Alhamisi, 4 Juni 2015

MAKUSANYO YA KAHAWA MKOANI YASHUKA






MAKUSANYO ya zao la kahawa mkoani Mbeya yameshuka kutoka tani 340 mwaka juzi hadi kufikia tani 120 mwaka jana kutokana na mgogoro wa kimaslahi ulioibuka kati ya Shirikisho la Vikundi vya Wakulima wa Kahawa Tanzania, SHIVIWAKA na baadhi ya wadau wa zao hilo.

Mwenyekiti wa SHIVIWAKA, Edward Masawe, alisema hali hiyo ilitokana na kampuni moja ya ununuzi wa kahawa mkoani hapa kuwarubuni baadhi ya wakulima waliokuwa wanachama wao na kusababisha kutouza kahawa yao kwa shirikisho hilo.

Masawe, alitoa taarifa hiyo wakati wa mkutano Mkutano wa mwaka wa shirikisho hilo ulioambatana na uchaguzi mkuu wa viongozi wake.

Alisema mgogoro huo wa kimaslahi ulitokana na msimamo wa SHIVIWAKA wa kuwahamasisha wakulima kutokubnali kuuza kahawa yao kwa bei nafuu kwa wanunuzi wanaotaka kuwanyionya wakulima hivyo kusababisha baadhi ya wanunuzi hao kulichukia shirikisho hilo.

“Kimsingi changamoto hii imetuathiri kwa kiasi kikubwa katika ununuzi wa kahawa kutoka kwa wakulima kwani baadhi yao walikataa kuuza kahawa yao kwa SHIVIWAKA na kuwauzia wengine na kusababisha makusanyo yetu kushuka ktoka tani 340 hadi 120.” Alisema Masawe.

Baadhi ya wakulima wa kahawa walisema wakulima wengi bado hawana ufahamu mzuri wa kubaini ujanja unaofanywa na wanunuzi katika kuwanyonya haki zao hivyo wamewashauri kuwa makini katika uuzaji wa kahawa yao.

Neema Mwaogoma, mkulima kutoka Mbozi alisema wakulima wengi wana haraka ya kuuza kahawa yao ili kujipatia pesa za haraka lakini hawachunguzi kwa makini bei zinazotolewa na wanunuzi hao.

Akitoa mfano, Neema, alisema katika msimu uliopita baadhi ya wakulima waliouza kahawa yao kwa wanunuzi binafsi waliuza kwa bei ya kati ya shilingi 3,000 hadi 3,500 kwa kilo moja wakati SHIVIWAKA ilinunua kahawa hiyo kwa bei ya shilingi 5,000.

Kutokana na hali hiyo, Masawe, alisema SHIVIWAKA imeweka mikakati ya kuwashawishi wakulima wa kahawa kuliamini shirikisho hilo na kuendelea kuliuzia zao hilo badala ya wanunuzi binafsi.

Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja kufungua vituo vipya vua ununuzi wa kahawa katika maeneo ya wakuima, kuongeza bei ya zao hilo na kuimarisha mfumo wa uongozi wa shirikisho hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...