WA UHURU 2014 WAMALIZA MBIO ZAKE MKOANI RUKWA, WAMMULIKA MLEMAVU WA NGOZI (ALBINO) ALIYEKATWA MKONO MWAKA JANA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (katikati) akishiriki mbio za Mwenge wa Uhuru (2014) na viongozi wa mbio hizo kitaifa, viongozi na wafanyakazi wa Serikali, vyama vya siasa Mkoani Rukwa na wananchi muda mfupi kabla ya kukabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro baada ya Mwenge huo kukamilisha mbio zake Mkoani Rukwa leo tarehe 25-05-2014. Mwenge huo wa Uhuru mkoani Rukwa ulitembelea miradi ya maendeleo 28 na vikundi 27 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni nne (4). 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro Mwenge wa Uhuru baada ya kumaliza mbio zake Mkoani Rukwa leo tarehe 25-05-2014. Mwenge huo wa Uhuru mkoani Rukwa ulitembelea miradi ya maendeleo 28 na vikundi 27 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni nne (4). 
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru (2014) kitaifa Ndugu Wito Mlemelwa (katikati) kwa niaba ya Kiongozi wa wakimbiza Mwenge kitaifa (2014) Ndugu Rachel Kassanda akimkabidhi mlemavu wa ngozi Bi. Maria Chambanenge mkazi wa Sumbawanga msaada wa ng'ombe wawili wa kulimia aina ya Maksai (hawapo pichani) na jembe la kulimia wanyama (Plau) jana tarehe 24-05-2014 vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni 2.3 kama msaada wa kujikimu kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kutokana na mama huyo kukatwa mkono wake wa kushoto kwa imani za kishirikina mwishoni mwa mwaka jana. Kushoto anayeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Methew Sedoyyeka.
Ng'ombe wawili wa kulimia aina ya Maksai waliotolewa msaada kwa Mama Maria Chambanenge.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru (2014) kitaifa Ndugu Wito Mlemelwa (katikati) kwa niaba ya Kiongozi wa wakimbiza Mwenge kitaifa (2014) Ndugu Rachel Kassanda akimkabidhi mlemavu wa ngozi Bi. Maria Chambanenge mkazi wa Sumbawanga msaada wa jembe la kulimia wanyama (Plau) na ng'ombe wawili wa kulimia aina ya Maksai (hawapo pichani) jana tarehe 24-05-2014 vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni 2.3 kama msaada wa kujikimu kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kutokana na mama huyo kukatwa mkono wake wa kushoto kwa imani za kishirikina mwishoni mwa mwaka jana. 
Mlemavu wa ngozi Bi. Maria Chambanenge mkazi wa Sumbawanga ambaye alisababishiwa ulemavu mwingine wa viungo mwaka jana 2013 na watu wasiojulikana baada ya kukatwa mkono wake wa kushoto kwa imani za kishirikina akishika Mwenge wa Uhuru jana tarehe 24-05-2014 ulipotembelea kijijini kwao kuzindua mradi wa maji na kumkabidhi msaada wa ng'ombe wawili wa kulimia aina ya Maksai (hawapo pichani) na jembe la kulimia wanyama (Plau) vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni 2.3 kama msaada wa kujikimu kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa mama huyo. 
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)

Ijumaa, 23 Mei 2014

DR.MWANJELWA ASAIDIA WAATHIRIKA MAFURIKO KYELA

Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akimkabidhi mashuka Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Magreth Malenga na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Clemens Kasongo, kabla ya kwenda kuwakabidhi wananchi walioathirika na mafuriko mwaka huu 2014.

Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akiwasalimu wanawake na kuwapa pole katika Kijiji cha Nyerere wilayani Kyela mkoani Mbeya.

Pokea mkono wa Baraka.....
 
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akivuka daraja la mianzi katika Kijiji cha Mpunguti.


