Alhamisi, 27 Februari 2014

MAMLAKA YA MAJI MBEYA YAZIDAI TAASISI ZA SERIKALI ZAIDI YA MILIONI 400

 Afisa Habari Mamlaka ya Majisafi na usafi wa mazingira Jijini Mbeya, Neema Stantoni akizungumza na kalulunga blog ofisini kwake.
 Akifafanua jambo....

TAASISI za serikali mkoani Mbeya, zinaongoza kwa kukwepa kulipia huduma za maji, hivyo kukwamisha tija ya uboreshaji wa usambazaji wa maji kwa wananchi mkoani hapa.

Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Jijini Mbeya (MBEYA-UWSA) imesema imekuwa kwenye changamoto kubwa, ingawa taasisi hizo zimekuwa zikipewa fedha na serikali ya kulipia huduma hiyo.

Afisa habari wa Mamlaka hiyo, Neema Stantoni, ameeleza kuwa, taasisi hizo zinadaiwa kiasi cha Tsh. Mil. 466,899,942.

Alisema tayari mamlaka hiyo imeanza zoezi la kuwakatia maji wateja wote ambao wanadaiwa na kwamba wateja zaidi ya Elfu mbili wamekatiwa maji.

‘’Tunahudumia wateja wa aina Nne, wakiwemo wa majumbani, Viwandani, biashara na taasisi za serikali ambapo wateja wanaoongoza kulipa vizuri ni wateja wa viwandani ambao wanalipa kwa wakati’’ alisema Neema.

Kati ya taasisi ambazo zinadaiwa ni pamoja na maeneo ya Afya, Magereza na Polisi ambapo imeelezwa kuwa taasisi hizo zikikatiwa maji kunauwezekano wa kutokea milipuko ya magonjwa kikiwemo kipindupindu.

 Afisa habari huyo amezitaka taasisi za serikali kulipa deni hilo hata kwa kupunguza, vinginevyo zoezi la kukata maji linaweza kuzikumba.

‘’Kwasababu Mamlaka na wateja tunategemeana ambapo mteja akilipa anasaidia matengenezo ya mabomba yanayopasuka, kununua dawa za kutibu maji na kulipia umeme ambao unasaidia kusukuma mashine kisha wateja kupata maji’’ alisema Neema Stantoni.

Alizitaja changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo kwa sasa kuwa ni pamoja na baadhi ya wateja kuiba maji kwa kuchepusha kabla ya mita, kubonda mita kwa lengo la kuiba maji na kutoa mita kisha kuchota maji.

Zoezi la kuwakatia maji wateja wote ambao hawajalipa kuanzia mwezi mmoja, amesema linaendelea nyumba kwa nyumba, wateja wa biashara yakiwemo mahotel kisha taasisi kwa taasisi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...