Jumatatu, 2 Desemba 2013

MAKAMBA AZUNGUMZIA SUALA LA KUGOMBEA URAIS 2015

blog post image
 
*Asema anakerwa na matumizi ya fedha kutafuta uongozi
*************************************************************************
NAIBU waziri wa Wizara ya Mawasiliano sayansi na teknolojia, January Makamba,  ambaye pia ni Munge wa Jimbo la Bumbuli, ametumia dakika 17 kueleza kwanini anaweza kuwania nafasi ya Urais mwaka 2015 kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Alitumia muda huo baada ya mmoja wa waadhiri wa vyuo na vyuo vikuu mkoani Mbeya kutaka kujua uhalisia wa uvumi kuwa yeye ni miongozi mwa vijana wa CCM ambao wanatajwa kuwa watawania nafasi hiyo.

Makamba alisema kuwa, makundi ya watu wa rika mbalimbali wameendelea kumshawishi kuwania nafasi hiyo mwaka 2015 na kumtaka atafakari na kuchukua hatua.

Alisema kuwania nafasi hiyo ni jambo kubwa sana hasa wakati huu ambao yeye anakerwa na matumizi ya fedha yenye lengo la kupata uongozi.

‘’Nakerwa sana na matumizi ya fedha kutafuta uongozi jambo ambalo linawanyima fursa watu wenye vipawa vya uongozi kutuongoza, mimi sina hela, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda watu wanazidi kunifuata’’alisema Makamba.

Alisema kabla hajachukua hatua ya kutamka kuwa atagombea, anaendelea kutafakari kama kazi yenyewe ataiweza au la kwasababu kazi ya kuwa Rais si kazi yeye na familia yake bali ni ya kuwatumikia watanzania.

‘’Natafakari kuwa je! Ninaweza kuungwa mkono na watu wote Tanzania? Isije ikawa ni kikundi cha ndugu au marafiki pekee ndiyo wanakuunga mkono, Urais siyo wa Bumbuli tu’’ alisema Makamba.

Aliongeza kuwa tafakuri yake ni kwamba akijiridhisha kuwa atapata wapi fedha za kuendeshea nchi katika utawala bora, elimu na mambo mengine, atatamka rasmi kuwa anagombea nafasi hiyo kubwa na ya heshima.

‘’Ni rahisi kusema kuwa unataka kugombea, lakini ni lazima ujiulize maswali kadhaa yakiwemo kuwa je unaweza kuwaridhisha watanzania kimwili, kiakiri, kifikra na kuwa na fikra za kubadili nchi kuwa kwanini tumeshindwa mahala fulani na tunawezaje kuziba mapengo hayo. Hivyo mimi bado natafakari’’ alisema Naibu Waziri huyo.

Katika kongamano hilo lililolenga kuwakaribisha wanafunzi ambao ni wanaCCM wa mwaka wa kwanza katika vyuo hivyo, Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa alitoa mada ya asilimia hamsini kwa hamsini ya uogozi kwa wanawake.

Alisema ili kufikia kiwango hicho cha Hamsini kwa hamsini, ni lazima wanawake waache kuchukiana na jamii iwape nafasi wanawake katika nafasi za kiungozi.

‘’Wanawake ndiyo wapiga kura wakubwa na Tanzania takwimu zinaonesha kuwa wanawake ni asilimia 52, lakini wanawake tuna tatizo la kutoungana mkono na kuchukiana’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Dr. Norman Sigalla, alitoa mada ya ukosefu wa ajira kwa wasomi ambapo alisema kuwa wasomi wengi hawafanikiwi kwasababu wanachagua kazi za kufanya.

‘’Hakuna serikali yeyote duniani ambayo inaajiri wasomi wake wote, na ukiangalia wafanyabiashara wakubwa zaidi ya asilimia 86 hawana elimu ya kidato cha sita ama shahada’’ alisema Dr. Sigalla.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...