MBALI na Mbunge wa Jimbo la Kyela mkoani Mbeya, Dr, Harrison Mwakyembe, kutoa misaada kwa waathirika wa mafuriko Jimboni humo,  Mbunge wa viti maalum (CCM), Mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, naye amejitokeza na kutoa misaada ya kiutu kwa wananchi wa wilaya hiyo.


Akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara wa Kijiji cha Nyerere, Dr. Mary Mwanjelwa, alisema mbali na kwamba mafuriko hayo yameathiri kaya nyingi, lakini ana uhakika kuwa wanawake na watoto ndiyo walioathirika zaidi.

“Maandiko yanasema lieni na wanaolia, najua wakati mafuriko yanatokea wengine yamewakuta wakiwa wajawazito, ninyi siyo wakiwa, tupo pamoja, nilipopata taarifa hii sikuweza kukaa na amani pale Bungeni, nimeacha posho na kuja kuwapa pole ndugu zangu’’ alisema Dr.Mwanjelwa huku akipiga magoti.


Diwani wa kata ya Bujonde, Paul Mwambafula, alisema Kata yake ndiyo kata iliyoathirika zaidi katika wilaya hiyo ambapo kaya 2,400 zilikumbwa na mafuriko hayo, lakini kaya 1800, ziliathirika zaidi.

Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania(UWT), Pricila Mbwaga na Katibu wa UWT Mkoa wa Mbeya, Mariam Yusuph, waliwaambia wananchi wa Kijiji cha Nyerere na Mpunguti kuwa, tatizo hilo siyo la kwao peke yao, maana dunia imelisikia.

Mkuu wa wilaya ya Kyela, Magreth Malenga na Afisa tarafa ya Unyakyusa, Kheri William, walimshukuru Mbunge, Dr. Mwanjelwa kuwa mstari wa mbele kujitoa kusaidia wenye uhitaji na kwamba kamati ya maafa ya wilaya hiyo, itamalizia kusaidia kaya zilizoathirika katika Kijiji cha Nyerere.

Dr. Mwanjelwa alitoa mashuka 150 katika Vijiji vya Nyerere na Mpunguti na kutoa wito kwa taasisi na watu binafsi kujitokeza kuwasaidia wananchi wa wilaya hiyo walioathirika na mafuriko hayo.

Baadhi ya mashuka yalitolewa na benki ya NMB baada ya Mbunge huyo kuiomba taasisi hiyo ya kifedha, ambayo mbali na mashuka, ilimkabidhi madawati 83 kwa ajili ya shule za Msingi.

“Benki ya NMB inatoa huduma zake katika jamii ya watu mbalimbali. Wanafunzi, watoto, watu wazima, wazee, mashirika na makampuni na wateja mbalimbali. Sis kwetu hawa wote ni wadau ambao ndio wanafanya NMB iendelee kuwepo’’ alisema Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za juu kusini, Lucresia Makiriye.

Akishukuru kwa niaba ya wananchi wenzake wa Kijiji cha Mpunguti, Mzee Water Butungulu, alienda mbali na kumweleza Dr. Mwanjelwa kuwa endapo atawania nafasi ya Ubunge mwakani, atashinda kutokana  na juhudi zake za kuhudumia jamii.

FEDHA ZA UKIMWI ZITUMIKE KWA UFANISI KUOKOA MAISHA YA WATU

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyotolewa hivi karibuni imebainisha kuwepo kwa kiasi kikubwa cha fedha za miradi ya UKIMWI ambazo hazikutumika kwa mwaka wa fedha 2013/14. Jumla ya Halmashauri 58 zimeshindwa kutumia kiasi cha shilingi bilioni 2.3 za Tanzania.

