Jumatano, 24 Septemba 2014

SUDAN KUSINI WANUSURIKA NA BAA LA NJAA

Jamii ambazo hazikuathirika na mapigano Sudan Kusini zilipanda vyakula
Sudan Kusini imeepuka baa la njaa lakini ukosefu wa chakula wasalia kuwa suala nyeti hasa mwakani.
Weledi wa masuala ya mlo wameonya kwamba watu wengi wataathirika na njaa endapo hatua za dharura hazitachukuliwa mara moja kuchanga fedha na kusambaza vyakula nchini humo.
Ripoti ambayo imetolewa hivi punde na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali nchini Sudan Kusini inasema kuwa ingawa hali ya chakula imeanza kuimarika hasa msimu huu wa mavuno, kuendelea kwa vita kumemaanisha sekta ya kilimo iliathirika na hali ilivyo sasa ni mbaya zaidi ikilinganishwa na miaka mingine.

Maeneo ambayo hayajashuhudia vita yamechangia kuzalisha chakula nchini humo.
Licha ya hayo, imekadiriwa kuwa watu milioni moja u nusu wanakumbwa na ukosefu wa chakula.
Idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka maradufu ifikapo mwaka ujao endapo hatua za dharura hazitachukuliwa kukabiliana na utapia mlo na njaa.
Ripoti hiyo imetolewa na mashirika 14 yanayofanya kazi nchini Sudan Kusini yakiwa pamoja na Umoja wa Mataifa.
Chanzo; BBC/SWAHILI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...