Jumatatu, 24 Novemba 2014

NI CCM NA CHADEMA SERIKALI ZA MITAA MBALIZI




VYAMA viwili pekee, ndivyo vimethibitisha na kurejesha fomu za kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbalizi, Mbeya Vijijini,mkoani hapa, ili kuunda mji mdogo wa Mbalizi.


 
Msimamizi wa uchaguzi wa eneo hilo, ambaye ni afisa mtendaji wa Kijiji cha Mbalizi, Malongo Sumuni, alivitaja vyama hivyo kuwa ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha demokrasia na Maendeleo(Chadema).

Aliwataja wagombea wa nafasi hiyo kuwa ni Asifiwe Godwin  Mwakalonge(CCM), na Elia Wilson  Mkono(Chadema), ambaye ni Mwenyekiti wa Kijiji hicho na ni diwani wa kata ya Utengule Usongwe kupitia Chadema.

“Mbali na kurejesha fomu na kuteuliwa kuwania nafasi hiyo, hawaruhusiwi kufanya kampeni mpaka zitakaporuhusiwa tarehe 30/11/2014 na mwisho itakuwa Desemba 13, mwaka huu” alisema msimamizi huyo.

Alipoulizwa idadi ya wakazi wa eneo hilo, alisema kuwa takwimu alizonazo zinaonesha wakazi 13,690, takwimu ambazo amesema siyo halisi.”Tuna vitongozji vitano ambavyo ni Mlimareli yenye kaya 2900 wakazi 3700, Chapa Kazi kaya 1800 wakazi 3200, DDC kaya 1534 wakazi 2320, Pipeline kaya 1250 wakazi 1650 na Mtakuja kaya 1650 chenye wakazi 3200” alisema Sumuni.

Uchunguzi umebaini kuwa, ofisi yake ilipelekewa idadi ndogo ya wakazi kwa kile wenyeviti wa vitongozi walichokuwa wakihofia katika ukusanyaji wa michango, kuwa endapo wakazi wachache wangechagia, wangesumbuliwa wao kufuatilia.

Mji huo wa Mbalizi, ndiyo kitovu cha siasa za Jimbo la Mbeya Vijijini, ambapo vyama vine vya siasa vimekuwa vikichuana vikiwemo Chama cha wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi, CCM na Chadema.

Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameendelea kujiandikisha kwa ajili ya upigaji kura wa viongozi wa serikali za mitaa ifikapo Desemba 14, mwaka huu, huku kila kituo kikiwa na mawakala wa vyama vya siasa, hususani CCM na Chadema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...