Jumapili, 9 Februari 2014

NJEZA; AJIRA ILIYOBAKI KWA VIJANA TANZANIA NI KILIMO

  KAMANDA wa UVCCM Mbeya Vijijini, ORAN NJEZA, akihutubia wananchi wa eneo la Jojo, kata ya Santilya, wilaya ya Mbeya, kwenye kampeni za udiwani, ambapo alishangiliwa aliposema kuwa ''Kipele kimempata mkunaji'' akiwa na maana kuwa anatosha kuwa kamanda wa UVCCM wilayani humo.
  KAMANDA wa UVCCM Mbeya Vijijini, ORAN NJEZA,(kulia),akizungumza na vijana wa UVCCM kata ya Santilya wilaya ya Mbeya, Jimbo la Mbya Vijijini, jana.
 Mkutano wa kampeni Jojo kata ya Santilya wilaya ya Mbeya.
 
MTAALAM aliyebobea katika masuala ya mifumo ya benki barani Afrika, Oran Njeza, amesema kuwa ajira nzuri iliyobaki kwa vijana wa kitanzania ni kilimo.

Hayo ameyasema jana Februari 8, mwaka huu, alipokuwa akizungumza na vijana wa kata ya Santilya wilaya ya Mbeya, Jimbo la Mbeya Vijijini wakiwa wanajiandaa kuelekea katika uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata hiyo, uliomalizika jana jioni.

Njeza, ambaye pia ni kamanda wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) UVCCM katika wilaya hiyo, alisema vijana wengi hawawezi kumwelewa kirahisi kwasababu ya mazoea.

‘’Najua wengi hamnielewi, lakini ajira nzuri Tanzania ni kilimo ambacho kwa hekali moja ukilima vizuri, kwa mwaka unaweza kupata Milioni mbili na zaidi, sifanyi utafiti maana mimi nimeacha kazi za benki Lagos nchini Nigeria sasa nalima, na nimelima karibia maisha yangu yote’’ alisema Njeza.

Akijibu maswali ya vijana hao ambao baadhi walihoji kuwa tatizo ni upatikanaji wa ardhi na masoko, alisema siyo kweli, kwasababu katika nchi ambayo haina tatizo la ardhi ni Tanzania. Ila vijana wengi wanachagua ardhi na wanataka kulima maeneo ya kwao tu, ila suala la soko alikiri kuwepo na tatizo hilo.

Aliwaonya vijana kote nchini, kujiepusha kuanzisha vurugu katika chaguzi mbaimbali kwa kutumiwa na wanasiasa ambao kiuhalisia hawawezi kubadilisha maisha yao kiuchumi bali wao wenyewe wanapaswa kutia bidii katika kufanya kazi.

‘’Taifa linapoharibika wanaoumia ni vijana kwa kutumika kwenye miparaganyiko na wanasiasa, kila mmoja ajiulize anawajibu gani kwa taifa maana ukitaka ushindi mzuri siyo magoli bali ni uchumi. Mimi nipo tayari kushirikiana kwa ushauri na yeyote anayetaka kujishughulisha katika kilimo ili kujikwamua kiuchumi’’alisema Njeza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...