Jumanne, 2 Januari 2018

DIWANI WA CHADEMA MBEYA ASIFU UTENDAJI WA RAIS MAGUFULI, MHE MWANJELWA AONGOZA MAOMBI KWA AJILI YA RAIS NA SERIKALI

Diwani wa Kata ya Sinde Mkoani Mbeya Mhe Newton Mwakijobe akizungumza mbele ya waumini wakati wa ibada ya Mwaka Mpya iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Jana Januari Mosi, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiongoza waumini wa kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli na serikali yake wakati wa ibada ya Mwaka Mpya, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisalimiana na Diwani wa Kata ya Sinde Mkoani Mbeya Mhe Newton Mwakijobe wakati wa ibada ya Mwaka Mpya iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Jana Januari Mosi, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiongoza waumini wa kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli na serikali yake wakati wa ibada ya Mwaka Mpya, 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akiongoza waumini wa kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli na serikali yake wakati wa ibada ya Mwaka Mpya, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya

Diwani wa Kata ya Manda Wilaya na Mkoa wa Mbeya Mhe Newton Mwakijobe amesifu Utendaji wa serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwatetea wanyonge huku akisimamia nidhamu na uwajibikaji kazini.

Diwani Huyo ametoa pongezi hizo wakati akitoa salamu wakati wa ibada ya Mwaka Mpya iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya.

Katika ibada hiyo iliyohudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa, Diwani Huyo amesifu zaidi usimamizi madhubuti wa rasilimali za Taifa unaofanywa na Rais Magufuli ambao utawanufaisha wananchi wote si MTU mmoja mmoja.

Mhe Mwakijobe pia amempongeza Rais Magufuli kwa kumchagua Mhe Mwanjelwa katika serikali yake kuwa Naibu Waziri anayeshughulikia sekta ya Kilimo jambo ambalo limeonyesha chachu na hamasa ya kuwakumbuka wakazi wa Mbeya Mjini kwa kupata Waziri wa kwanza tangu nchi ilipopata Uhuru.

Aidha, Mhe Mwakijobe alimsihi Mhe Mwanjelwa kumfikishia salamu Rais Magufuli ikiwa ni pamoja na kumuomba kuzuru Mkoani Mbeya katika ziara yake ya kikazi ili kuzungumza na wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambao wanatambua majukumu makubwa na mazito anayoyafanya kwa manufaa ya wananchi wote.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo aliongoza waumini wa kanisa la Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) kumuombea Rais Magufuli sambamba na serikali kwa ujumla ili wananchi waendelea kujivunia matunda ya kiongozi Huyo makini na shupavu.

Mhe Mwanjelwa Alisema kuwa maombi hayo ni kwa ajili ya kumshukuru Mungu, kwa kuwawezesha kumpata Rais John Magufuli, ambaye amekuwa akiibua na kufichua maovu mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka nchini.

Aliongeza kuwa, juhudi alizozionyesha Mhe Rais Magufuli zinafaa kuungwa mkono na jamii yenye hofu na Mungu kwani ndani yake kuna mtihani mgumu unaohitaji kumuweka kwenye maombi ya wananchi ya kila siku katika sehemu yeyote iwe kazi na hata majumbani.

Kanisa hilo pia limefanya ibada maalumu kwa ajili ya Mhe Mwanjelwa ili awe kiongozi shupavu mwenye maono na utendaji uliotukuka katika serikali na aweze kuwa muwakilishi mzuri wa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na Taifa kwa Ujumla wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...