Jumatatu, 21 Aprili 2014

DC CHANG'A AFARIKI DUNIA

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, Moshi Chang’a enzi za uhai wake akifafanua jambo. Picha na Maktaba 

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, Moshi Chang’a amefariki dunia. Kiongozi huyo alifariki dunia jana saa 10: 15 jioni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya siku 20.
Ofisa Habari wa hospitali hiyo, Aminieli Aligaesha alisema DC Chang’a alifika hospitalini hapo Machi 29, mwaka huu akiwa anaumwa na kulazwa.
Alisema madaktari wamekuwa wakimpatia matibabu, lakini ilipofika jana saa 9:30 alasiri hali yake ilibadilika ghafla.
“Walijitahidi kuokoa uhai wake bila mafanikio na ilipofika saa 10: 15 alikata roho, alisema Aligaesha huku akikataa kueleza tatizo lililokuwa linamsibu.
“Huyu ni kiongozi wa Serikali, bila shaka wakubwa huko serikalini wataeleza zaidi kuhusu kifo hicho,” alisema.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia alithibitisha kutokea kwa kifo hicho mchana wa jana, baada ya kiongozi huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Alisema amemwagiza katibu wake (wa waziri) na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya kufuatilia na kushughulikia msiba huo na taarifa zaidi kuhusu utaratibu zitapatikana leo baada ya kuzungumza na familia.
Chang’a kabla ya kuhamishiwa katika Wilaya ya Kalambo alikuwa DC wa Wilaya Mpya ya Mkalama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...