Jumapili, 20 Julai 2014

NDOO ZA MSUMBIJI MARUFUKU KUNUNULIA MPUNGA KYELA

NDOO zinazotoka nchini Msumbiji, zimepigwa marufuku kununulia mpunga katika kata ya Ipande,wilayani Kyela mkoani Mbeya, kutokana na ndoo hizo kuwa na ujazo mkubwa.

Marufuku hiyo imepgwa na Halmashauri ya  Chama Cha Mapinduzi(CCM), Ipande, na kwamba atakayekutwa akinunulia ndoo hizo au kuwapeleka watu kununua mpunga kwa kutumia ndoo hizo, atatozwa faini ya Tsh.20,000/=

Diwani wa kata hiyo, Steven Mwangalaba, amethibitisha na kwamba, wao hawakatazi mtu kununua mpunga wala kuuza, bali wanazikataa ndoo hizo kwasababu zinawanyonya wakulima.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...