Jumatatu, 30 Juni 2014

KANDORO AKANA SERIKALI KUTOZA USHURU ''VITENDANISHI'' VYA DAWA ZA KULEYA

 Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, akijibu maswali ya waandishi wa habari, kabla ya kuazimishwa kwa siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani mwaka huu 2014.
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro akisoma taarifa ya ujio wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Mohamed Bilal, mkoani Mbeya, ambapo alikuwa mgeni rasmi katika kilele cha siku ya kupiga vita dawa za kulevya.
  Baadhi ya waandishi wa habari waliokuwepo ofisini kwa mkuu wa mkoa wa Mbeya siku hiyo.
 
MKUU wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amekana serikali kutoza ushuru vitendanishi vya dawa za kulevya hapa nchini.

Kandoro alisema serikali haihusiki kutoza ushuru vitu vinavyotumika kuvutia dawa za kulevya, bali watumiaji wanageuza matumizi sahihi ya vitendanishi hivyo.

Jibu hilo alilitoa ofisini kwake Juni 24, mwaka huu, alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari ambao waliuliza kuwa karatasi aina ya Rizila, ambazo kwa sasa zinatumika kusokotea bangi, serikali inachukua ushuru, hivyo je serikali haioni kuwa inachochea matumizi ya bangi?

Kabla hajajibu swali hilo, alilirejesha swali hilo kwa waandishi hao kama wanajua lengo la karatasi hizo ambazo zinatozwa ushuru. 

Baadhi walijibu kuwa karatasi hizo zimetengenezwa kwa ajili ya matumizi ya kusokotea tumbaku.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...