Jumatano, 19 Novemba 2014

MTOTO 1 KATI YA 9 WANAOZALIWA HAI TANZANIA NI NJITI


Vunja ukimya wa watoto njiti wa Tanzania!


Paza sauti yako kwa ajili yao!

 
Zaidi ya watoto 210,000 huzaliwa njiti Tanzania kila mwaka

Ni sawa na mtoto 1 kati ya kila watoto  9 wanaozaliwa hai Tanzania ni njiti

Watoto wachanga 9,400 hufariki kila mwaka kutokana na matatizo ya kuzaliwa njiti

Idadi hiyo ni sawa na karibu robo ya vifo vyote vya watoto wachanga 


 
Habari njema ni kuwa kuna njia rahisi zinazoweza kusaidia kuwaokoa wengi!
  •  matumizi ya njia za uzazi wa mpango;
  • uanzishaji mapema wa unyonyeshaji na unyonyeshaji maziwa ya mama pekee;
  • kuhakikisha watoto wanapewa joto la mwili hasa ngozi kwa mgozi baina ya mzazi na mtoto mchanga (njia hii inajulikana pia kama kangaroo mothercare);
  • uangalizi sahihi baada ya kuzaliwa, kujifungulia kwenye vituo vya afya na kuhakikisha mtoto anachunguzwa na wataalamu na kupata uangalizi sahihi baada ya kuzaliwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...