Wabunge
 wa Bunge la Kumi na Moja wamewachagua Wenyeviti wa tatu wa Bunge ambao 
watasaidiana na Spika wa Bunge na Naibu Spika katika kuliongoza Bunge la
 Kumi na Moja katika kipindi cha Nusu ya Uhai wake.
Waliochaguliwa
 ni Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo Mhe. Andrew Chenge (MB), 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dr Mary 
Mwanjelwa (MB) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Katiba 
Mhe.Najma Giga (MB).
Akizungumza
 kabla ya uchaguzi wa Wenyeviti hao Katibu wa Bunge Dkt Thomas 
Kashililah alisema Kamati ya Uongozi iliwapitisha Wabunge watatu 
kugombea nafasi hizo tatu za Uenyekiti wa Bunge.
Dkt
 Kashililah alisema kwa kuwa Wagombea waliopitishwa ni watatu na kwa 
kuwa nafasi zilikuwa tatu hivo Bunge lilikuwa na kazi ya kuwadhibitisha.
Hivyo
  Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai aliwaita Wagombea wote watatu kujinadi 
mbele ya Bunge kabla ya kupigiwa kura ya pamoja ya Ndio au Hapana.
Ambapo
 Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo Mhe. Andrew Chenge (MB), 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dr Mary 
Mwanjelwa (MB) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Katiba 
Mhe.Najma Giga (MB) walichaguliwa kwa kura nyingi za Ndio kuwa Wenyeviti
 wa Bunge.

 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni