Jumanne, 25 Februari 2014

TRA YAWATOA HOFU WAFANYABIASHARA JUU YA EFD



Na Kenneth Ngelesi, Mbeya

MAMLAKA ya mapato nchini TRA imewatoa hofu wafanyabishara kutumia mashine za EFD kwani kodi inakatwa asilimia 30 ya faida baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji na manunuzi.


Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa juma na Afisa Mwandamizi Mkuu wa Elimu wa mamlaka ya Mapato nchini (TRA) makao Makuu Hamis Lepenza katika hotel ya Paridise jiji hapa katika Mkutano na waandishi kutoka vyombo mbalimbali ambao  uliyo itishwa na mamlaka hiyo kwa lengo la kuwataka wandishi wasaidie kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa mashine hizo.


Lupenza alisema kuwa hofu ya wafanyabiashara wengi kuto taka kutumia mashine hizo ni kuto kuwa tayari kukatwa asilimia hiyo ni kwamba wengi hawana elimu ya juu utumiaji wa mashine hizo.


Afisa huyo alisema kuwa wengi wao wamekuwa na malalamiko kuwa hawaja soma hivyo  kuwa nguma kwao kuzitumia miashine hizo jambo alilodai siyo la kweli bali ni janja ya wafanyabishara kwani wana hofia mashine hizo zitasababisha kuonyesha mauzo kuongezeka na kodi ya kulipa kuwa kubwa.


Aliongeza kuwa kutokana makato kuwa wazi katika ulipaji wa kodi ndiyo sabababu wafanyabiashara kutokuwa tayari kutuma mashine hizo.


Lepenzi alisema kuwa wafanyabishara wengi wamekuwa wakilala mika kuwa hawaja soma jambo hivyo uwezo wa kutumia msahine ni mgumu.


'Ndugu zangu huyu mfanyabishara anasema hajasoma hivyo hataweza kutumia mashine hizo lakini mtu huyo huyo unanunua simu nzuri kubwa na yenye mambo mengi kuliko hata hiyo mashine ya EFD' alisema Lupenza.


Aliongeza kuwa tatizo lingine lililopelekea zoezi kuwa gumu ni ugeni wa utamaduni wa kutumia mashine hizo katika jamii yetu na siyo kigezo cha elimu kama kinavyo tolewa na baadhi ya wafanyabishara walio wengi.


Katika hatau nyingine Afisa elimu na huduna ya mlipa kodi kutoka
makao Makao Makuu Sigsimund Kafuru aliwataka waandishi kusaidia kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhumu wa kudai risiti pindi wanapo nunua bidhaa kwani kutochukua risiti ni kuisosesha serikali mapato na hatimaye inashindwa kutoa huduma stahiki kwa wananchi wake.


Aidha Aliongeza kuwa ni vema wananchi wakajenga utamaduni wakudai risiti pindi wanapoa nunua bidhaa  yoyote ile.


Akijibu swali kwa waandishi habari sababu za kuteua makampuni kumi na moja tu kupewa jukuma na kusambaza mashine hizo kutokana na kushinda tenda baada ya kushindanisha kwa mujibu wa sheria ya manunuzi.


Tangu mwaka 2010 serikali kupitia kwa mamlaka ya mapato nchi iliwatka wafanyabisha kutoa risiti  kwa kumtumia mashine hizo kwa sawamu ya kwanza ikianza na wafanyabisha lakini 200,000/ lakini mpka sasa bado kumekuwa na mvutano mkubwa baini ya ya Serikali na wafanya bishara hao.


Hata hivyo  zoezi hilo bado lina leta mvutano mamlaka hiyo imesema kuwa ipo katika mchakato wa kuanza kutoa hudumnu ya risiti kwa kutumia mashine hizo kwenye magari makubwa na mabasi ya kusafirishia abiria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...