Jumatano, 26 Machi 2014

FISTULA YAENDELEA KUDHIBITIWA MBEYA

Bingwa wa magonjwa ya Akinamama pamoja na Uzazi Dr. John Frances akifafanua jambo juu ya ugonjwa wa Fistula katika hospitali ya wazazi Meta Jijini Mbeya.

Baadhi ya wagonjwa wa Ugonjwa wa Fistula toka maeneo mbalimbali ya mkoa wa mbeya ambao wamelazwa katika hospital hiyo kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
IDADI ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa ugonjwa fistula katika Hospital ya Rufaa Mbeya kitengo cha Wazazi (META) na vituo vingine vya afya katika jiji la Mbeya imeendelea kupungua mwaka hadi mwaka.

Bingwa wa Magonjwa ya Akina mama na Uzazi ambaye pia ni Mkuu wa Hospital ya Wazazi Meta, Dr. Frances John amethibitisha jambo hilo.

Amesema kupungua kwa ugonjwa huo, kunatokana na juhudi za serikali na wadau katika utoaji wa elimu na upatikanaji wa matibabu yenye uhakika.

Katika Hospital hiyo wanahakikisha wanadhibiti ugonjwa huo hasa kwa mama ambaye anataka kujifungua na wapo madaktari Bingwa pamoja na vifaa vya kutosha.

Dr. Frances, amewataka akina mama wajawazito kuhakikisha wanahudhuria kliniki pamoja na kujifungulia katika vituo vya Afya vilivyo karibu na maeneo yao ili kuepuka maradhi hayo.

Amefafanua kuwa, asilimia kubwa ya wajawazito wanaopata ugonjwa huo wamekuwa wakikaa na uchungu  kwa muda mrefu bila kuhudhuria katika vituo vya afya kitendo ambacho kimechangia kuwepo kwa hali hiyo.

Ametoa wito kwa Madaktari ambao wamesomea magonjwa ya akina mama kuhakikisha wanawasaidia akina mama ambao wanasumbulia na ugonjwa huo kwani  ni ugonjwa wenye kutia aibu  ambao pia umechangia kwa asilimia kubwa kuwepo kwa manyanyaso  ndani ya familia zao pamoja na jamii kuwatenga. 

 Dalili za ugonjwa huoni  maumivu, kutokwa haja kubwa laini bila mgonjwa kujitambua, hivyo kuchafua nguo hivyo hali hiyo humsababishia mgonjwa msongo wa mawazo, kutokujiamini na adha katika jamii kutokana na kutoa majimaji hayo ya choo ambayo huwa na harufu mbaya.
Credit; jamiimoja.blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...