Jumatatu, 24 Februari 2014

PRISON YAZOA MASHABIKI MBEYA, KUPOKELEWA KESHO KUTWA J5.


TIMU ya soka ya Tanzania Prison(wajelawajela) ya Jijini Mbeya, imeandaliwa mapokezi mazito baada ya mashabiki kuridhishwa na kiwango cha wachezaji wake.

Mapokezi hayo yatafanyika kesho kutwa Jumatano eneo la Oil Com Uyole Jijini hapa, huku mashabiki kadhaa wakifika katika ofisi za Jiji la Mbeya kuomba vibali vya kufungua matawi ya timu hiyo.

Mjumbe wa kamati tendaji ya timu hiyo Mohamed Lalika, amethibitisha kuwepo kwa mapokezi hayo na kwamba wanawakaribisha mashabiki wa timu zingine ambao waliasi.

‘’Kama ilivyo kauli mbiu yetu kuwa tumejipanga hatoki mtu, hivyo wale wote waliopotea wanaruhusiwa kurudi kushabikia timu yao halisi bila masharti yeyote’’ alisema Lalika.

Naye mwanachama wa Yanga Christopher Nyenyembe ambaye amesema kuwa ni shabiki  timu ya Prison, alisema timu hiyo ina umbo la timu.

‘’Mimi ni shabiki mkubwa wa timu ya Prison na nitaendelea kuwa shabiki kwasababu timu hiyo ina umbo la timu tofauti na timu ya Mbeya City ambayo wachezaji hawachezi kama timu bali kila mmoja anacheza kwa uwezo wake’’ anasema Nyenyembe.

Ayas Yusuph(Asia), mkazi wa Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini, alisema kuwa katika eneo la Mbalizi tayari wamefanya uchaguzi wa tawi la timu hiyo kwa lengo la ushindani.


Shabiki wa muda mrefu wa timu hiyo Jijini hapa, Herode Mdoe, alisema katika ligi kuu kuna timu Nne pekee ambazo zina mfumo wa timu ambazo ni Tanzania Prison, Mtibwa, Azam na Coast Union.


Aidha alichangia mfuko mmoja wa saruji kwa ajili ya ujenzi wa tawi la Mbeya Peack ambalo linaongozwa na Christopher Nyenyembe ambaye kitaaluma ni Mwandishi wa Habari.

Wakielezea mafanikio ya timu hiyo na juhudi zinazofanywa na uongozi wa Prison, shabiki Emmanuel Baganda(Swahida) na Adamu, alisema kuwa siri kubwa ni kutokana na Mwalimu David Mwamwaja kusikiliza ushauri kwa kila mtu bila dharau.
 
Credit;kalulunga blog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

NAIBU WAZIRI WA KILIMO MHE MWANJELWA AMUAGIZA MRAJIS KUFANYA UCHUNGUZI SACCOS YA MADIBIRA-MBARALI NDANI YA SIKU 14

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na kamati ya uli...