Jumamosi, 23 Agosti 2014


Shule waliyosoma Rais Joseph Kabila (wa DRC), Assah Mwambene yachakaa vibaya!

Posted By - (2656) Views
SHULE ya Sekondari ya Irambo inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), iliyopo katika Wilaya ya Mbeya Vijijini inakabiliwa na tatizo la uchakavu wa miundombinu ya majengo hali inayotajwa kufanyiwa ukarabati ili kuendana na hadhi ya shule hiyo. 


Shule hiyo inatwajwa kuongoza kutoa matokeo bora ya kitaaluma tangu kuanzishwa kwake, ambapo pia shule inatwajwa kuwa ndiyo waliyosoma viongozi maarufu Nchini Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assa Mwambene na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Irambo
Uchunguzi uliofanywa na FikraPevu leo Agosti 19, 2014 mkoani humo umebaini kuwa licha ya viongozi hao kusoma shuleni hapo, ufaulu wa shule hiyo umeshuka kwa kiwango kikubwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali. 



Makamu Mkuu wa shule hiyo, Aliko Mwanjala, amebainisha kuwa shule hiyo haina miundombinu ya kutosha licha ya kuwa na uhaba wa vifaa vya kufundishia huku akisema hali ya majengo ya shule hiyo kuwa sio rafiki. 




Amesema awali shule hiyo ilikuwa ni shule ya mfano kitaaluma na kimalezi katika mkoa wa Mbeya na kuwa juhudi za kuinusuru na kuiinua kupitia kwa wadau mbalimbali wakiwemo wanafunzi waliowahi kusoma katika shule hiyo bado zinaendelea. 



Mmoja wa watu waliowahi kusoma katika shule hiyo akiwemo Sambwee Shitambala, ambaye sasa ni Mwanasheria alikaririwa na FikraPevu akisema “Nitajitahidi kuwashirikisha wenzangu kuhusu hali hii naona majengo yamechakaa sana tofauti na tulivyokuwa tunasoma hapa kikiwemo jingo lenye chumba alichokuwa analala, Rais Kabila”.

Madarasa

Sehemu ya madarasa ya Shule ya Irambo
 
 
Hata hivyo, amebainisha kuwa hapo awali shule hiyo ilikuwa inatumimiw ana watu wengi waliokuwa wakiwekwa kwa ajilio ya kufanya kazi kwenye idara nyeti za serikali na hivyo kuwataka watu wote waliosoma katika shule hiyo kwende shuleni hapo na kutoa misaada ya kuikarabati shule hiyo.
Darasa la Kabila
Chumba ambacho kilikuwa bweni ambalo, Rais Joseph Kabila, wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), alikuwa akikitumia kwa ajili ya kulala kwa sasa hili ni darasa la kidato cha pili, aliyesimama ni mwandishi wa habari Gordon Kalulunga
 
 
Taarifa za ndani kutoka kwa wanafunzi waliosoma katika shule hiyo waliopo katika maeneo mbalimbali nchini, wameidokeza FikraPevu kuwa mwanzoni mwa mwezi Septemba, 2014 wanakusudia kutoa misaada mbalimbali kwa ajili ya shule hiyo kupitia kikundi ambacho hawajapenda kukiweka wazi kilicho mbioni kusajiliwa kwa ajili ya shule hiyo.

CHANZO; FIKRA PEVU YA JF

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...