Ijumaa, 27 Juni 2014

VIONGOZI WA SERIKALI MBEYA WAKUTANA KUJADILI UBORESHAJI WA BIMA YA AFYA YA JAMII




 Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa, Charles Kajege, akizungumza neno mbele ya viongozi waliokuwa wamehudhuria, wakiwemo wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Mbeya.
 Baadhi ya wenyeviti wa Halmashauri za mkoa wa Mbeya, wakisikiliza.
 Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa, Charles Kajege.
 Wakuu wa wilaya za Ileje na Kyela mkoani Mbeya, wakisikiliza na kufurahia...
 Mkuu wa wilaya ya Rungwe, akifurahia jambo baada ya kutaniwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, ambaye aliuwa mgeni rasmi.
 Wakuu wa wilaya za Mbarali na Mbozi.
 Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Dr. Norman Sigalla.
 Picha ya pamoja kati ya viongozi wa Bima ya Afya, Mkuu wa mkoa wa Mbeya na wakuu wa wilaya za Mbeya. Kisha zikafuata picha zingine za pamoja.



 Meneja wa NHIF Mkoa wa Mbeya, Dr. Mohamed Kilolile(kushoto), wakiwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro baada ya kufungua mkutano huo.
 Baadhi ya waganga wakuu wa Hospitali za wilaya za mkoa wa Mbeya.
 Meneja Matekelezo wa NHIF makao makuu, Grace Lobulu, ambaye alimwakilisha Naibu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, akitoa mada.
 Afisa wa NHIF Mbeya.
  Meneja wa NHIF Mkoa wa Mbeya, Dr. Mohamed Kilolile, akizungumza jambo katika mkutano wa CHF kwa viongozi wa mkoa wa Mbeya wakiwemo Wakuu wa wilaya za Mbeya, Wakurugenzi, waganga wakuu, Wenyeviti wa Halmashauri na wenyeviti wa bodi za afya za halmashauri, ulioandaliwa na Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa,  (NHIF).
 
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, akifungua mkutano wa CHF kwa viongozi wa mkoa wa Mbeya wakiwemo Wakuu wa wilaya za Mbeya, Wakurugenzi, waganga wakuu, Wenyeviti wa Halmashauri na wenyeviti wa bodi za afya za halmashauri, ulioandaliwa na Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa,  (NHIF).
Mkutano wa CHF kwa viongozi wa mkoa wa Mbeya wakiwemo Wakuu wa wilaya za Mbeya, Wakurugenzi, waganga wakuu, Wenyeviti wa Halmashauri na wenyeviti wa bodi za afya za halmashauri, umefanyika jana katika hospitali ya mkoa wa Mbeya, kwa maandalizi ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa,  (NHIF).
Imebainika kuwa, mfuko wa KfW, alisema ni mradi mzuri ambao unalenga kupunguza vifo vya mama na mtoto ili kutekeleza malengo ya milenia kufikia mwaka 2015 na kwamba tayari kwa mkoa wa Mbeya, wanawake 70,000 wamejiunga.
Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa, Charles Kajege, alisema lengo la mkutano huo na viongozi hao, ni kuhakikisha viongozi hasa wakuu wa wilaya kupanga mipango ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma zkiwemo dawa kwa wanachama wa CHF.
“Fedha zipo nyingi kwenye mfuko wetu kwa ajili ya dawa na vifaa tiba, leteni maombi ya mahitaji, tutawapeni ili wananchi wapate huduma’’ alisema Kajege.
Meneja Matekelezo wa NHIF makao makuu, Grace Lobulu, ambaye alimwakilisha Naibu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, alisema kuwa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), ulianza rasmi jukumu la kusimamia mfuko wa Afya ya Jamii(CHF), Kitaifa mwezi Julai 2009.
Meneja wa NHIF Mkoa wa Mbeya, Dr. Mohamed Kilolile, alizitaja sababu za kuanzishwa kwa CHF kuwa ni Kushirikisha jamii kutoa mawazo yao ili kuboresha huduma za afya kupitia mikutano na kamati mbalimbali watakazozichagua wao wenyewe.
“Kuiwezesha jamii kumiliki hudum za Afya zinazowahusu katika maeneo wanayoishi na kuboresha huduma za matibabu kupitia utaratibu rahisi na nafuu wa uchangiaji kwenye mifuko ya bima ya jamii’’ alisema Dr. Kilolile.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...