Kiasi kingine cha fedha za VVU na UKIMWI ambacho hakikutumika ni shilingi milioni 624.49 za Mradi wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP),  shilingi milion 307.2 za Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) pamoja na   milioni 428.49 za Tanzania zilizotengwa kwa TAMISEMI. Inasikitisha kuona kwamba kiasi hiki kikubwa cha fedha hakikutumika wakati utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI ukikabiliwa na changamoto nyingi. Kama CAG alivyoainisha, hali hii inasababisha kutokukamilika ama kutokutekelezwa kabisa kwa shughuli zilizopangwa.

Baadhi ya sababu za kutotumika kwa kiasi hicho cha fedha zilitajwa na CAG kuwa ni ucheleweshwaji wa fedha kutoka Hazina na urasimu katika matumizi ya fedha za miradi kwenye halmashauri. Inahuzunisha kwamba haya yanatokea wakati bado kuna uhitaji mkubwa wa huduma za VVU na UKIMWI katika jamii.

Mapema mwaka huu, vyombo vya habari viliripoti kuwepo kwa uhaba mkubwa wa dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs) hususani katika mikoa ya Dar es salaam, Kilimanjaro and Mara. Sikika pia ilibaini upungufu wa dawa hususan Combivir na Septrin katika baadhi ya vituo wilayani Iramba, huku  mkoa wa Manyara ukiripotiwa kuwa na tatizo kubwa la ucheleweshwaji wa usambazaji wa dawa kutoka MSD. Katika mkoa wa Dar es Salaam, baadhi ya Watu wanaoishi na VVU (WAVIU) waliripoti kubadilishiwa dawa bila kupewa maelezo na wahudumu wa afya. Wakati huohuo, baadhi ya watoa huduma katika wilaya ya Ilala walieleza kuwa iliwalazimu kutoa dawa za mwezi mmoja kwa wagonjwa badala ya miezi miwili kama ilivyozoeleka kutokana na upungufu wa dawa hizo katika vituo vyao.

Utafiti juu ya Maoni ya watumia huduma za VVU na UKIMWI uliochapishwa na Sikika mwaka 2013, ulionesha kuwa upungufu wa upatikanaji wa huduma za VVU na UKIMWI una athari za moja kwa moja kwa WAVIU.  Athari hizo ni pamoja na gharama kubwa za usafiri kufuata huduma za afya, kukosa usiri wakati wa kutoa ushauri nasaha kutokana na uhaba wa vyumba katika vituo vya huduma, kutokuwepo kwa huduma endelevu za vipimo vya CD4 na wagonjwa kutozingatia matibabu kunakochangiwa na uhaba wa dawa za ARVs.

Mkakati wa Tatu wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (NMSF III) umetaja sababu za upatikanaji wa huduma duni za VVU na UKIMWI kuwa ni uhaba na kutokuwa na uhakika wa fedha; umbali wa kufikia vituo vya huduma hususan vijijini, hali inayochangia WAVIU kutohudhuria kliniki. Huduma tembezi zimeanzishwa ili kupunguza tatizo la umbali wa kufika vituoni. Hata hivyo, uhaba wa rasilimali unakwamisha utolewaji wa huduma hii.  Upungufu wa ARVs na huduma za mashine za CD4 na  miundombinu duni, kwa pamoja vinaathiri matunzo, matibabu na misaada kwa WAVIU.  Swali la kujiuliza ni: Kama nchi imeweka mkakati wa kuwezesha upatikanaji wa huduma bora za viwango vya juu kama ilivyoainishwa katika NMSF III; na kama bado sekta inakabiliwa na changamoto nyingi, kwanini basi kiasi hicho kikubwa cha fedha hakikutumika?

Wadau wa maendeleo wanachangia kiasi kikubwa cha rasilimali ili kusaidia utekelezaji wa shughuli za VVU na UKIMWI nchini. Kwa mujibu wa NMSF III, sekta ya VVU na UKIMWI ni moja kati ya sekta zenye utegemezi mkubwa wa fedha za wafadhili, takribani 97%. Kwa vile mchango wa serikali katika huduma za VVU na UKIMWI ni mdogo; ufanisi kwenye matumizi na usimamizi wa fedha hauna budi kupewa kipaumbele.  Serikali inatakiwa ioneshe wananchi, mamlaka za serikali za mitaa pamoja na wadau wa maendeleo ni kwa jinsi gani rasilimali chache zilizopo zimetumika kwa ufanisi.

