Jumapili, 19 Januari 2014

DR. MWANJELWA SIKU ALIPOWAPONGEZA NA KUTOA MSAADA KWA WAISLAM MBEYA

 Dr. Mary Mwanjelwa, akimkabidhi Imamu Mkuu wa msikiti huo, Iliyasa Mchalikwao, mifuko 60 yenye saruji ndani ya gari.
 Sasa kumekucha......sasa kumekucha...
*****************************************************************************************************8


WAISLAM wa msikiti wa Almasjid Tawfiq,  Soweto Jijini Mbeya, wamepongezwa kwa ubunifu wa maendeleo na kuwa na nia ya dhati ya kuleta amani na mshikamano nchini.


Pogezi hizo zimetolewa Juzi na Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(CCM), alipokuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchagia ujenzi wa msikiti wa kisasa unaotarajiwa kujengwa eneo hilo la Soweto. 
 
Dr. Mwanjelwa alisema, Misikiti na makanisa ni maeneo ya kiimani pia ni maeneo ya kutengeneza maadili na kuiweka jamii kuwa salama.

‘’Kiongozi mzuri ni yule mwenye maadili, asiyejali itikadi za kiimani, bali kuhudumia jamii, mimi ni kiongozi wa wote sibagui kabila, dini wala tabaka lolote, moyo wangu ni wa kusaidia jamii’’ alisema Dr. Mwanjelwa.

Alisema kuna baadhi ya wananchi na makundi yenye nia nzuri ya kimaendeleo, wanawachukia baadhi ya viongozi hata bila kuwashirikisha, jambo ambalo alisema jamii inapaswa kuondokana nalo na aliomba yeye ashirikishwe kwa kila jambo la kimaendeleo kwasababu yeye ni mwanamaendeleo na si ‘’longolongo’’.

Katika harambee hiyo, Mbunge huyo alitoa mifuko 60 ya saruji yenye thamani ya Shilingi Milioni moja na Laki Nne, ambayo aliikabidhi papo hapo ikiwa kwenye gari aina ya Canter  T 441 BRL, na kuahidi kuwatafutia viongozi wengine wa kuchangia ujenzi wa msikiti huo wa kisasa.

Imamu mkuu wa msikiti huo, Ilyasa Mchalikwao, alimshukuru Mbunge huyo kwa ajili ya moyo wake wa kukubali kuchangia msikiti huo bila kujali itikadi ya kidini na kwamba huo ndiyo uongozi.

Awali akisoma risala ya Msikiti,  Katibu wa Maendeleo ya Msikiti huo wa Almasjid Tawfiq, Juma Ramadhani, alisema wanatarajia kujenga msikiti wa kisasa wenye ghorofa tatu ambao utajengwa kwa awamu nne na kugharimu zaidi ya Shilingi Milioni 700.

Alisema lengo la ujenzi wa msikiti huo wa kisasa ni maendeleo na kwamba msikiti huo ukikamilika, utakuwa ni wa mfano katika mkoa wa Mbeya na Dr. Mwanjelwa tayari ameingizwa kwenye historia ya msikiti huo kwa kuwa ni kiongozi wa kwanza kuchangia.

‘’Tayari tumekusanya Shilingi Milioni 34, na tumeshauriwa kuacha kusambaza majengo ardhini, tuna imani nawe kwasababu unaweza na ni makini sana tena sana na tunakutegemea kututafutia wafadhili kwasababu unao marafiki ndani na nje ya nchi’’ alisema Juma Ramadhani.

Alisema historia na maisha ya Mwanadamu vinaenda sawa, hivyo wanamtakia kheri katika kazi zake za kisiasa na kutumikia wananchi na kwamba mbali na yeye pia Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Aesh Hilary(CCM), alituma Sh. 1.5 Milioni kwa ajili ya kumwongezea nguvu ya harambee Dr, Mwanjelwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...