Jumanne, 24 Juni 2014

ASKOFU MWAIJANDE AFARIKI DUNIA. NI WA JIMBO LA MBEYA

ALIYEKUWA  Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship Jimbo la Mbeya, Kingdom Mwaijande,(pichani), amefariki dunia nchini Afrika Kusini alikokwenda kupatiwa matibabu baada ya kuishi na kufanya kazi ya Kuhubiri Injili, kwa zaidi ya miaka saba baada ya kuvamiwa na majambazi.

Mwili wa Askofu huyo, unatarajiwa kufika katika uwanja wa ndege wa Songwe mkoani Mbeya kesho Jumatano Tarehe 25,06,2014 kwa usafiri wa ndege na kwenda kuuhifadhi wilayani Rungwe.

Tunatoa pole kwa kanisa zima la FGBF, wananchi na familia ya askofu Mwaijande.

Mungu alitoa na sasa ametwaa, jina lake libarikiwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...