Alhamisi, 20 Novemba 2014

POLISI MBEYA JELA KWA KUMUUA MWANAFUNZI

  Huu ni mwili wa Marehemu kijana Daniel Mwakyusa mara baada ya kufanyiwa uchunguzi baada ya kuuawa, Daniel alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo cha TEKU Mbeya, aliuawa na askari alipokutwa Univesal Pub siku ya Valentine day 2013, akiwa na mwanamke aliyesadikiwa kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na askari Maduhu.



 Mwili wa mwanafunzi huyo kabla ya kuzikwa mara baada ya kuagwa na ndugu,jamaa na marafiki.Jeshi la polisi liligharamia shughuli za maziko ya mwanafunzi huyo na hapo ndipo shitaka likaanza kuunguruma mahakamani.
                             
                        HABARI KAMILI
MAHAKAMA Kuu kanda ya Mbeya imemhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa askari wa jeshi la polisi F 5842 DC Maduhu aliyekuwa akikabiliwa na shitaka la mauaji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji(TEKU) Daniel Mwakyusa.
Aidha mahakama hiyo pia imewaaachia huru washitakiwa wengine wawili wa kesi hiyo F 7769 DC Shaban na WP 6545 DC Neema baada ya kuwakuta hawana hatia.
Hukumu hiyo ya kesi namba 16 ya mwaka 2013 imetolewa leo(Nov 19) na jaji Rose Temba baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili.
Awali ilielezwa mahakamani hapo na mawakili wa serikali Archiles Mulisa akisaidiwa na Catherine Paul kuwa washitakiwa walifanya mauaji ya kukusudia mnamo Februari 14 mwaka 2012 kinyume cha kifungu namba 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.
Kwa mujibu wa Wakili Mulisa washitakiwa hao kwa pamoja walihusika na mauaji ya Daniel Mwakyusa baada ya kumpiga marehemu huyo kwa kutumia silaha inayodhaniwa kuwa ni bunduki nje ya ukumbi wa starehe ujulikanao Univesal uliopo Uyole jijini Mbeya.
Akitoa hukumu ya kesi hiyo,jaji Temba amesema mshitakiwa namba moja DC Maduhu anahusika moja kwa moja na mauaji hayo kutokana na ushahidi wa kimazingira ikiwamo yeye kuwa mtu wa mwisho kuondoka na marehemu eneo la tukio na kumpeleka kwenye gari,risasi tatu kupungua kwenye bunduki yake na pia kuwa mtu wa mwisho kurejesha silaha kituoni.
 
Credit;lyamba lya mfipa blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...