Jumanne, 29 Aprili 2014

BULEMBO: BIMA YA MOTO SHULE ZA WAZAZI TANZANIA NI LAZIMA



  Mwenyekit wa Jumuiya ya wazazi(CCM) Taifa, Abdallah Majura Bulembo, akimkabidhi Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Ivumwe Jijini Mbeya, Dr. Victoria Kanama, kiasi cha Shilingi Milioni tatu (Tsh. 3,000,000/=) kwa ajili ya ukarabati wa mabweni ya wavulana wa shule hiyo, yaliyoteketea April 23, mwaka huu.
  Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi(CCM) Taifa, Abdallah Majura Bulembo, akiwapa pole wanafunzi wa Sekondari ya Ivumwe, Jijini Mbeya jana, baada ya shule hiyo kupata janga la moto ulioteketeza mabweni saba ya wavulana wa shule hiyo, April 23, Mwaka huu na kusababisha hasara ya Milioni 30.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ivumwe Jijini Mbeya jana.
 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi(CCM) Taifa, Abdallah Majura Bulembo(kulia), akiwa anakagua moja ya bweni la wavulana wa shule ya Sekondari Ivumwe Jijini Mbeya jana, baada ya shule hiyo kupata janga la moto.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania(CCM), Abdallah Majura Bulembo, ameamuru shule zote zinazomilikiwa na jumuiya hiyo kote nchini kukata bima ya moto.

Agizo hilo alilitoa jana mjini Mbeya, alipokuwa akikagua uhalibifu uliojitokeza baada ya janga la moto kuteketeza mabweni saba ya wavulana katika shule ya Sekondari Ivumwe, iliyopo Jijini hapa.

Alisema katika bima ambazo ni rahisi na bei nafuu nchini ni bima ya moto, lakini ndiyo bima pekee ambayo haikatwi na wananchi na taasisi nyingi.

“Kuanzia sasa, suala la bima ya moto ni la lazima kwa shule zote za jumuiya ya wazazi wa CCM Tanzania. Baraza kuu tutakutana kwa dharula mjini Dodoma Mei 17, mwaka huu na tutakachokipata tutakileta haraka kwenu ili kusaidia katika janga hili la moto’’ alisema Bulembo.

Mbali na agizo hilo, aliwapa pole wanafunzi waliounguliwa na vitu vyao vyote na kuwataka wawe wavumulivu, pia alitoa mchango wa Milioni tatu (3,000,000/=)kwa ajili ya ukarabati wa mabweni hayo na mahitaji mengine ya haraka na kuahidi kuwashirikisha wadau wengine wa elimu ili kuwasaidia wanafunzi waliokuwa wakiishi kwenye mabweni hayo.

Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dr. Victoria Kanama, alimshukuru Mwenyekiti huyo wa wazazi Taifa na kwamba kutokana na mchango wake, mabweni hayo yatakamilika ndani ya mwezi mmoja.

“Umetupa nguvu sana na tutahakiisha tunakarabati mabweni haya ndani ya mwezi mmoja na kufanya jitihada za kuongeza ufanisi wa ufaulu katika shule yetu kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita” alisema Dr. Kanama.

Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo ya Ivumwe, Emerry Muhondwa alisema janga la moto lilitokea April 23, mwaka huu majira ya saa 3 hadi saa 4 asubuhi wakati wanafunzi wapo madarasani.

“Mabweni saba ya wavulana ndiyo yaliteketea na moto uliteketeza Vitanda 93, Magodoro 186, mashuka 372, Mablanketi 186, mabegi 186, matranker 186 pamoja na vitabu na madaftari, vyote vikiwa na jumla ya Milioni 30’’ alisema Mwalimu Mohondwa.

Katika taarifa yake kwa Bulembo, mkuu huyo wa shule alisema kwa sasa wanafunzi hao wanalala katika madarasa na wameazima magodoro katika shule ya wasichana ya Loleza ya Jijini hapa.

Ivumwe, ni kati ya shule zenye sifa ya kufaulisha, ambapo katika mtihani wa utamilifu(Mock), kidato cha sita mwaka huu, shule hiyo imeshika nafasi ya pili kati ya shule 26 zilizokuwa na watahiniwa 30 katika kanda ya Nyanda za juu kusini mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...