Jumatatu, 27 Januari 2014

SUGU AWATUHUMU MAAFISA USALAMA KUTOA SIRI ZA SERIKALI


 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa (N i kama anamuonya kitu) Mbunge wa Jmbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi(SUGU).

..........................................................................................................

MBUNGE wa Jimbo la Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi(sugu), amesema kuwa chama chake cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), kinapata taarifa za serikali kutoka kwa baadhi ya maafisa usalama wa taifa.

Hayo aliyasema Januari 25, mwaka huu, katika mkutano wa hadhara wa chama hicho, uliofanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya.

Alilazimika kutoa siri hiyo alipokuwa akizungumza kuwa amepata taarifa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), kupeleka vijana 300 kambini katika shule ya sekondari Chimala wilayani Mbarali mkoani hapa, kwa ajili ya mafunzo ya kuvuruga mikutano ya Chadema.

‘’Chama cha magamba kimepasuka na ndiyo maana tunapata siri zote, na popote palipo na maafisa usalama zaidi ya watatu mmoja wao ni wa Chadema na walipo maafisa watatu au wanne wa Polisi, wawili ni wetu’’ alisema Mbilinyi huku akishangiliwa na wafuasi wake.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dr,Wilbroad Slaa, alisema kutokana na taarifa hiyo anaagiza kukutana na vijana wake wa kikosi cha Red Briged kwa ajili ya kukabiliana na vijana hao wa CCM.

Mbali na hilo, alisema wamepata taarifa kuwa serikali inataka kutumia jopo la waganga wa kienyeji kuwashughulikia wapinzani lakini yeye hawatamuweza kwasababu yeye pia ni Mganga wa jadi na kwao Karatu wanamfahamu alipokuwa Fratee katika kanisa Katoliki.

Aidha, aliweka wazi kuwa pamoja na mambo mengine, hakupendezwa na suala la kuona jeneza ambalo lilitengenezwa na chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini na kuandika buriani Zitto Kabwe, kwasababu ishara hiyo siyo nzuri kwa mtu aliye hai.

Kutokana na tamko la viongozi hao, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), Mkoa wa Mbeya, ulilazimika kuitisha waandishi wa habari na kukanusha jambo hilo.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, Aman Kajuna, alisema kuwa chama hicho kimepeleka vijana wasiozidi 280 katika kambi lenye lengo la mafunzo ya haraiki kwa ajili ya sherehe za miaka 37 ya CCM zitakazofanyika Jijini Mbeya kitaifa.

Hata hivyo, baadhi ya waandishi wa habari mkoani Mbeya, walitembelea kambi hilo baada ya mkutano wa Chadema uliofanyika karibu na shule ya Chimala kuisha na kukuta vijana hao wakifanya mazoezi ya kuumba maumbo yanayoashiria sherehe hizo sambamba na kuimba nyimbo za chama chao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...