Alhamisi, 27 Februari 2014

TANZANIA PRISON KUWAWEKA ''RUMANDE'' MGAMBO

 Mashabiki a Mbeya City, wakiipokea kwa shangwe timu yao.

MASHABIKI wa timu ya Tanzania Prison, wamesema kuwa Mgambo kazi yao ni kufundisha mchakamchaka na wala siyo kucheza mpira, hivyo timu ya Mgambo, wajiandae kufungwa katika uga wa Sokoine.



Kocha wa timu ya kukuza vipaji ya Mbeya umoja Sports Academy, ambaye ni shabiki  wa timu ya Tanzania Prison, Peus Nsheka, aliyasema hayo jana ukumbi wa magereza, wakati wa hafla ya mapokezi ya timu hiyo mbele ya mkuu wa magereza mkoa wa Mbeya(RPO), Emmanuel Sanguti.



Wadau hao walikabidhi matunda na juice kwa wachezaji ambapo nahodha wa timu hiyo Lugano Mwangama, alipokea zawadi hizo kwa niaba ya wachezaji wenzake.



Shabiki mwingine, Christopher Nyenyembe, ambaye ni mwandishi wa habari, aliuambia uongozi wa timu hiyo kuwa, hawapaswi kubadilisha walimu kwasababu imeonesha kuwa walimu wazalendo wanao uwezo mkubwa wa kufundisha timu za Tanzania.



“Makocha kutoka nje ya nchi wanakula fedha za timu pasipo sababu yeyote. Fedha hizo zinapaswa kuimarisha timu badala ya kuwapa makocha hao kwasababu makocha wazalendo akiwemo Mwamwaja wanao uwezo mzuri’’ alisema Nyenyembe.



Mkuu wa Magereza mkoa wa Mbeya, aliwapongeza wachezaji, mashabiki, askari na vyombo vya habari kuifikisha timu hiyo hapo ilipo na kwamba mchezo uliooneshwa na timu hiyo kwenye uwanja wa Chamanzi wa Azam Jijini Dar es Salaam, inaonesha timu hiyo inao uwezo wa kufikia nafasi ya tatu bora.



“ Kila mechi iwe fainali, kama ilivyokuwa pale chamanzi, Azam waliomba mechi iishe haraka na hizi timu kubwa zina mambo yao, tulinyimwa penati zaidi ya tatu lakini tuliishusha kutoka kileleni’’ alisema Sanguti.



Mkuu wa gereza la Ruanda, SSP Ismail Misama, aliwaambia wachezaji wa timu hiyo kuwa hawapaswi kubweteka ili kufikia nafasi ya tatu bora na kwamba uwezo na nia kwa pamoja na umoja wa wadau ipo.


Naye mkuu wa chuo ambaye ni mlezi wa timu hiyo, Mashaka Soja na mhamasishaji SP Enock Lupyuto, walisema timu zilizobakiza mechi na timu hiyo zijiandae kisaikolojia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...