Jumatano, 29 Januari 2014

DR.MARY MANJELWA ATEMBELEA KAMBI LA VIJANA WA HALAIKI CHIMALA MBEYA NA KUWAPONGEZA

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(kushoto), akiwa na katibu wa Jumuiya ya wazazi katika shule ya sekondari Chimala, ambapo limewekwa kambi la vijana wa Halaiki kwa ajili ya maazimisho ya miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), yatakayofanyika Februari 2, mwak huu mkoani Mbeya.
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akizungumza na viongozi wa umoja wa vijana (UVCCM) Mkoani Mbeya.

 Vijana wa halaiki, wakifanya mazoezi yao katika uwanja wa shule ya sekondari Chimala, wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
 Vijana wa halaiki, wakichora maumbo mbalimbali kwa kutumia miili yao.....ubunifu....
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa(kushoto), akizungumza na mwalimu wa halaiki hiyo uwanjani hapo, katikati ni katibu wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, Mr. Yassin.
 Sarakasi....


 CCM HOYEEEE.....Akapusipusi, akanyaunyau....
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, akizungumza na vijana wa halaiki uwanja wa Chima;la Sekondari.
 Vijana wa halaiki wakiwa wamembeba juu Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Mbeya, Amani Kajuna.
 Wakimbeba mmoja wa matron wao....




MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, amewatembelea vijana walioko kambini katika shule ya Sekondari ya Chimala wilayani Mbarali mkoani Mbeya na kuwapa moyo na kuwachangia Mchele nusu gunia, viazi viroba viwili na mahitaji muhimu kwa kutoa Tsh. 200,000.

Dr. Mwanjelwa amewaambia vijana hao kuwa mbalina halaiki hiyo, wao ni chachu kubwa kwa chama na chama kitawathamini kwa kuzingatia msemo wa mchumia juani, kivulini.

Sherehe za miaka hiyo 37 za Chama Cha Mapinduzi(CCM), zinatarajia kufanyika Jijini Mbeya na mgeni rasmi atakuwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...