Jumatano, 23 Septemba 2015

Shule tano za mkoa wa Mwanza zafungwa baada ya Kipindupindu kuua watu Nane


HADI sasa mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro, Singida na Mwanza, imekumbwa na kuathiriwa kwa kiasi kikubwa na ugonjwa wa kipindupindu ambao umeua watu kadhaa, ambapo hali inazidi kuwa mbaya katika maeneo mbalimbali nchini, hali iliyopelekea Shule nne za Msingi na moja ya Sekondari katika Kata ya Irugwa wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, zimefungwa kufuatia mlipuko wa ugonjwa huo kisiwani humo. 

Shule hizo ambazo ni za Buruza, Nabweko, Sambi na Kulazu, ambazo ni za msingi pamoja na shule ya Sekondari ya Irugwa, zimefungwa leo baada ya wanafunzi 22 wa shule za Msingi Nabweko kuambukizwa kipindupindu na watu wengine waliokuwa wanakusmbuliwa na ugonjwa huo. 

Diwani wa kata hiyo ya Irugwa, Juma Msongi ameithibitishia FikraPevu kwamba tangu ugonjwa huo ulipolipuka wiki iliyopita katika baadhi ya maeneo ya Kata hiyo, watu 8 wamefariki na hali inazidi kuwa mbaya kutokana na kukosekana kwa huduma madhubuti. 

Kwa mujibu wa diwani huyo, kutokana na hali ilivyo sasa wananchi wanatakiwa kuzingatia usafi wa mazingira ikiwemo matumizi sahihi ya kutumia vyoo na kujiepusha na ulaji ovyo wa vyakula.
FikraPevu inaendelea kufuatilia tukio hilo kwa karibu na kadri tutakapopata taarifa zaidi tutawataarifu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...