Tunatoa wito kwa Hazina kuhakikisha fedha zinatolewa kwa wakati ili kuwezesha utekelezaji wa shughuli zilizopangwa. Mamlaka za serikali za mitaa zitekeleze shughuli kulingana na mipango na bajeti bila kuchelewa na TAMISEMI isimamie utekelezaji wa shughuli hizo ngazi ya halmashauri. Hii itapunguza ama kumaliza tatizo la bakaa ya kiasi kikubwa cha fedha mwishoni mwa mwaka. Kushindwa kutumia fedha za miradi ambazo asilimia kubwa zimetolewa na wafadhili,  tena kwa miaka mitatu mfululizo si jambo la kufumbiwa macho; ni lazima hatua za haraka zichukuliwe na watendaji wasiowajibika ni wawajibishwe.

Mr. Irenei Kiria, Mkurugenzi wa Sikika, S.L.P 12183 Dar es Salaam,
Simu: +255 222 666355/57, Nukushi: 2668015, Barua pepe: info@sikika.or.tz,
Twitter: @sikika1, Facebook: Sikika Tanzania, Tovuti: www.sikika.or.tz

TFDA YAHAMASISHA WAHARIRI NA WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI KUHUSU USIMAMIZI WA SHERIA YA CHAKULA, DAWA NA VIPODOZI YA MWAKA 2003 JIJINI MBEYA

Wakongwe Peti Siyame wa Sumbawanga na Frank Leonard wa Iringa

Mmoja wa wawezeshaji wa TFDA,  Chary Ugullum ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA na Mkurugenzi wa Huduma za Maabara wa taasisi hiyo
wanahabari kutoka mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa
Usikivu ulikuwepo


Walikuwepo walioona umuhimu wa kuchukua kilichokuwa kikiwasilishwa

Alhamisi, 22 Mei 2014

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA MBEYA DR. MARY MWANJELWA, ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KYELA, AKABIDHWA MASHUKA NA MADAWATI NA NMB

Kulia ni Meneja wa benki ya NMB Kanda ya nyanda za juu kusini LUCRESIA MAKIRIYE, akimkabidhi mashuka Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa Jijini Mbeya.


 Meneja wa benki ya NMB Kanda ya nyanda za juu kusini LUCRESIA MAKIRIYE, akizungumza na waandishi wa habari.
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa Jijini Mbeya leo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa mashuka na madawati ya shule za msingi, alivyoomba katika benki ya NMB.

  Meneja wa benki ya NMB Kanda ya nyanda za juu kusini LUCRESIA MAKIRIYE, akizungumza na waandishi wa habari.
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akipokelewa wilayani Kyela mkoani Mbeya leo.
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akiwa Ofisini kwa mkuu wa wilaya ya Kyela.

 Kamati ya maafa wilaya ya Kyela.





 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akiwasalimu wanawake na kuwapa pole katika Kijiji cha Nyerere wilayani Kyela mkoani Mbeya.





 Usafiri huo......madaraja yameharibika....
 Katibu wa UWT Mkoa wa Mbeya, Mariam. Akivuka daraja Mpunguti wilayani Kyela mkoani Mbeya.

 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akivuka daraja.
 Mjumbe wa kamati tendaji ya UWT Mbeya, Prisca Mahundi, akivuka daraja katika Kijiji cha Mpunguti, wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.


 Mchele wa Kyela......
 Tunatwanga Mchele wa Kyela hapa......
 Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akipiga magoti na kuwapa pole waathirika wa mafuriko wilayani Kyela mkoani Mbeya leo.


NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...