Jumatatu, 21 Aprili 2014

ASKARI AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUIBA MTOTO WA UMRI WA SIKU SABA

ASKARI wa Jeshi la Polisi aliyefahamika kwa jina la Prisca Kilwai mwenye namba WP 5367 wa Ilala Jijini Dar es Salaam amekamatwa kwa tuhuma za wizi wa mtoto  
Baba Mzazi  wa mtoto aliyeibiwa  Salehe Issah Mwangosi(31) ndiye alieshirikiana na polisi huyo kumwiba mtoto

 Mboka Mwakikagile(20) mama mzazi wa mtoto aliyeibwa



ASKARI wa Jeshi la Polisi aliyefahamika kwa jina la Prisca Kilwai mwenye namba WP 5367 wa Ilala Jijini Dar es Salaam amekamatwa kwa tuhuma za wizi wa mtoto jinsi ya kiume aliyefahamika kwa jina la Goodluck Salehe(siku 7) aliyeibwa April 6 mwaka huu huko Kasumulu Kata ya Itope Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya.

Mtoto alizaliwa Machi 30 na alipoibiwa alikuwa na umri wa siku sita ambapo mtuhumiwa alishirikiana na Baba Mzazi aliyefahamika kwa jina la Salehe Issah Mwangosi(31) mkazi wa Matankini Kyela aliyemtambulisha kwa mama mzazi aliyefahamika kwa jina la Mboka Mwakikagile(20) kuwa Prisca ni shangazi yake Salehe hivyo anakuja kumwona mtoto aliyezaliwa.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ahmed Msangi amethibitisha kukamatwa kwa Askari huyo ambapo amesema kuwa ikithibitika kutenda kosa hilo atafikishwa mahakama ya kijeshi na baada ya taratibu hizo kukamilika atafikishwa Mahakamani ili kujibu tuhuma zinazo mkabili.

Mtuhumiwa amekamatwa April 17 mwaka huu huko eneo la Meta Jijini Mbeya majira ya saa nne asubuhi akiwa na mtoto huyo mkononi ambapo alitiwa nguvuni na kufikishwa makao makuu ya Polisi Mkoa Forest ya Zamani kwa mahojiano zaidi.

Msangi amesema kuwa Salehe na Prisca hawana mahusiano ya Damu ila wana mahusiano ya kibiashara ambapo wanaendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo wakabili.
 
 

MTOTO ALIYEIBWA AKABIDHIWA KWA WAZAZI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi akimkabidhi kwa mama yake mzazi mtoto Goodluck mara baada ya kupatikana

Akipokea Mtoto wake Mama mzazi Mboka Mwakikagile(20) amelishukuru Jeshi la polisi na wananchi wema kwa kufanikisha kupatikana kwa mtoto wake  Goodluck Salehe aliyeibwa na Askari wa Jeshi la Polisi WP 5367 Prisca Kilwai April 6, mwaka huu huko Kasumulu wilayani Kyela.


 Mtoto  Goodluck Salehe 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi,akizungumza baada ya kukabidhi mtoto huyo aliwasihi wazazi kuwa makini na utunzaji wa watoto ili kuepuka vitendo kama hivyo kujirudia.





Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi akizungumza na shangazi wa mtoto aliyeibiwa pembeni ni baadhi ya waandishi wa habari walioshuhudia makabidhiano hayo




BAADA ya Jeshi la Polisi mkoani Mbeya  kumtia nguvuni Askari wake anayetuhumiwa kuiba mtoto wilayani Kyela,Mtoto huyo akabidhiwa kwa wazazi wake huku wakiendelea na uchunguzi zaidi.
Makabidhiano hayo yamefanyika   katika Hospitali ya Wazazi Meta alikokuwa akipatiwa matibabu mtoto huyo katika chumba cha Joto na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi.
Akipokea Mtoto wake Mama mzazi Mboka Mwakikagile(20) amelishukuru Jeshi la polisi na wananchi wema kwa kufanikisha kupatikana kwa mtoto wake  Goodluck Salehe aliyeibwa na Askari wa Jeshi la Polisi WP 5367 Prisca Kilwai April 6, mwaka huu huko Kasumulu wilayani Kyela.
Aidha mwanamke huyo amemshukuru zaidi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi pamoja na Askari wengine  waliofanikisha mtoto wake kupatikana akiwa hai.
Baadhi ya ndugu waliofurika katika Hospitali ya Meta kushuhudia makabidhiano hayo wamesema hawaamini  kile kilichotokea baada ya kuwa katika hofu takribani siku kumi na moja baada ya kuibwa katika zahanati ya Njisi iliyopo Kasumulu Kyela.
Aidha ndugu hao wamelipongeza Jeshi la Polisi kwa kufanikisha kupatikana mtoto na wasamaria wote walioshirikiana nao katika maombi hata kufanikisha upatikanaji wa mtoto huyo akiwa salama salimini.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi,akizungumza baada ya kukabidhi mtoto huyo aliwasihi wazazi kuwa makini na utunzaji wa watoto ili kuepuka vitendo kama hivyo kujirudia.
Ameongeza kuwa Jeshi la polisi bado linafanya upelelezi na kukusanya ushahidi zaidi ili waweze kuwafikisha mahakamani watumiwa kujibu mashtaka wanayokabiliana nayo.
Amesema Mtoto huyo alipatikana Aprili 17, mwaka huu akiwa na Askari huyo majira ya saa nne asubuhi  na kuongeza kuwa mpaka sasa sababu za kuiba mtoto huyo hazijafahamika na atafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya kuhukumiwa kijeshi.

Na Mbeya yetu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...