Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa ofisini kwake,mganga mkuu wa gospitali 
ya Makandana Stanfod Mwakatage alilitaja jengo la wagonjwa wa nje 
kuezuliwa paa na kusababisha maji ya mvua kulowanisha vifaa kwenye 
chumba cha wagonjwa mahututi.
 Dk.Mwakatage alisema katika  vifaa vilivyolowa maji ni pamoja na mashine
 mbalimbali zenye gharama kubwa ambazo haijafahamika iwapo zimeharibika 
au la kwani ilikuwa vigumu kuziwasha kwa hofu ya kuziharibu zaidi iwapo 
maji yaliingia kwa ndani.
 “Ni vigumu kujua iwapo vimeharibika kwani tunaogopa kuviunganisha katika
 umeme vinaweza kuharibika iwapo maji yaliingia kwa ndani.
Tunasubiri 
upite muda wa kutosha ndipo tuanze kujaribu na hapo tutaweza kujua iwapo
 mashine hizi zimeharibika”
“Ni mashine za mamilioni kwakweli itakuwa hasara kubwa iwapo zitakuwa 
zimeharibika kwa kuingiza maji.
Lakini uhakika tutaupata tukizijaribu”
Alisemaa pia majui yaliyoingia kupitia paa lililoezuliwa pia yaliweza 
kuathiri chumba cha kumbukumbu kwa kulowanisha majalada kati ya 100 na 
150 yaliyokuwa ndani ya chumba hicho. 
Alisema ni muhimu chumba hicho kikaezekwa haraka kutokana na umuhimu 
wake hospitalini hapo na kubainisha kuwa jitihada mbalimbali zimekwisha 
anza kuchukuliwa ili kukirejesha katika hali yake ya kawaida.
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni